PATO LA MKOA WA TANGA LAONGEZEKA TOKA TRILIONI 1.78 HADI TRILIONI 2.009

January 04, 2014
Na Oscar Assenga
Pato la Mkoa wa Tanga limeongezeka kutoka trilioni 1.78 hadi kufikia trilioni 2.099 kwa mwaka 2012 ambapo ongezeko hilo ni sawa na asilimia 17.8.
Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Luteni Mstaafu Chiku Gallawa wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Mkoani hapa desemba 30 mwaka huu kuhusiana na mafanikio ya Mkoa wa Tanga ya mwaka 2012 hadi 2013.
Gallawa amesema katika ongezeko hilo Mkoa umechangia wastani wa asilimia 4.69 ya pato la Taifa ambalo ni Trilioni 44.7  kwa mwaka 2012 kulinganisha na 37.5 Trilioni kwa mwaka 2011.
Mkuu huyo wa Mkoa alisema pia pato la mtu mmoja mmoja limeongezeka kutoka wastani wa shilingi laki 8,86,343 mwaka 2011 hadi shilingi 1,26,432 kwa mwaka 2012 ambapo wastani wa kitaifa ni shilingi 1,025,038 kiasi ambacho Mkoa wa Tanga unashika nafasi ya nane kati ya mikoa 25 ya Tanzania bara tangu mwaka 2010.
Aidha katika utekelezaji wa malengo ya kukuza uchumi Mkoa wa Tanga umeandaa mkakati wa kutekeleza miradi kwa kutumia mfumo wa tekeleza sasa kwa matokeo makubwa kwa miaka 2013 hadi 2015.
Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa   ameainisha vipaumbele katika maeneo ya kukuza mapato kwa mtu mmoja mmoja kufikia wastani 1.5, kuendeleza huduma za jamii za  elimu kwa kuongeza ufaulu kutoka asilimia 32 hadi 60 msingi na sekondari na maji kufikia asilimia 50 ifikapo 2015 kwa kutoa huduma za maji kwa umbali usiozidi mita 400 kutoka eneo la makazi.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »