ZAHANATI YA MAJENGO YAPATA CHUMBA CHA UPASUAJI MDOGO NA KUZINDULIWA NA MWENGE HVI KARIBUNI.

August 24, 2014

Kaimu Mkuu wa wilaya ya Kilindi ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Handeni Muhingo Rweyamamu(mwenye 'track suit') akikabidhi Mwenge wa uhuru kwa Kaimu Mkuu wa wilaya ya Korogwe Majjid Mwanga.
Mwenge wa uhuru mwaka 2014 umeweka jiwe la msingi katika chumba cha upasuaji mdogo kilichojengwa katika zahanati ya Majengo iliyopo kata ya Manundu mjini Korogwe.

Akisoma taarifa ya mradi kabla ya kuwekewa  jiwe la msingi na Mkimbiza Mwenge kitaifa Rachel Kassanda, Mganga Mkuu wa halmashauri ya mji Korogwe Dkt Jerry Mwakanyamale alisema kuwa mradi huo ulioanza kujengwa mwaka 2013 kwa fedha za bajeti ya CDG na MMAM mpaka sasa umegharimu jumla ya Tsh.21,048,410/-
Aliongeza kuwa mwaka wa fedha 2012/2013 mradi huo ulitengewa jumla ya Tsh.34,147,000 zikiwa ni CDG Tsh.24,100,000/- ambapo Tsh .18,000,000/- zimeshaletwa na Serikali wakati MMAM ilitengwa Tsh 10,047,000 na fedha zote zimeshatolewa.
Dkt Mwakanyamale alifafanua mpaka sasa ujenzi huo ili kukamilika  umebakisha vyumba 2 vya kubadilishia nguo kabla ya kuingia chumba cha upasuaji,vyoo viwili na korido la kusubiria wagonjwa wakiwa 'theatre'
Wakizungumza na Mwandishiwa habari  katika mahojiano maalumu baadhi ya Wananchi waliohudhuria uwekaji wa jiwe la msingi katika zahanati hiyo, walisema kuwa wanaishukuru sana Serikali kwa kuzidi kuwasogezea huduma za afya jirani na makazi yao na kuongeza kuwa wana imani  chumba hicho cha upasuaji mdogo kitakuwa msaada mkubwa kwao katika masuala ya afya.
"Hii 'theatre' itatusaidia sana hasa ukizingatia kuwa Korogwe imekuwa ikikumbwa na ajali nyingi za barabarani kwa kuwa ni njia kuu ya miji mikuu ya Tanzania,hivyo itaipunguzia mzigo Magunga".Alisema Asha Hassan mkazi wa Manundu.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa wilaya ya Korogwe Dkt Rashid Said alisema kuwa chumba hicho cha upasuaji mdogo kitaisaidia sana wilaya yake kwani kitapunguza msongamano katika hospitali ya  Magunga kwa kuwa wagonjwa wengi  wa upasuaji mdogo,kufungwa na kusafishwa vidonda,walioumia katika ajali wataweza kupata huduma  katika 'thearter' hiyo ya zahanati  ya Majengo pindi itakapokamilika tofauti na sasa ambapo Magunga huhudumia wagonjwa wote na hivyo kuwa na mzigo mkubwa sana hasa zinapotokea ajali za barabarani. 
Baadhi ya viongozi wa wilaya ya Korogwe wakisikiliza taarifa ya mradi mbele ya jengo la chumba cha upsuaji mdogo katika zahanati ya Majengo mara baada ya Mwenge wa uhuru kuwasili kattika zahanati hiyo

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Majjid Mwanga akimkaribisha kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Rachel Kassanda wilayani Korogwe (Kilole),akitokea wilaya ya Kilindi.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »