SERIKALI YAITAKA COMMUNITY NETWORK KUSAMBAZA TEHAMA VIJIJINI

May 27, 2025 Add Comment
Serikali kupitia Tume ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) imeitaka Taasisi ya School of Community Network kuongeza juhudi za kuanzisha vituo vya mafunzo ya TEHAMA katika mikoa mbalimbali nchini, hususan vijijini, ili kuwajengea vijana ujuzi wa kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidigitali.

LESOTHO WAVUTIWA NA REA

May 27, 2025 Add Comment
-Wampongeza Rais Samia katika suala la uhamasishaji wa nishati safi ya kupikia

MBOGGO ACHUKUA FOMU YA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA TANGA KUPITIA ACT- WAZALENDO HUKU AKIHAIDI KUIREJESHA TANGA YA VIWANDA

May 27, 2025 Add Comment
Katibu wa Chama cha ACT -Wazalendo  Wa Jimbo la Tanga Mohamed Salim Ponda (kushoto)  akimkabidhi fomu ya kuomba kuteuliwa kuwa mgombea Ubunge Jimbo la Tanga mwanachama wao John Charles Mboggo  (katikati)  kulia ni Mwenyekiti wa Wazee Jimbo la Tanga (ACT Wazalendo) Zaharan Mohamed


Na Oscar Assenga, Tanga.

KADA wa Chama Cha ACT –Wazalendo Mkoani Tanga John Charles Mboggo amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kuwania Ubunge katika Jimbo la Tanga kupitia chama hicho huku akihaidi kuirejesha Tanga ya Viwanda ambayo ni ndoto kubwa ya wananchi wa mkoa huo.

Akizungumza leo na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu hiyo alisema lenbgo la kuchukua fomu ya kuwania Ubunge ni kutaka kuhakikisha anatoa mchango wake katika kurejesha viwanda vya Tanga ambavyo wananchi wamekuwa na kiu navyo.

Alisema kwamba kwa sababu viwanda ni ajira  na nguvu kazi ya Tanga wanaongelea kuna vijana asilimia 68 ya vijana wakitumika kwenye viwanda watakuwa na uchumi kwenye Jimbo hilo na Mkoa kwa Ujumla.

“Tanga tunaamini sisi ni watu tunaamini watu wa kuleta maendeleo na ndio maana tunawahamasisha wananchi wenye sifa za kupiga kura kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye zoezi la kura  kwa lengo la kuwachaguoa viongozi watakaowaongoza”Alisema



Aidha alisema kwamba wasione aibu kutokana na uwepo wa hila mbalimbali wanajua namna ya kubaliana nayo ili kuhakikisha hazijitokezi kwenye mchakato huo.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Jimbo la Tanga  Anasi Mohamed Rweymamu alisema kwamba wanaendelea kuwakaribisha wagombe na kura zao wa maoni ndani ya chama ndizo zitakazoamua nani anaweza kupeperusha tiketi ya chama hicho kwenye nafasi ya Ubunge.

Alisema kwamba ACT Wazalendo ndio chama pekee ambacho kinaweza kupeperusha vyema Bendera yake katika kuibuka na ushindi kwenye nafasi ya Ubunge Jimbo la Tanga na Tanzania kwa upekee.

Naye kwa upande Katibu wa ACT  WaaJimbo la Tanga Mohamed Salim Ponda alisema kwamba wapo kwenye maandalizi ya uchaguzi kama chama hicho Taifa kilipotangaza kwamba zoezi la kuchukua fomu kutoka Aprili 18 mwaka huu mpaka 31 mwezi Mei katika nafasi za Ubunge na Udiwani.

Alisema kwamba katika uchaguzi huo wamejipanga kwamba wagombea watakao wapitisha katika kinyang’anyiro cha Ubunge katika Jimbo hilo watakuwa imara kuhakikisha wanapeperusha vyema bendera hiyo.

Mwisho.

TPAWU YATAKA MCHAKATO KIMA CHA CHINI SEKTA BINAFSI UHARAKISHWE

May 27, 2025 Add Comment

 

 Mwenyekiti TPAWU Taifa Daniel Bariyanka Joachim akizungumza kwenye kikao hicho

Na Godwin Myovela, Morogoro

CHAMA cha Wafanyakazi Mashambani na Kilimo nchini (TPAWU) kupitia kikao cha Baraza Kuu la chama hichoTaifa, kimeomba kuharakishwa kwa mchakato unaoendelea wa kupanga kima cha chini cha mshahara sekta binafsi, kuzingatia maoni ya wadau-sambamba na kuhakikisha kima hicho kutopungua Tsh. 350,000 kwa mwezi, ili kusaidia kumudu gharama za maisha.

Mwenyekiti TPAWU Taifa, Daniel Joachim, alitoa tamko hilo wakati wa kikao hicho kilichofanyika mkoani hapa mwishoni mwa wiki, ambapo pamoja na mambo mengine, alieleza baraza hilo limezingatia hotuba ya Rais aliyotoa wakati wa kilele cha sherehe za Mei Mosi mwaka huu, kuhusu utaratibu wa kisheria unaoendelea kwa wafanyakazi wa sekta binafsi.

“Kufuatia tamko la Rais mkoani Singida, tunamuomba waziri mwenye dhamana kuharakisha mchakato wa utafiti wa kima cha chini cha mshahara sekta binafsi na kitangazwe kwenye gazeti la serikali ili kianze kutumika sambamba na kile cha watumishi wa umma kitakachoanza Julai Mosi mwaka huu,” alisema Joachim  na kuongeza;

“Wakati wa mchakato huo baraza linamuomba waziri mwenye dhamana pamoja na bodi ya kima cha chini cha mshahara sekta binafsi ifanye maandalizi hayo kwa kuzingatia maoni ya wadau ambao ni waajiri na wafanyakazi.”

Aidha, baraza hilo limewaomba waajiri wote kuzingatia takwa la sheria la majadiliano mahali pa kazi ili kuboresha maslahi ya wafanyakazi kupitia mikataba ya hali bora za kazi kwa mujibu wa kifungu cha 68 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini sura ya 366.

Katika hatua nyingine, Tpawu imekemea na kulaani vitendo vya baadhi ya waajiri ambao hutumia kima cha chini cha sekta husika kama sababu ya wao kutoongeza mishahara, jambo ambalo halikubaliki.

“Huu ni mtazamo potofu sababu unakwamisha lengo la kutungwa kwa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, pamoja na Mkataba wa Shirika la Kazi Duniani Na. 98 vinavyotoa haki ya majadiliano mahali pa kazi,” alisisitiza Joachim

Hata hivyo, alimsihi Rais Samia kusaidia wafanyakazi wa sekta binafsi hasa sekta ya kilimo kupata mshahara unaoweza kuwasaidia kumudu gharama za maisha ya kila siku-mathalani-ikiwa sekta ya umma watalipwa kima cha chini Tsh.500,000 basi sekta binafsi kima cha chini kabisa kisipungue Tsh.350,000 kwa mwezi.Katibu Mkuu TPAWU Taifa John Vahaye akizungumza kwenye kikao hicho.Wajumbe Baraza Kuu TPAWU Taifa wakiimba wimbo wa mshikamano kwenye kikao hicho

Wajumbe Baraza Kuu TPAWU Taifa wakifuatilia ajenda mbalimbali kwenye kikao hicho.Wajumbe Baraza Kuu TPAWU Taifa wakiimba wimbo wa mshikamano kwenye kikao hicho 

MITAA 58 HALMASHAURI YA MJI WA TARIME IMEFIKIWA NA UMEME-MHE KAPINGA

May 27, 2025 Add Comment


📌 *Ni kati ya mitaa 81 ya Halmashauri  ya Mji wa Tarime*


*📌  Asema kazi ya kupeleka umeme vitongojini ni endelevu*


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali imefikisha  umeme kwenye mitaa 58 ya Mji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kati ya mitaa 81 ya Halmashauri hiyo.


Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Mei 26, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Tarime Mjini, Mhe. Michael Kembaki aliyeuliza Serikali itapeleka lini umeme katika mitaa 18 ya Halmashauri ya Mji wa Tarime. 

 

"Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Mji wa Tarime ina mitaa 81, kati ya hiyo mitaa 58 tayari  imefikiwa na umeme, na mitaa 23 bado haijafikiwa na umeme."  Amesema  Kapinga


Ameongeza kuwa, mitaa 13 inapelekewa umeme kupitia mradi wa Hamlets Electrification Project - IIA (HEP IIA) unaotekelezwa na Mkandarasi Dyname Construction Engineering,  na mitaa 10 iliyobaki itafikishiwa umeme katika miradi inayofuata.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu Wanawake (UWT), Mhe. Zaytuni Swai aliyeuliza kuhusu jinsi  Serikali ilivyojipanga  kupeleka umeme maeneo ya pembezoni mwa mji wa Arusha hususan kwenye Kata ya Telat, Mhe. Kapinga ameeleza kuwa, Serikali inatekeleza miradi mbalimbali katika maeneo ya pembezoni  (Peri Urban)  kupitia Wakala wa Nishati Vijijini  (REA) ambayo lengo lake ni kusambaza  umeme maeneo ya pembezoni mwa mji.


Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Cecilia Pareso alyeuliza kuhusu Vitongoji vya Wilaya ya Karatu kutokuwa na umeme na vichache vilivyo kwenye mradi kupelekewa nguzo 40 ambazo hazitoshelezi mahutaji na kuiomba Serikali  kuongeza idadi hiyo, Mhe. Kapinga amesema kuwa kwa kawaida miradi ya Vitongoji inawigo kulingana na kazi aliyopewa  Mkandarasi, hata hivyo amesema  kuwa Wilaya ya Karatu ipo katika mradi wa Vitongoji 9,000 ambao utaanza kutekelezwa hivi karibuni na kusisitiza kuwa, miradi ya kupeleka umeme kwenye Vitongoji ni endelevu.