NMB YAFUNGUA RASMI TAWI LA USA RIVER-ARUSHA
Mkuu
wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Nyerembe D. Munasa Sabi (kati) akikata utepe
kuashiria uzinduzi rasmi wa tawi la NMB Usa River.Wakishuhudia kutoka
kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Biashara kwa Wateja Wakubwa wa Benki
ya NMB, Richard Makungwa pamoja na Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini,
Vicky Bishubo . Hafla ya uzinduzi wa tawi hili la NMB Usa River
umefanyika mwanzoni mwa wiki katika viwanja vya tawi hili mkoani Arusha.
Mkuu
wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Nyerembe D. Munasa Sabi akipata maelezo
kutoka kwa Meneja wa Tawi la NMB Usa River Bernadetha Mmary mara baada
ya kuzindua tawi na kulitembelea ndani.
Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya uzinduzi huu wakifurahia ufunguzi wa tawi jipya la NMB Usa River