ZDFA:HATUNA MPANGO NA HALL

November 11, 2013
Na Masanja Mabula -Pemba .11/11/2013.

Siku chache baada ya aliyekuwa kocha mkuu wa timu ya Azma Stewart John Hall kufungasha virago kutoka  klabu hiyo , Chama cha Soka cha Zanzibar ZFA kimesema hakina mpango wa kumuita kocha huyo kwa ajili ya kuifundisha timu ya taifa ya Zanzibar .

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi  , katibu Mkuu wa ZFA Kassim Haji amesema kuwa mpango wa kumrejesha kocha huyo kukionoa kikosi cha Heroes hakupo na badala yake wataendelea kumwamini Salum Bausi .

Kassim amezidi kufahamisha kwamba pamoja na  ZFA kuwa ndiyo iliyomleta Stowart kwa mara ya kwanza hapa nchini , lakini fursa ya kuifundisha timu ya Taifa ya Zanzibar kwa sasa itakuwa ni ndoto .

"Tunaelewa uwezo wa Stowart , kwani ndiyo sisi tuliomfungulia milango hapa nchini , lakini mipango ya kumrejesha kwa sasa haipo kwani tunawapa nafasi makocha wazawa " alifahamisha Kassim .

Aidha akizungumzia maandalizi ya timu hiyo ambayo inajiandaa na michuano ya Tusker Challenge Cup , Kassim amesema kuwa yanaendelea vyema na kupongeza uwamuzi wa kocha wa  kuwapima afya wachezaji .

Hata hivyo alikiri kuwa  ZFA inakabiliwa na ukata wa fedha wa kuweza kuindalia michezo ya kimataifa ya kujipima nguvu kabla ya kuelekea Mjini Nairobu Kenya kushiriki michuano hiyo .

"Kunahitajika zaidi ya shilingi milioni 15 , kuandaa  mechi ya kimataifa , kwani tunatakiwa kuigharamia timu ili iweze kufika Zanzibar au timu yetu kuweza kusafiri , lakini tuna mpango wa kucheza mechi za kirafiki na vilabu vya Tanzania Bara ikiwemo Kilimanjaro Stars " alieleza .

Awali uteuzi wa timu ya Taifa ya Zanzibar ulipingwa na wajumbe wa kamati Tendaji wa ZFA Pemba ambayo nayo ilitangaza kikosi cha wachezaji 30 kuunda  timu ya kombaini  ya Pemba kwa lengo la kukutana na iliyochaguliwa na Bausi ili kupata kikosi cha Heroes

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »