“WANANCHI WA MUHEZA WAHAMASIKA KUJIUNGA NA MFUKO WA AFYA YA JAMII, ZAIDI YA KAYA 65 ZENYE WANACHAMA 390 WAHAMASIKA NA KUJIUNGA PAPO HAPO”

November 10, 2014
 Mkuu wa wilaya ya Muheza,Subira Mgalu akisisitiza jambo wakati uzinduzi wa kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya Jamii(CHF) kwenye kata ya Potwe wilayani Muheza uliofanyika
leo ambapo zaidi ya kaya 65 zenye wanachama 390 walihamasiska na kujiunga paoo hapo.


 MAAFISA wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) wahamasika kwenye zoezi hilo na kuamua kuwalipia wanafunzi wa shule za msingi wapatao 80 kwenye Kata ya Potwe wilayani Muheza wanaoishi kwenye mazingira magumu wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya Jamii (CHF) wilayani humo ambapo zoezi hilo linaendelea kwa muda wa siku kumi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)
wilayani Muheza George Mhada kushoto akipokea fedha kutoka kwa Diwani wa Kata ya
Potwe katikati Rashid Mdachi  anayeshuhudia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza,Subira Mgalu wakati wa uzinduzi wa uhamasishaji wa wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya Jamii(CHF) wilayani humo ambapo zaidi ya kaya 65 zenye wanachama 390 zilifanikiwa kujiunga.

Afisa wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)kutoka Makao
Makuu Isaya Shekifu wa pili kulia akifuatilia uandikishwaji wa wanachama wapya wa mfuko wa afya ya Jamii(CHF) leo wakati wa uzinduzi wake uliofanyika Kata ya Potwe wilayani Muheza wa kwanza kulia ni Afisa Tabibu wa Zahanati ya Potwe kulikofanyika uzinduzi huo,Dr.Swalehe Mudhihiri ambapo zaidi ya kaya 65 zenye wanachama 390 zilifanikiwa kujiunga.


Mkuu wa wilaya ya Muheza, Subira Mgalu na wafanyakazi wa mfuko wa Bima ya Afya mkoani Tanga,viongozi wa Kata ya Potwe na wanafunzi wa shule ya msingi kwenye Kata hiyo leo ambapo zaidi ya kaya 65 zenye wanachama 390 zilifanikiwa kujiunga.

Wananchi kutoka sehemu mbalimbali kwenye Kata ya Potwe wilayani Muheza wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Muheza ambaye hayupo pichani wakati wa uzinduzi wa uhamasishaji wa wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii(CHF) leo ambapo zaidi ya kaya 65 zenye wanachama 390 walihamasika na kujiunga papo hapo.

Mkuu wa wilaya ya Muheza Subira Mgalu kushoto akipokea risiti ya malipo mara baada ya kujiunga kuwa mwanachama wa mfuko wa afya ya Jamii (CHF) leo wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo iliyofanyika kwenye Kata ya Potwe wilayani humo anayemkabidhi risiti hiyo ni Afisa Tabibu wa Zahanati ya Potwe
wilayani humo Dr.Samweli Mudhihiri ambapo zaidi ya kaya 65 zenye wanachama 390 walihamasika na kujiunga papo hapo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »