Korogwe
JUMUIYA ya Vijana wa chama cha mapinduzi UVCCM mjini Korogwe imetakiwa kuonyesha uhai wao kwa kuimarisha umoja wao na kuunda vikundi vya uzalishaji mali ambavyo vitawawezesha katika kujikwamua kiuchumi badala ya kujitumbukiza kwenye migogoro yenye kuzorotesha maendeleo yao.
Mwenyekiti wa UVCCM Korogwe mjini, Thomas Ngonyani Majimarefu ametoa kauli hiyo wakati alipozungumza na wanachama na viongozi wa jumuiya hiyo tawi la Old Korogwe wakati alipofanya ziara yake kwenye eneo hilo kama sehemu ya kutoa shukrani zake mara baada ya kuchaguliwa kushikilia kiti hicho cha wilaya.
Ngonyani amesema kwamba ili jumuiya hiyo iwe imara kuna kila haja kwa viongozi khakikisha wanakuwa na wanachama walio hai huku wakithubtu kjianzishia miradi ambayo itawasaidia kjikwamua kiuchumi utaratibu ambao utasababisha vijana wengi kuvtiwa kujiunga na umoja wao na kuharakisha maendeleo.
Naye Katibu wa jumuiya hiyo ya vijana eneo la Korogwe mjini Anna Jorojick aliwakumbusha vijana hao umuhimu wa kutunza siri za vikao vyao ili kutotoa fursa kwa wengine kufanya propaganda ambapo zitasababisha hujuma ndani ya maazimio yao waliojiwekea njia aliyoeleza pia kuimarisha umoja wao.
JUMUIYA ya Vijana wa chama cha mapinduzi UVCCM mjini Korogwe imetakiwa kuonyesha uhai wao kwa kuimarisha umoja wao na kuunda vikundi vya uzalishaji mali ambavyo vitawawezesha katika kujikwamua kiuchumi badala ya kujitumbukiza kwenye migogoro yenye kuzorotesha maendeleo yao.
Mwenyekiti wa UVCCM Korogwe mjini, Thomas Ngonyani Majimarefu ametoa kauli hiyo wakati alipozungumza na wanachama na viongozi wa jumuiya hiyo tawi la Old Korogwe wakati alipofanya ziara yake kwenye eneo hilo kama sehemu ya kutoa shukrani zake mara baada ya kuchaguliwa kushikilia kiti hicho cha wilaya.
Ngonyani amesema kwamba ili jumuiya hiyo iwe imara kuna kila haja kwa viongozi khakikisha wanakuwa na wanachama walio hai huku wakithubtu kjianzishia miradi ambayo itawasaidia kjikwamua kiuchumi utaratibu ambao utasababisha vijana wengi kuvtiwa kujiunga na umoja wao na kuharakisha maendeleo.
Naye Katibu wa jumuiya hiyo ya vijana eneo la Korogwe mjini Anna Jorojick aliwakumbusha vijana hao umuhimu wa kutunza siri za vikao vyao ili kutotoa fursa kwa wengine kufanya propaganda ambapo zitasababisha hujuma ndani ya maazimio yao waliojiwekea njia aliyoeleza pia kuimarisha umoja wao.

EmoticonEmoticon