PRISON YAIPIGISHA KWATA MGAMBO SHOOTING.

October 06, 2013
NA OSCAR ASSENGA,TANGA.
TIMU ya Maafande wa Jeshi la Magereza nchini Tanzania Prison leo wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Maafande wenzao wa Jeshi la Kujenga Taifa Mgambo Shooting katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania bara iliyochezwa uwanja wa Mkwakwani.

Katika mchezo huo ambao ulianza kwa kasi na upinzani mkubwa kutokana na kukamiana kwa timu hizo ambapo mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika hakuna timu iliyokuwa imeona lango la mwenzake ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi ya mashambulizi kwa timu zote iliyotokana na mabadiliko ya baadhi ya wachezaji wao.

Mabadiliko yalianzia kwa timu ya Mgambo Shooting ambapo walimtoa Martin Mlolela ambapo nafasi yake ilichukuliwa na Mohamed Namkopwe huku Prison wakimtoa Julius Kwanga na kumuingiza Hamis Mahingo

Wakionekana kujipanga na kucheza kwa umakini mkubwa licha ya uwanja wa mkwakwani kuteleza kutokana na mvua ilionyesha nyakati za mchana kabla ya kuanza mchezo huo.

Tanzania Prison waliweza kufanya mashambulzi ya kushtukiza lango mwa Mgambo Shooting na kuwachukua dakika 17 ya kupindi cha pili kuweza kupata bao lao kupitia Julius Kwanga kwenye dakika ya 62 baada ya kutokea piga nikupige lango mwa Mgambo Shooting.

Baada ya kuingia bao hilo,Mgambo Shooting walijaribu kupambana ili kuweza kurudisha bao hilo bila mafanikio yoyote yale ambapo mpaka dakika 90 mwamuzi wa mchezo huo anapuliza kipenga ubao ukasomeka 1-0.

Kwa matokeo hayo Tanzania Prison watakuwa wamejikusanyia pointi 7 katika msimamo wa Ligi kuu Tanzania bara huku wakijiandaa na mechi yao inayofuata na Simba kwenye uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »