MAKANGE AWASHAURI WANAVYUO KUACHANA NA MIGOMO

May 20, 2014
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana Mkoa wa Tanga (UVCCM),Abdi Makange amewataka wanafunzi katika vyuo mbalimbali hapa nchini kuacha kufikiria masuala ya migomo na maandamano badala yake waone namna ya watakavyo jiajiri wakati watakapokuwa wamemaliza kwenye vyuo hivyo.

Makange alitoa wito huo mwishoni mwa wiki wakati wa mahafali ya Chuo cha  kujiendeleza kielimu cha  Noverty kilichopo  mjini Tanga ambapo alisema masuala hayo hayana faida yoyote kwao zaidi ya kuwaharibia malengo yao waliyojiwekea kwenye maisha yao ya baadae.

Alisema ni vema wakamua njia za busara kuiepuka migomo na maandamano yasiyo na tija kwenye vyuo vyao lengo likiwa kukaa chini na kuzungumza ili kuweza kupata muafaka badala ya kujichukulia hatua za aina hiyo kwani sio suluhu ya kile wanachokuwa wakikitaka zaidia ya kuwapa  hasara jamii zao wanazotoka.

Alisema serikali inatambua mchango mkubwa wa chuo hicho kwa kutoa elimu kwenye jamii ndio maana wamekuwa wakiwaalika kwenye matamasha na vikao mbalimbali ikiwemo baadhi ya misaada wanayoipeleka.

Aidha alisema chuo hicho kimekuwa mkombozi mkubwa wa vijana kwa kuwawezesha kupata ajira kwenye sekta mbalimbali mkoani hapa kitendo ambacho kinachangia kukuza maendeleo yao na jamii zinazowazunguka.

Akilizungumzia suala la Katiba,Makange alisema nchi imeingia kwenye mchakato wa katiba mpya ambapo itakayoandikwa leo itaishi miaka 59 ijayo na walengwa ni vijana hivyo wahakikisha wanakataa mambo ambayo yanaweza kuwagawa watanzania na mshikamano wao.

Mwenyekiti huyo aliwataka pia wahitimu hao kuhakikisha wanakuwa mabalozi wazuri kwenye jamii wanazoishi pamoja ikiwemo kuwaasa wanafunzi wa kike kujiadhari na mafataki ambao wanaweza kuwaharibia maisha yao hali itakayowafanya kushindwa kufikia malengo yao.

  “Hakikisheni mnakuwa mabalozi wazuri kwenye jamii zenu lakini kwa upande wa wasichana napenda kuwaasa mjihadhari na mafataki wanaoweza kuwaharibia malengo yenu ikiwemo wanafunz mnaobaki tilieni mkazo elimu kwani ndio njia pekee itayowaletea maisha bora “Alisema Makange.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »