YANGA TUNAWASUBIRI MOROGORO KUWAPA KICHAPO: MTIBWA SUGER

September 02, 2014


N a Fadharkidev Blog
KOCHA wa Mtibwa Sugar Mecky Mexime,amesema kikosi chake kimejiandaa kuitoa nishai Yanga katika mchezo wa ufunguzi utakaochezwa Septemba 20 kwenye uwanja wa Jamhuri Morogoro.

Mexime aliyewahi kufundishwa na kocha wa Yanga Mbrazili Marcio Maximo wakati huo akiwa kocha wa ‘Taifa Stars,alisema namuheshimu kocha huyo lakini hatokubali kuona timu yake ikipoteza mchezo huo wa ufunguzi tena mbele ya mashabiki wao.

“Hatukuwa na matokeo mazuri sana msimu uliopita lakini kwa sasa tumejipanga kuhakikisha tunarekebisha kasoro zutu ndiyo maana tumefanya usajili mzuri ambao ninaimani tutapata matokeo ya ushindi kuanzia mchezo wetu wa kwanza dhidi ya Yanga,”alisema Mexime.

Yanga ambayo itaanzia ugenini dhidi ya Wakata miwa hao wa Manungu wanabidi kujipanga kwani hawana matokeo mazuri katika uwanja huo wa Jamuhuri katika kipindi cha misimu mitatu iliyopita zaidi ya kuambulia kipigo na sare.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »