SHIME:MGAMBO IPO TAYARI KWA LIGI KUU TANZANIA BARA

September 02, 2014
KOCHA Mkuu wa timu ya Mgambo Shooting ya Tanga, Bakari Shime amesema kikosi cha timu hiyo kipo imara na kimekamilika vilivyo kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa Ligi kuu soka Tanzania bara inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 20 mwaka huu hapa nchini.
Shime alitoa kauli hiyo wakati akiongea na TANGA RAHA BLOG mara baada ya kumalizika mchezo wao maalumu wa kujaribu matumizi ya mfumo wa kieletronici kati yao na African Sports ambapo timu hizo ziitoka suluhu pacha ya kutokufungana, uliofanyika kwenye uwanja wa Mkwakwani mkoani hapa.
Alisema kuwa wao wataendelea na maandalizi ya kawaida kujiandaa na mechi yao ya Kagera Sugar ikiwa ni kufungua pazia la michuano hiyo mikubwa hapa nchini na kuhaidia kufanya vizuri kwa sababu ya kikosi hicho kuimarika kila siku.
Katika hatua nyengine, Kocha Shime alisema uongozi wa timu hiyo umeingia mkataba wa miezi sita na aliyekuwa mlinda Coastal Union, Said Lubawa kuichezea kwenye msimu mpya wa Ligi kuu soka Tanzania bara.
Akizungumzia sababu za wao kutokucheza mechi za majaribio,alisema kuwa mechi za aina hiyo wakati mwengine zinaweza zikawa hazina faida kwa timu kutokana na kuwa timu inaweza kucheza mechi hiyo lakini ikifika kwenye ligi kuu ikafanya vibaya.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »