MISS KANDA YA ZIWA KUTOKA NA VITZ

August 17, 2014
Na Elias Kimaro
MREMBO wa Kanda ya Ziwa 2014, ‘Miss Lake Zone 2014’, anataibuka na zawadi ya gari aina ya Vitz lenye thamani ya Sh.10,000,000, katika shindano litakalofanyika Agosti 30 CCM Kirumba.
 
Akizungumza na TANGA RAHA BLOG, muandaaji wa shindano hilo, Flora Lauwo, alisema jumla ya warembo 18 wanatarajiwa kuchuana kuwania zawadi hiyo iliyotolewa na Lenny wa Geita.
 
“Shindano hili limedhaminiwa na kampuni ya bia TBL kupitia kinywaji cha Redd’s na Pepsi…shindano hili litafanyika Kirumba baada ya lile la Miss Talent kufanyika Agosti 23 mkoani Geita,” alisema Lauwo.
 
Aidha, Lauwo alisema washindi watano wa awali watapewa ving’amuzi, na mshindi wa tatu wa Miss talent atapata Bajaj yenye thamani ya Sh.3,000,000.
 
Awali, meneja wa matukio wa TBL kanda ya ziwa, Erick Mwayela, alisema kampuni yake imekuwa mstari wa mble kudhamini vipaji vya warembo kwa miaka mingi.
 
“Lengo la kampuni yetu ni kuendeleza vipaji vya warembo na mavazi nchini,” alisema Mwayela.
 
Warembo watakaowania zawadi hiyo ya kwanza ni Christina William, Moshi Shaban na Doreen Robert wote wa Mwanza, Cecilia Kibanda, Evelyne Charles, Chritine John (Simiyu), Winfrida Nashon, Elinaja Nnko na Martha John wote toka Mara.
 
Wengine ni Mary Emanuel, Nicole Sarakyika na Recho Judica toka Shinyanga, Jackline Kimanbo, Nyangi Warioba na Faudhia Haruna (Kagera), wakati toka Geita ni Recho Clavery, Farida Ramadhani na Rose Msuya.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »