POULSEN AMTEMA IVO MAPUNDA TAIFA STARS

November 11, 2013


Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen amemtema kipa Ivo Mapunda katika kikosi chake.

Baada ya zaidi ya miaka mitatu, Ivo anayekipiga Gor Mahia ya Kenya aliitwa katika kikosi hicho.

Lakini baadaye Poulsen amemuondoa katika kikosi hicho kwa madai kulikuwa na ukimya.
 
"Sikusikia lolote kuhusiana na Mapunda, sifanya mkutano wa waandishi lakini ni uamuzi umepita kwa ajili huenda atakuwa na majukumu mengine," alisema.

Hata hivyo kuna taarifa zinaeleza TFF hawakupeleka barua ya kumtambulisha Ivo kuitwa katika kikosi hicho.

Ivo ni kati ya makipa wlaiong'ara katika Ligi Kuu Kenya na amesaidia Gor Mahia kutwaa ubingwa wa Kenya ambao mara ya mwisho waliubeba miaka 13 iliyopita.
 
chanzo:salehjembe.blogspot.com

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »