RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN ZIARANI COMORO

September 16, 2014


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mawaziri mbali mbali wakati alipowasili katika   Ikulu ya Comoro kwa mazungumzo na Rais wa Nchi hiyo Dr. Ikililou Dhoinine jana akiwa katika ziara ya kiserikali.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwa katika mazungumzo na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Comoro Dr.Ikililou Dhoinine Ikulu Mjini Comoro jana,Dk.Shein yupo Comoro kwa ziara ya kiserikali akiwa na ujumbe aliofuatana nao.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Comoro Dr.Ikililou Dhoinine (katikati) wakiwa katika mazungumzo ya pamoja na ujumbe wa Rais na Viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Comoro   Ikulu Mjini Comoro jana katika  ziara ya kiserikali akiwa na ujumbe aliofuatana nao. 
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  akifuatana na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Comoro Dr.Ikililou Dhoinine baada ya  mazungumzo Ikulu Mjini Comoro jana,akiwa katika  ziara ya kiserikali  na ujumbe aliofuatana nao.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiteta na  mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Comoro Dr.Ikililou Dhoinine Ikulu Mjini Comoro jana, wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa ujumbe Serikali ya Mapinduzi ukiwa katika ziara Nchini Comoro. Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »