MEATU MTAENDEA KUPATA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO IKIWEMO NISHATI -DKT.SAMIA

June 18, 2025 Add Comment


*📌Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini*


📌 *Ataka umeme utumike kuongeza thamani ya mazao, kilimo na ufugaji*.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani amesema Serikali imeendelea kupeleka maendeleo katika Wilaya ya Meatu ikiwemo ukamilishaji wa usambazaji  umeme katika Vijiji vyote 109 vya Wilaya hiyo.


Dkt. Samia ameyasema hayo Juni 17, 2025 Wilayani Meatu Mkoa wa Simiyu akiwa kwenye ziara ya kikazi.

"Kama tulivyoahidi, hatujaishia hapo, kazi ya usambazaji umeme sasa inaendelea kwenye vitongoji lakini pamoja na jitihada hizi zote ninafahamu kuna changamoto ya umeme kutokuwa na nguvu ambayo inatatuliwa." Amesema Dkt. Samia

Ameeleza kuwa, Wizara ya Nishati inatatua   changamoto hiyo  ya umeme kutokuwa na nguvu  kwa kujenga  njia ya kusafirisha umeme kutoka Shinyanga hadi Simiyu na ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme. 

Amesema kukamilika kwa miradi hiyo kutapelekea uwepo wa umeme wenye nguvu na wa kutosha kwa ajili ya shughuli mbalimbali za uzalishaji ikiwemo Viwanda.

Amesisitiza kuwa, lengo la Serikali ni kuona wananchi wanatumia nishati ya umeme kwa shughuli mbalimbali ikiwemo kuongeza thamani ya mazao, kilimo na ufugaji.



Wazalishaji wa Chanjo za Mifugo Kuungana Afrika Waandaa Mwongozo wa Kudhibiti Chanjo

June 17, 2025 Add Comment
Na Daudi Nyingo, Dar es Salaam

Wasajili wa Chanjo na Wakurugenzi wanaosimamia uzalishaji wa chanjo za mifugo kutoka nchi 25 za ukanda wa Afrika wamekutana nchini Tanzania kujadili namna ya kuwa na mfumo wa pamoja wa kutokomeza ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo. Mkutano huu umeanza tarehe 16 hadi 20 Juni 2025 katika Ukumbi wa King Jada Hotel uliopo jijini Dar es Salaam.

MRAMBA AWASILI NCHINI AFRIKA KUSINI KUSHIRIKI JUKWAA LA NISHATI AFRIKA 2025

June 17, 2025 Add Comment

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felichesm Mramba amewasili nchini Afrika ya Kusini kushiriki Jukwaa la Nishati Afrika 2025 ambalo ambalo litaangalia masuala mbalimbali ya Nishati ikiwemo Nishati Safi ya Kupikia.

Jukwaa hilo linaanza leo Juni 17,2025 na linatarajiwa kumalizika Juni 20,2025.

Nchini Afrika Kusini, Mhandisi Mramba ameambata na Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu Mhandisi Innocent Luoga na Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia kutoka Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia Wizara ya Nishati Bw. Nolasco Mlay sambamba na wataalam kutoka Wakala wa Nishati Vijijini ( REA), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA).


MWENYEKITI REB AIHAKIKISHIA USHIRIKIANO KAMPUNI YA KUZALISHA NA KUSAMBAZA UMEME YA MATEMBWE VILLAGE COMPANY YA MKOANI NJOMBE

June 17, 2025 Add Comment
-Inazalisha umeme wa kilowati 550 kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Kiyepa

MHE. RAIS AZINDUA HOSPITALI YA ZAIDI YA BILIONI 4, WANANCHI WAMPA TANO

June 17, 2025 Add Comment

Na John Mapepele - OR TAMISEMI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt, Samia Suluhu Hassan leo amezindua Hospitali ya Wilaya ya Itilima iliyogharimu shilingi bilioni 4.7 iliyojumuisha ujenzi wa miundombinu na ununuzi wa vifaatiba huku wananchi wakimpongeza.