UBALOZI WA TANZANIA WASHINGTON, DC WAMKARIBISHA BALOZI OMBENI SEFUE KWA CHAKULA CHA JIONI

October 09, 2014


Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akiwasili kwenye Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Washington, DC nchini Marekani alikokaribishwa chakula cha jioni wakiwemo viongozi mbalimbali wa Wizara ya Fedha na Benki Kuu ya Tanzania. Mhe. Ombeni Sefue ndiye aliyewezesha ununuzi wa jengo hilo la Ubalozi wakati alipokua Balozi wa Tanzania nchini Marekani mwaka 2007
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula akimpokea Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue siku ya Jumatano Oct 8, 2014 siku Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani ulipomkaribisha chakula cha jioni wakiwemo viongozi mbalimbali wa Wizara ya Fedha na Benki Kuu ya Tanzania.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akiongea mawili matatu na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dr. Servacius Likwelile.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akisalimiana na Naibu Gavana Dr. Natu Mwamba.
Mkuu wa Utawala na Fedha Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mama Lily Munanka akiongea machche na baadae kumkaribisha Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula.
Mhe. Liberata Mulamula akimkaribisha Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue na kumshukuru kwa kuwezesha upatikanaji wa jengo hilo la Ubalozi.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akimshukuru Balozi Liberata Mulamula na kuelezea ununuzi wa Jengo hilo ulivyofanyika yakiwemo majengo mengine ya Ubalozi Canada na New York huku akisema ni jambo jema kwa Serikali kuangalia uwezekano wa kununua majengo ya Ubalozi na makazi ya maafisa wake badala ya kukodisha kwani kufanya hivyo kunapunguza gharama kwa kiasi kikubwa sana yeye aliliona hilo ndio maana alipendekeza na hatimae kuwezesha ununuzi wa majengo hayo.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akijichukuli chakula.
Wageni wakiendelea kupata chakula cha jioni. Picha na Vijimambo Blog.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »