WAENDELEZAJI MIRADI YA NISHATI JADIDIFU WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA UWEZESHWAJI KUTOKA REA

June 19, 2025 Add Comment
-Ni kwa miradi inayozalisha chini ya Megawati 10

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu ametoa wito kwa waendelezaji wa miradi ya nishati jadidifu kote nchini kuchangamkia fursa za uwezeshwaji zinazotolewa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kuwa na miradi yenye tija kwa Taifa.

WMA YAENDESHA ZOEZI LA UHAKIKI MITA ZA UMEME VIWANDANI

June 19, 2025 Add Comment

 



Wakala wa Vipimo (WMA) unaendesha zoezi la kuhakiki mita za umeme zilizofungwa katika viwanda mbalimbali nchini ili kuhakikisha Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) inapata mapato stahiki na wenye viwanda wanalipa gharama stahiki kulingana na huduma ya umeme wanaotumia.

Hayo yalibainishwa Juni 18, 2025 na Meneja wa WMA Makao Makuu, Albogast Kajungu wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika uwanja wa Chinangali, Dodoma.

Kajungu alisema kuwa hadi sasa WMA imekagua mita za umeme zaidi ya 2,000 huku lengo likiwa ni kuhakiki mita zote zilizo kwenye matumizi katika viwanda vyote nchini katika zoezi lililoanza Mei mwaka huu



“Hali inaonesha kwamba mita nyingi zilizo kwenye matumizi viwandani ziko vizuri. Chache ambazo tumekuta zina mapungufu, tumewasiliana na Mamlaka husika kwa ajili ya kuzirekebisha na nyingine kuzibadilisha ili kuhakikisha vipimo viko sahihi kwenye eneo hilo,” alisema Kajungu.
Akieleza zaidi, alisema kuwa zoezi hilo la uhakiki linahusisha mita zote za umeme zilizo katika matumizi lakini Wakala imeona ianze na zile zilizoko viwandani kwakuwa zinatumia umeme mkubwa hivyo ikiwa haziko sawasawa, kuna uwezekano wa TANESCO au wenye viwanda kupata hasara.

Aidha, alieleza kuwa zoezi la uhakiki linahusisha pia bidhaa za chuma hususan zinazotumika katika ujenzi kwani kumekuwa na malalamiko katika eneo hilo.

Akifafanua, Kajungu alisema kuwa sekta ya ujenzi hapa nchini inakua kwa kasi ambapo miradi mingi ya ujenzi inayotekelezwa na serikali inatumia bidhaa za chuma hivyo WMA imeona iongeze nguvu kuhakiki bidhaa hizo hususani zinazozalishwa kwenye viwanda vya ndani ili kuhakikisha zina vipimo vilivyo sahihi.




Alisema kuwa wazalishaji wanajitahidi kuzalisha kwa kuzingatia viwango lakini lengo la Wakala hiyo ni kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi zinaendelea kuwa na vipimo sahihi ili kuwalinda wananchi dhidi ya madhara ambayo yanaweza kutokea kwa kutumia bidhaa za chuma ambazo hazikidhi vipimo vinavyokubalika kisheria.

Sambamba na uhakiki wa mita za umeme na bidhaa za chuma, Kajungu alieleza kuwa zoezi hilo la uhakiki pia linahusisha dira za maji zilizo kwenye matumizi kwakuwa ndizo zenye malalamiko yanayohusiana na bili na mengineyo.

Hata hivyo, alibainisha kuwa pamoja na kuhakiki bidhaa zilizo kwenye matumizi, WMA kupitia Kituo cha Vipimo Misugusugu kilichopo mkoani Pwani, pamoja na kazi nyingine, huhakiki mita mpya za umeme na dira mpya za maji ili zinapokwenda kufungwa kwa wateja ziwe zimeshathibitishwa kuwa vipimo vyake ni sahihi.

Kajungu alitumia fursa hiyo kuwaalika wananchi wafike kwa wingi kwenye Banda la Wakala wa Vipimo ili kujipatia elimu kuhusiana na vipimo mbalimbali vinavyotumika ili kuwalinda kwa maana ya kupata thamani ya fedha wanazotoa wanapokwenda kununua bidhaa.

Wakala wa Vipimo ni mojawapo ya Wakala za Serikali yenye dhima ya kutoa huduma za kumlinda mlaji kupitia uhakiki wa vipimo, usimamizi wa vipimo na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Majukumu yake ni kumlinda mlaji na umma kwa ujumla kupitia uhakiki na uthibiti wa vipimo vinavyotumika katika biashara na huduma nyingine ili kuhakikisha kuwa vipimo hivyo ni sahihi na vinatumika kwa usahihi kulingana na Sheria ya Vipimo Sura 340, mapitio ya mwaka 2002 na maboresho yake ya mwaka 2026 pamoja na kanuni zake.




AFRIKA IPEWE UHURU WA KUZALISHA NISHATI KWA KUTUMIA RASILIMALI ZAKE -DKT .BITEKO

June 19, 2025 Add Comment
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko(wa pili kushoto) akishiriki kwenye mdahalo wa Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg 2025 (SPIEF'25) lililofanyika leo 19 Juni, 2025 katika kituo cha Mikutano na Maonesho ExpoForum katika jiji la St. Petersburg nchini Urusi. 


📌 Ahimiza Tanzania na Urusi kuendeleza uhusiano wake wa kuheshimiana


📌 Tanzania kutumia makaa ya mawe kuzalisha umeme wastani wa  megawati 120


📌  Tanzania yapongezwa kwa mafanikio yake sekta ya nishati


📌  Ahimiza mfumo sawa wa uzalishaji nishati kati ya nchi tajiri na masikini 


📌  Kampuni za Urusi zaombwa kuwekeza zaidi Afrika 


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa nchi za Afrika kupewa uhuru wa kuzalisha nishati kwa kutumia raslimali zilizopo barani humo.


Dkt. Biteko ametoa wito huo Juni 19, 2025 wakati akizungumza katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg linalofanyika nchini Urusi.


Amesema Afrika inahitaji programu itakayosaidia kufikia dhamira yake ya kuondoa idadi kubwa ya watu ambao hawatumii nishati safi huku akitaja baadhi ya athari za matumizi ya nishati isiyo safi ikiwemo uharibifu wa mazingira.


Ameongeza kuwa Afrika ina vyanzo  vingi vya kuzalisha nishati, mfano Tanzania kuna vyanzo kama vile jua, maji na gesi asilia. Hata hivyo barani humo hakuna uhuru wa kutumia makaa ya mawe licha ya kuwepo kwa kiwango kikubwa pamoja na kuwa nchi kubwa duniani zinaweza kufanya hivyo.

Wa kwanza kulia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Baraza la Nishati Afrika, NJ Ayuk. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Alexander Pankin. Waziri wa Nishati Urusi Mhe. Sergey Tsivilyov na kushoto ni msimamizi wa mdahalo Alexey Bobrovsky na kushoto ni msimamizi wa mdahalo Alexey Bobrovsky. (Picha na ONWM & WN)

“ Hivyo iangaliwe namna kwa kila nchi kutumia raslimali zake ili kuzalisha nishati, mfumo uliopo unazifanya nchi zote kuwa sawa lakini ukweli ni kwamba hatuko sawa. Kwa mfano Afrika inachangia asilimia 3 hadi 4 pekee ya uchafuzi wa mazingira, lakini imepewa mzigo mkubwa zaidi.” Amesema Dkt. Biteko.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza kwenye mdahalo wa Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg 2025 (SPIEF'25) lililofanyika leo 19 Juni, 2025 katika kituo cha Mikutano na Maonesho ExpoForum uliopo katika jiji la St. Petersburg nchini Urusi. (Picha na ONWM & WN)


Amesisitiza” Kila nchi itumie utaratibu wake wa kuzalisha nishati lakini kwa lengo la kupunguza uchafuzi wa mazingira.”


Amezungumzia uhusiano  mzuri uliopo wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi na kusema kuwa uendelee kuwa wa kuheshimiana na kukubaliana.

Ambapo ametaja manufaa yake kuwa ni  pamoja na kubadilishana ujuzi na kuisaidia Tanzania katika mitaji ya  miradi nishati.


Amebainisha kuwa Tanzania ina mpango wa kutumia makaa ya mawe kwa ajili ya kuzalisha takribani megawati 120 za umeme.


Kwa upande wake, Waziri wa Nishati wa Urusi, Mhe. Sergey Tsivilev amesema kuwa Rais wa nchi hiyo Mhe. Vladimir Putin amekuwa na jitihada mbalimbali za kuhakikisha zinaungana na nchi zingine katika kupatia ufumbuzi  changamoto za masuala ya nishati.

Naye, Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya African Energy Chamber, Bw. NJ Ayuk amesema kuwa ni muhimu kwa nchi za Afrika na Urusi kuungana na kuhakikisha sauti ya Afrika inasikika na kutekeleza wanayokubaliana ili wote waweze kunufaika na uhusiano kati yao.


Aidha, ameiomba Serikali ya Urusi kuwezesha kampuni kutoka nchini humo ili ziweze kuwekeza zaidi Afrika hususan katika sekta ya nishati.


Pia, ameipongeza Tanzania katika hatua iliyopiga na mafanikio yake katika sekta ya nishati  sambamba na kutoa wito kwa nchi za Afrika kujifunza zaidi kutokana na mafanikio yaliyopo nchini Urusi.


Jukwaa hilo la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg linatarajiwa kuwa na washiriki kutoka takribani nchi 140.


Mwisho.

AFRIKA IPEWE UHURU WA KUZALISHA NISHATI KWA KUTUMIA RASILIMALI ZAKE -DKT.BITEKO

June 19, 2025 Add Comment


📌*Ahimiza Tanzania na Urusi kuendeleza uhusiano wake wa kuheshimiana*


📌*Tanzania kutumia makaa ya mawe kuzalisha umeme wastani wa  megawati 120*


📌 *Tanzania yapongezwa kwa mafanikio yake sekta ya nishati*


📌 *Ahimiza mfumo sawa wa uzalishaji nishati kati ya nchi tajiri na masikini*


📌 *Kampuni za Urusi zaombwa kuwekeza zaidi Afrika* 


*Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa nchi za Afrika kupewa uhuru wa kuzalisha nishati kwa kutumia raslimali zilizopo barani humo.


Dkt. Biteko ametoa wito huo leo Juni 19, 2025 wakati akizungumza katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg linalofanyika nchini Urusi.

Amesema Afrika inahitaji programu itakayosaidia kufikia dhamira yake ya kuondoa idadi kubwa ya watu ambao hawatumii nishati safi huku akitaja baadhi ya athari za matumizi ya nishati isiyo safi ikiwemo uharibifu wa mazingira.


Ameongeza kuwa Afrika ina vyanzo  vingi vya kuzalisha nishati, mfano Tanzania kuna vyanzo kama vile jua, maji na gesi asilia. Hata hivyo barani humo hakuna uhuru wa kutumia makaa ya mawe licha ya kuwepo kwa kiwango kikubwa pamoja na kuwa nchi kubwa duniani zinaweza kufanya hivyo.

“ Hivyo iangaliwe namna kwa kila nchi kutumia raslimali zake ili kuzalisha nishati, mfumo uliopo unazifanya nchi zote kuwa sawa lakini ukweli ni kwamba hatuko sawa. Kwa mfano Afrika inachangia asilimia 3 hadi 4 pekee ya uchafuzi wa mazingira, lakini imepewa mzigo mkubwa zaidi.” Amesema Dkt. Biteko.


Amesisitiza” Kila nchi itumie utaratibu wake wa kuzalisha nishati lakini kwa lengo la kupunguza uchafuzi wa mazingira.”

Amezungumzia uhusiano  mzuri uliopo wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi na kusema kuwa uendelee kuwa wa kuheshimiana na kukubaliana.


Ambapo ametaja manufaa yake kuwa ni  pamoja na kubadilishana ujuzi na kuisaidia Tanzania katika mitaji ya  miradi nishati.

Amebainisha kuwa Tanzania ina mpango wa kutumia makaa ya mawe kwa ajili ya kuzalisha takribani megawati 120 za umeme.


Kwa upande wake, Waziri wa Nishati wa Urusi, Mhe. Sergey Tsivilev amesema kuwa Rais wa nchi hiyo Mhe. Vladimir Putin amekuwa na jitihada mbalimbali za kuhakikisha zinaungana na nchi zingine katika kupatia ufumbuzi  changamoto za masuala ya nishati.

Naye, Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya African Energy Chamber, Bw. NJ Ayuk amesema kuwa ni muhimu kwa nchi za Afrika na Urusi kuungana na kuhakikisha sauti ya Afrika inasikika na kutekeleza wanayokubaliana ili wote waweze kunufaika na uhusiano kati yao.


Aidha, ameiomba Serikali ya Urusi kuwezesha kampuni kutoka nchini humo ili ziweze kuwekeza zaidi Afrika hususan katika sekta ya nishati.



Pia, ameipongeza Tanzania katika hatua iliyopiga na mafanikio yake katika sekta ya nishati  sambamba na kutoa wito kwa nchi za Afrika kujifunza zaidi kutokana na mafanikio yaliyopo nchini Urusi.


Jukwaa hilo la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg linatarajiwa kuwa na washiriki kutoka takribani nchi 140.


Mwisho.

TANZANIA NA BENKI YA DUNIA WAJADILIANA UTEKELEZAJI MPANGO MAHSUSI WA NISHATI WA MISHENI 300

June 19, 2025 Add Comment


📌 *Mhandisi Mramba aeleza hatua zinazochukuliwa na Serikali kutekeleza Misheni 300*


📌 *Benki ya Dunia yapongeza*


📌 *Yaahidi kuendelea kuiunga mkono Tanzania*



Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felichesmi Mramba amekutana na Viongozi Waandamizi kutoka Benki ya Dunia ( WB) kwa lengo la kujadili hatua mbalimbali zilizofikiwa katika utekelezaji wa Mpango Mahsusi wa kuwafikishia  umeme Waafrika milioni 300 ifikapo 2030 ujulikanao kama Misheni 300.


Kikao hicho kimefanyika  katika Jiji la Cape Town nchini Afrika Kusini kando ya Mkutano wa Jukwaa la Nishati Afrika ambapo Tanzania inashiriki.


 Mhandisi Mramba ameeleza kuwa, katika Mpango huo uliosainiwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika uliofanyika mwezi Januari 2025, Tanzania kwa upande wake imeuweka Mpango huo kwenye mipango yake ya Serikali ili kutimiza malengo yaliyowekwa.


Amesema  kukamilika kwa Mpango huo kutaiwezesha Tanzania kuongeza upatikanaji umeme kutoka asilimia 78.4 ya sasa hadi asilmia 100 ifikapo mwaka 2030 na kuongeza matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia hadi kufikia asilimia 75 ifikapo 2030.


Kwa upande wao, Watendaji wa Benki ya Dunia, Bi.Yadviga Semikolenova, Meneja Mtendaji Ukanda wa  Kusini Mashariki mwa Afrika pamoja na Dkt. Rhonda  Antoine, Mtaalam Mwandamizi wa Nishati Ukanda wa Afrika wameipongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua inazochukua ili kuhakikisha Mpango wa Misheni 300 unafanikiwa na hivyo kuwezesha wananchi kupata nishati ya uhakika. 

Aidha, Benki ya Dunia imeonyesha utayari wa kuendelea kuunga mkono juhudi  zinazofanywa na Tanzania  kuhakikisha inaendelea kuutekeleza mpango wa Misheni 300.


Katika kikao hicho, Mhandisi Mramba aliambatana na Mhandisi Innocent Luoga, Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu pamoja na wataalam kutoka Wizara ya Nishati, TANESCO, REA, TPDC na EWURA