RAIS SAMIA AELEKEA DODOMA KWA TRENI YA SGR KUSHIRIKI ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KATIKA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

May 17, 2025 Add Comment

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisafiri kwa treni ya SGR kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma ambapo pamoja na majukumu mengine pia atashiriki  zoezi la uboreshaji wa taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura leo tarehe 17 Mei, 2025 katika Ofisi ya Serikali ya Kijiji, Chamwino mkoani Dodoma.



MWALIMU ASHEHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA NA WATOTO WENYE UHITAJI ,RAIS SAMIA ATAJWA

May 17, 2025 Add Comment


CDE Mwalimu Nebu Malekela (katikati), wa Shule ya Msingi Magereza iliyopo Tukuyu Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya akikata keki wakati wa sherehe ya kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa aliyo sherehekea na watoto wenye uhitaji wanaolelewa Kituo cha malezi ya watoto hao Hospitali ya Igogwe Mei 12, 2025. Kushoto ni Mlezi wa kituo hicho, Sister Gloria Mwanjelila.

...................................

Na Dotto Mwaibale

JAMII imetakiwa kujenga tabia ya kusaidia watu wenye uhitaji hasa watoto kwani inasaidia kuwapa faraja na kujiona kama watoto wengine wanaoishi na familia zao.

Ombi hilo limetolewa na Mlezi wa Kituo cha kulea watoto wenye uhitaji katika Hospitali ya Igogwe iliyopo Kiwira Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya, Sister Gloria Mwanjelila wakati wa sherehe ya kuzaliwa kwa Cde. Mwalimu Nebu Malekela wa Shule ya Msingi Magereza Tukuyu Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya iliyofanyika Mei 12, 2025.

“Hawa watoto wanahitaji faraja kama wanayopata watoto wengine katika familia zao jamii inapokuja kuwatembelea na kushiriki nao kwa mambo mbalimbali kwao inakuwa faraja kubwa na si lazima mpaka kutoa msaada wa vitu ingawa ni wa muhimu kulingana na mahitaji yao mbalimbali,” alisema Mwanjelila.

Akimzungumzia Mwalimu huyo alisema amekuwa ni mtu wa kujitoa mara kwa mara kutembelea kituo hicho na kutoa msaada kwa watoto hao na kueleza kuwa hata wakati wa kusherehekea sikukuu ya pasaka alifika katika kituo hicho na kuwaletea vitu mbalimbali akiwa ameongoza na wanajumbe Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM ) kutoka Kata ya Kiwira baada ya kuratibu tukio hilo.

“Hawa watoto ni wa jamii nzima na ndio tunaowategemea kuwa viongozi wa kesho sisi kama walezi wao hatuwezi kuwatoshelezea mahitaji yao yote hivyo kwa pamoja tukishirikiana tutaweza kuwapatia mahitaji yao mengine ambayo wanayakosa kutoka kwetu,” alisema mlezi huyo.

Alisema Serikali chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanaznia Dkt. Samia Suluhu Hassan haiwezi kuvihudumia vituo vyote vyenye wahitaji hapa nchini hivyo ni vema jamii ikajenga utamaduni wa kusaidia eneo hilo ikiwa ni kuungamkono jitihada hizo za Serikali

Akizungumza wakati wa sherehe hiyo Mwalimu Nebu Malekela alisema aliona sherehe ya kumbukizi yake ya kuzaliwa afike katika kituo hicho na kusherehekea na watoto hao kwa kukata keki pamoja ambapo pia aliwapelekea zawadi.

“Lilikuwa tukio dogo lakini lenye furaha tulikata keki , tukala, kunywa, kuimba na kucheza pamoja na watoto hakika tuli ‘enjoy’sana,” alisema Mwalimu Malekela.

Ndugu zangu wanajamii Neno la Mungu linasema dunia na vyote vilivyopo ni mali ya Mungu pamoja na wewe mwenyewe na hata akiamua kuichukua mali zake atazichukua zote lakini kwa upendo mkubwa ametupa akili ya kuimiliki mali hiyo na zaidi ya yote akatupa nafasi ya kumrudishia sehemu ndogo tu ya mali zetu akituhitaji kuwasaidia wahitaji badala yake na ndio maana anatoa nafasi kwa wenye kitu kidogo kulisaidia kundi hilo kwani kutoa ni moyo na wala sio utajiri.

Mwalimu Nebu Malekela  akionesha upendo kwa kumlisha keki mmoja wa watoto wa kituo hichoMwalimu Nebu Malekela akiwa katika picha ya pamoja na watoto hao wenye uhitaji

MKURUGENZI MKUU REA AISISITIZA BODI MPYA YA ZABUNI KUFUATA SHERIA, KANUNI NA TARATIBU

May 17, 2025 Add Comment
-Aipongeza Bodi ya Zabuni iliyomaliza muda wake kwa kazi nzuri iliyofanya

INEC YATAKA VIONGOZI MIKOA 16 KUSHIRIKI KUONDOA WALIOKOSA SIFA

May 17, 2025 Add Comment

 

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Vunja nazi, Omary Mngwali kutoka Wilayani Mafia mkoani Pwani  akimuonesha Mwenyekiti wa Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele orodha yawatu wasio stahili kuwepo kwenye Daftari. 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akitazama Mwandikishaji Msaidizi katika Kituo cha Kata ya Kilindoni kilichopo Shule ya Msingi Kilimani akichukua taarifa za watu waliopoteza sifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa Vunja nazi, Omary Mngwali wakati Mwenyekiti wa Tume alipotembelea vituo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Mkoani Pwani leo Mei 16, 2025 kuangalia mwenendo wa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura linaloendelea katika mikoa 16. (Picha na INEC).

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Vunja nazi, Omary Mngwali kutoka Wilayani Mafia mkoani Pwani akitazama daftari la Awali la Wapiga Kura.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akikagua mwenendo wa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili wakati akitembelea vituo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Mkoani Pwani leo Mei 16, 2025(Picha na INEC).


Mkazi wa Mafia Mkoani Pwani akichukuliwa picha baada ya kujitokeza kuboresha taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akimkabidhi kadi mmoja wa wananchi aliyefika katika kituo cha Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili wakati akitembelea vituo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Mkoani Pwani leo Mei 16, 2025(Picha na INEC).


Mwenyekiti wa Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akikagua mwenendo wa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili wakati akitembelea vituo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Mkoani Pwani leo Mei 16, 2025(Picha na INEC).


Na Mwandishi wetu, Mafia
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka viongozi wa Mitaa na Vijiji pamoja na wananchi kwa ujumla katika mikoa 16 inayoendelea na zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kushirikiana na watendaji wa zoezi hilo vituoni kutoa taarifa za Wapiga Kura waliopoteza sifa za kuwepo katuika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
 
Akiwa Wilayani Mafia, Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele, alishuhudia wenye viti wa Mitaa katika vituo mbalimbali alivyopita wakiwaondoa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika zoezi linaloendelea la Uboreshaji wa Daftari awamu ya pili.
 
Akizungumza baada ya kutembelea Vituo vya Uboreshaji Wilayani humo, Jaji Mwambegele aliwa pongeza viongozi wa serikali za mitaa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mafia mkoani Pwani wanavyoshiriki katikia uhakiki wa Daftari la awali la Wapiga Kura na kubaini watu ambao wamepotesa sifa hivyo kuwatolea taarifa na kuondolewa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
 
“Viongozi wa hapa Mafia wamejitokeza vizuri kuja na orodha ya watu wasiostahili tena kuwepo kwenye Daftari, sasa nawasihi viongozi katika mikoa hii 16 hapa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar pale ambapo wanaona kuna mwenyeji wao amepoteza sifa za kuwemo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura basi wasisite kuja kujitokeza na kufuta taarifa zao,”alisema Jaji Mwambegele.
 
Aidha, Jaji Mwambegele amesema zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika mikoa yote 16 limeanza vizuri na vituo vimefunguliwa kwa wakati na kuwataka wananchi ambao hawakupata fursa ya kujiandikisha hapo awali basi wafanye hivyo sasa ili wapate fursa ya kushiriki katika Uchaguzi Mwezi oktoba mwaka huu.
 
Afisa Mwadikishaji wa Jimbo la Mafia, Mohamed Hussein Othman akizungumzia zoezi hilo amesema limeanza vyema katika vituo vyote 15 ndani ya jimbo hilo na wananchi waliokosa fursa ya kujiandikisha na kuboresha taarifa zao hapo awali wanajitokeza hivi sasa.
 
“Zoezi letu la Uboreshaji wa daftari la Kudumu la Wapiga Kura limeanza vizuri, vituo vyote 15 vimefunguliwa saa 2:00 asubuhi wananchi wanajitokeza kuboresha taarifa zao na wale ambao hawakupata fursa katika uboreshaji wa awamu ya kwanza nao wanajitokeza kuhakikisha kwamba wanakuwepo katika Dafrari la Kudumu la Wapiga Kura,”alisema Othman.
 
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Vunja nazi kilichopo Kata ya Kilindoni Wilayani Mafia, Mwl. Omar Mngwali amesema yeye amekua kiongozi katika kitongoji hicho kwa muda mrefu na kushiriki vyema katika shughuli za kijamii imemuwezsha kutambua watu wake waliopoteza sifa wapatao 11 na kutoa taarifa ili waondolewe kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
 
Mzunguko wa pili wa uboreshaji umeanza leo Mei 16 na utaenda hadi Mei 22, 2025 unahusisha mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Kaskazini Pemba na Kusini Pemba ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 16 hadi 22, 2025.
 
Zoezi hilo linakwenda sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la awali la Wapiga Kura ambapo  wananchi watapata fursa ya kukagua, kufanya marekebisho ya taarifa za wapiga kura na uwekaji wa pingamizi dhidi ya wapiga kura waliomo kwenye daftari ambao hawana sifa na litabandikwa katika vituo vyote vilivyotumika wakati wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza.
 
Vituo vinafunguliwa Saa 2:00 asubuhi na kufungwa Saa 12:00 jioni kila siku kwa siku zote saba za utekelezaji wa zoezi hilo.

Dkt. Mpango azindua Shule ya Sekondari ya Mfano ya Benki ya CRDB, Benki hiyo ikitimiza Miaka 30

May 17, 2025 Add Comment

 

Arusha 16 Mei 2025 - Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango, amezindua rasmi Shule ya Sekondari ya Mfano ya Benki ya CRDB, itayojengwa katika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 ya Benki ya CRDB.

Shule hiyo ya kisasa ni matokeo ya dhamira ya Benki hiyo ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuwekeza kwenye elimu bora kwa watoto wa Kitanzania.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa shule hiyo uliofanyika katika seimna ya wanahisa wa Benki ya CRDB kuelekea Mkutano Mkuu, Dkt. Mpango aliipongeza Benki ya CRDB kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya kijamii, hususan sekta ya elimu.
“Nawapongeza kwa kuwa mfano wa kuigwa kwa sekta binafsi. Mmekuwa mstari wa mbele sio tu kwenye huduma za kifedha bali pia katika kuleta mabadiliko ya kweli kwenye jamii,” alisema Dkt. Mpango huku akiipongeza benki hiyo pia kwa kutimiza miaka 30 tokea kuanzishwa kwake mwaka 1996.


Akizungumza katika semina hiyo ya wanahisa, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay, tangu kuanzishwa kwake mwaka 1996, Benki ya CRDB imeendelea kuwa mshirika muhimu wa maendeleo kwa Taifa kwa kutoa huduma za kifedha zenye kugusa maisha ya wananchi moja kwa moja.
Shule ya Sekondari ya Mfano ya Benki ya CRDB ina uwezo wa kuchukua wanafunzi zaidi ya 600 na imejengwa kwa viwango vya kisasa ikiwa na madarasa ya kisasa 16, maabara 4, maktaba 1 chumba cha TEHAMA 1, ofisi za walimu na wafanyakazi 11, vyoo 53, miundombinu rafiki kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum, pamoja na maeneo rafiki ya michezo. Mradi huu unatarajiwa kugharimu takribani shilingi bilioni 5.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Mussa Nsekela, alisema shule hiyo ni zawadi ya Benki kwa Watanzania katika kuadhimisha miaka 30 ya mafanikio ya benki hiyo. “Tulipojiuliza ni zawadi gani ya kipekee tungeweza kuwapa Watanzania katika kutimiza miaka 30, tulikubaliana kwamba elimu ni urithi wenye nguvu kuliko wote. Shule hii ni ushahidi wa dhamira yetu ya kuwekeza katika kizazi kijacho,” alisema Nsekela.
Nsekela aliongeza kuwa shule hiyo ni sehemu ya mpango mpana wa Benki ya CRDB wa kurudisha kwa jamii katika nyanja za ya elimu, afya, mazingira na uwezeshaji wanawake kupitia CRDB Bank Foundation. “Tunaamini kuwa maendeleo endelevu hayawezi kufikiwa bila uwekezaji wa makusudi katika elimu. Kupitia shule hii, tunaweka msingi wa taifa lenye maarifa, maadili na ushindani wa kimataifa,” alibainisha.
Akitoa salamu zake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda (Mb), aliishukuru Benki ya CRDB kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya sekta ya elimu nchini. “Kwa niaba ya Serikali na Wizara ya Elimu, naishukuru sana Benki ya CRDB kwa maono na uamuzi huu wa kujenga shule ya kisasa kwa ajili ya watoto wa Kitanzania. Huu ni mfano hai wa jinsi sekta binafsi inavyoweza kushirikiana na Serikali katika kujenga musatakabali bora kwa watoto na vijana wetu.”
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa CRDB Bank Foundation, Martin Warioba, alisema shule hiyo ni sehemu ya mkakati mpana wa Benki ya CRDB kuboresha mazingira ya elimu nchini na kufungua fursa kwa watoto wa Kitanzania. “Mbali na kujenga shule hii ya mfano, tumejipanga pia kuanzisha mpango wa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi kwa kushirikiana na Wizara ya elimu.”

Uzinduzi wa shule hiyo unachukuliwa kama alama ya mafanikio ya miaka 30 ya Benki ya CRDB, na uthibitisho wa maono yake ya kujenga taifa lenye misingi imara ya elimu, usawa na maendeleo endelevu. “Tunajivunia kuona uwekezaji wetu ukiendelea kuzaa faida zaidi katika jamii,” alisema mmoja ya Wanahisa waliohudhuria semina hiyo.
Wanahisa wa Benki ya CRDB watafanya Mkutano Mkuu wa 30 kesho ambapo ajenda mbalimbali zinatarajiwa kujadiliwa ikiwamo kuidhinisha pendekezo la bodi ya wakurugenzi la gawio la shilingi 65 kwa hisa ikiwa ni ongezeko la asilimia 30 kulinganisha na gawio la shilingi 50 kwa hisa lililotolewa kwa mwaka 2023.