Afisa
Mazingira kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Emmanuel Shija
akiwasilisha mada kuhusu ‘Uchimbaji mdogo wa Madini na Mazingira’ wakati
wa semina ya mafunzo kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya
Ziwa. Semina hiyo ya siku nne inafanyika jijini Mwanza (Septemba 1-4,
2014) na imeandaliwa na Kitengo cha Mazingira cha Wizara husika.
Katibu
Mtendaji wa TAREA (Tanzania Renewable Energy Association) Tawi la Kanda
ya Ziwa, Bw. Jacob Ruhonyora akizungumzia uzoefu wake kuhusu faida za
matumizi ya nishati jadidifu,kwa Wajumbe wa semina ya mafunzo ya mambo
ya mazingira inayoendelea jijini Mwanza kuanzia Septemba 1, 2014. Semina
hiyo ya siku nne imeandaliwa na Kitengo cha Mazingira cha Wizara ya
Nshati na Madini.
Afisa
Mazingira kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Nassor Abdullatif
(Kushoto), akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa kufanya Tathmini ya
Mazingira (Environmental Impact Assessment – EIA) kabla ya kuanza
utekelezaji wa mradi wowote katika siku ya pili ya semina kwa Maafisa
Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa, inayofanyika jijini Mwanza
Septemba 1 – 4, 2014.
EmoticonEmoticon