ADC YAPATA PIGO TANGA.

November 24, 2013
Na Oscar Assenga,Tanga.
CHAMA  cha  siasa  cha ADC   kilichokuwa kikijiimarisha Mkoani hapa, kimepata pigo baada ya kuondokewa na viongozi wake  watatu  wa  ngazi ya Mkoa na Wilaya waliyohamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA).
 
Viongozi hao  wa ADC  waliyokihama chama hicho na kujiunga na Chadema  na nyazifa zao ni Kamishina wa Mkoa wa Tanga, Jadi Bamba, Mwenyekiti wa wanawake Wilaya ya Handeni, Mwanamvua  Mganga na Katibu wa Chama  wa  Wilaya ya  hiyo, Hamida Msumeno.
 
Wakizungumza mara baada ya kupokea  kadi mpya za uanachama wa Chadema, viongozi hao walieleza sababu za kukihama chama chao cha ADC  kuwa zinatokana na kuridhishwa na siasa za Chadema  ambazo hazipo Chama kingine.

Walisema kuwa  hawakuhama kwa kurubuniwa bali  ni baada  ya  kubaini kuwa ADC  hakuna kazi za siasa ambazo walizitegemea kuwepo kwa ajili ya kukomboa wananchi wa Tanzania na kwamba Chama makini ni Chadema.
 
Akiwatangaza  katika sherehe za kuwapokea wanachama hao wapya, Katibu wa Chadema Mkoa wa Tanga, Jonathan Bahweje alisema kuwa  viongozi hao ni mashujaa na kwamba anatarajia watakuwa chachu ya vuguvugu la kisiasa ndani ya Mkoa wa Tanga.
 
Bahweje  alisema kuwa si viongozi hao pekee lakini anampango wa kupokea wengine kutoka vyamba mbalimbali vya siasa ikiwemo CCM  ambacho alidai kuwa kimekuwa mufirisi kwa kuwa na viongozi wasiyo na maono juu ya wananchi na taifa kwa ujumla.
 
Aidha aliwaomba wananchi na wanaCCM kwa ujumla kukiunga mkono Chadema kwa madai kuwa ndicho chenye malengo na mikakati ya  kulikomboa taifa hili kutokana na kuendesha siasa za kistaarabu na zenye kuleta matumaini.
 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »