NISHATI NA MADINI WAIMARISHA MKAKATI WA UTUNZAJI MAZINGIRA

September 02, 2014
day 2 - pic 1Afisa Mazingira kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Emmanuel Shija akiwasilisha mada kuhusu ‘Uchimbaji mdogo wa Madini na Mazingira’ wakati wa semina ya mafunzo kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa. Semina hiyo ya siku nne inafanyika jijini Mwanza (Septemba 1-4, 2014) na imeandaliwa na Kitengo cha Mazingira cha Wizara husika.

day 2 - pic 2Katibu Mtendaji wa TAREA (Tanzania Renewable Energy Association) Tawi la Kanda ya Ziwa, Bw. Jacob Ruhonyora akizungumzia uzoefu wake kuhusu faida za matumizi ya nishati jadidifu,kwa Wajumbe wa semina ya mafunzo ya mambo ya mazingira inayoendelea jijini Mwanza kuanzia Septemba 1, 2014. Semina hiyo ya siku nne imeandaliwa na Kitengo cha Mazingira cha Wizara ya Nshati na Madini.
day 2 - pic 3Afisa Misitu Mkuu kutoka Kitengo cha Mazingira – Wizara ya Nishati na Madini (Kulia), Theodory Silinge akitoa ufafanuzi kuhusu umuhimu wa kuhimiza jamii kutumia nishati mbadala wakati wa semina ya mafunzo kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa, inayofanyika jijini Mwanza, Septemba 1 – 4, 2014day 2 - pic 4Afisa Sheria kutoka Wizara ya Nishati na Madini Renatus Damian, akiwasilisha mada kuhusu masuala ya sheria katika utunzaji mazingira wakati wa semina kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa, inayofanyika jijini Mwanza Septemba 1 – 4, 2014.
day 2 - pic 5Afisa Mazingira kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Nassor Abdullatif (Kushoto), akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa kufanya Tathmini ya Mazingira (Environmental Impact Assessment – EIA) kabla ya kuanza utekelezaji wa mradi wowote katika siku ya pili ya semina kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa, inayofanyika jijini Mwanza Septemba 1 – 4, 2014.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »