Showing posts with label michezo. Show all posts
Showing posts with label michezo. Show all posts
WAZIRI MCHENGERWA AONGOZA KIKAO CHA UJUMBE WA TANZANIA BIRMINGHAM UINGEREZA
michezo




Na John Mapepele
Waziri
wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohammed Mchengerwa ameongoza
kikao cha maandalizi ya ujumbe wa Tanzania katika kikao cha Mawaziri wa
Michezo wa Jumuiya ya Madola kitakachoanza leo Julai 26 mjini
Birmingham, Uingereza.
Kikao
hicho ni maandakizi mahususi kabla ya uzinduzi rasmi wa mashindano ya
michezo ya Jumuiya ya Madola ya mwaka huu yanayofanyika nchini Uingereza
huku Tanzania ikiwa imeshiriki katika michezo hiyo.
Katika
mashindano hayo kwa mara ya kwanza Serikali imetoa motisha kubwa kwa
wachezaji watakaofanya vizuri na kurejea na tuzo nchini.
Mhe. Mchengerwa amesema dhamira ya Serikali ni kuhakikisha michezo inatumika kikakamilifu kuitangaza Tanzania kimataifa.
Aidha,
amesema michezo ni ajira na uchumi mkubwa ambapo amesisitiza wachezaji
wote kuwa wazalendo kujituma kufa na kupona kwa ajili ya taifa la
Tanzania.
Amepongeza
jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali chini ya Rais Samia Suluhu
Hassan za kuleta mapinduzi makubwa kwenye sekta za michezo katika
kipindi kifupi iliyopo madarakani.
Miongoni
mwa motisha hizo amesema Serikali itatoa kiasi cha dola 10,000 za
kimarekani kwa mchezaji atakayerejea na medali ya dhahabu, dola 7000 kwa
medali ya Shaba na dola 5000 kwa medali ya fedha.
Kikao
hicho kimehudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Dkt,
Asha-Rose Migiro, Mhe. Mussa Sima ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara
ya Michezo Ndugu Saidi Yakubu pamoja na wajumbe kutoka Tanzania.
WAZIRI MCHENGERWA AMWAGA VIFAA VYA MICHEZO SHULE ZOTE WILAYA YA RUFIJI,AANZISHA LIGI YA SENSA
michezo
Na John Mapepele
Waziri
wa Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Jimbo la Rufiji. Mhe,
Mohamed Omary Mchengerwa ametoa vifaa vya michezo kwa shule zote za
msingi na Sekondari na wanafunzi wanamichezo wote wanaoshiriki kwenye
mashindano ya michezo kwa shule za Msingi (UMITASHUMTA) na Mashindano
ya Shule za Sekondari (UMISSETA) kwa mwaka 2022 Wilaya ya Rufiji.
Mhe.
Mchengerwa amekabidhi vifaa hivyo kwa Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Julai
17, 2022 kwenye shule ya Sekondari ya Ikwiriri Wilaya ya Rufiji
ambapo amesema ameamua kufadhili vifaa hivyo katika Wilaya ya Rufiji
ili kuiendeleza michezo kwa kuwa michezo ni biashara na ajira kubwa
kwa vijana.
“Nimeamua
kusaidia vifaa hivi kwakuwa natambua kwa sasa michezo ni miongoni mwa
chanzo cha ajira na biashara kubwa duniani hivyo ni vema kufanya michezo
kwa umakini mkubwa ili kujipatia ajira” amefafanua
Amewataka wachezaji hao kuwa na nidhamu na kujituma kwa kufanya mazoezi ili waweze kushinda kwenye mashindano mbalimbali.
“Nendeni
mkajitume, michezo ni ajira na furaha wasikilizeni walimu wenu, hata
shuleni mtafanya vizuri”amesisitiza Mhe. Mchengerwa.
Aidha
amesema dhamila ya Serikali kwa sasa ni kuendeleza michezo ambapo
amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu
Hassan kwa jitihada kubwa anazofanya kwenye michezo katika kipindi
kifupi cha utawala wake ambazo zimeleta mapinduzi makubwa kwenye sekta
hiyo.
Vifaa hivyo vimegharimu zaidi ya milioni 23 ambazo zimenunua zaidi ya jezi seti 200, trakisuti pea 100, kofia 200 na mipira 100.
Pia
amefadhili Ligi ya mpira wa miguu ya sensa katika Wilaya ya Rufiji
ambapo ametoa seti 6 za jezi kwa timu sita na mipira 12 kwa ajili ya
mashindano hayo.
Amesema
lengo la mashindano hayo ni kuhamasisha wananchi kushiriki
kuhesabiwa kwenye sensa ya kitaifa yam waka huu kwa manufaa mapana ya
wananchi wa Rufiji na Taifa kwa ujumla.
Aidha,
amewahimiza wananchi wa Wilaya ya Rufiji na watanzania wote kujitokeza
kwa wingi Agosti 23, mwaka huu kuhesabiwa kwenye zoezi la sensa kitaifa.
Mwenyekiti
wa Halimashauri ya Wilaya ya Rufiji amemshukuru Mhe. Mchengerwa kwa
jitihada zake na mchango wake kwenye sekta ya michezo ambapo
amemhakikishia kuwa michango anayotoa itatumika vizuri ili kupata
matokeo chanya.
WAZIRI MCHENGERWA AIPONGEZA TIMU YA KRIKETI KUTWAA UBINGWA RWANDA, AMSHUKURU RAIS SAMIA
michezo
Na John Mapepele
Waziri
wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa pongezi
kwa Timu ya Tanzania ya Wanawake ya Kriketi kwa kutwaa Ubingwa leo
Juni 18, 2022 kwenye mashindano ya Kwibuka Cup nchini Rwanda,
yaliyoshirikisha nchi nane ( Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Botswana ,
Nigeria, Brazil na Ujerumani) bila kufungwa na timu yoyote.
Aidha, amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa mchango wake mkubwa anaoutoa katika michezo.
Amesema
hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuboresha michezo kwa kuweka
mikakati kabambe chini ya uongozi wa Samia imeleta matokeo chanya
kwenye sekta za michezo na sanaa hapa nchini.
Amesema
taarifa ya hali ya uchumi wa nchi iliyosomwa bungeni hivi karibuni
imeonesha kuwa sanaa na burudani zimechangia kwa asilimia 19.4 katika
kipindi cha mwaka 2021 na kuziacha kwa mbali sekta mbalimbali.
Amesema
dhamira ya Serikali kwa sasa ni kuifanya michezo kuwa uchumi badala
mazoe ya kuifanya michezo kama kitu cha burudani pekee.
Aidha,
amesema Serikali tayari inazigharimia timu zote za taifa zinazojiandaa
kwa ajili ya mashindano ya kimataifa kwa kuziweka kambini kuanzia mwanzo
wa mwaka huu.
Hivi
karibuni Mhe. Mchengerwa amekaririwa vyombo vya habari akisisitiza kuwa
michezo na sanaa ni uchumi hivyo wanamichezo na wasanii wanapaswa
kutambua kuwa vipaji walivyonavyo ni mtaji wa maisha yao.
Ujumbe
wa Klabu ya Southampton uliokutana na Mhe. Waziri Mchengerwa na kufanya
mazungumzo ya kuinua michezo ulioongozwa na Mkuu wa Idara ya Biashara
ya klabu hiyo David Thomas pia ulimpongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan
kwa kazi kubwa anayoifanya kwenye michezo na kumzawadia jezi ambayo
ilipokelewa kwa niaba yake na Mhe. Mchengerwa.
SOUTHAMPTON KUWANOA MAKOCHA WA TANZANIA -WAZIRI MCHENGERWA
michezoWaziri
wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amesema
Tanzania inakwenda kushirikiana na klabu ya Soka ya Southampton
kuwandaa makocha wa soka ili wawe kwenye kiwango cha kimataifa.
Mhe.
Mchengerwa amesema haya leo juni 17, 2022 ofisini kwake akiambatana na
Katibu Mkuu wa Wizara yake, Dk. Hassan Abbasi wakati alipokutana na
ujumbe wa Klabu hiyo ulioongozwa na Afisa Biashara Mkuu wa Klabu hiyo
David Thomas.
Amesema
dhamira ya Serikali ni kuona kuwa michezo mbalimbali inasimamiwa
kisayansi ili kuleta tija ikiwa ni pamoja na kuwa na makocha ambao
watasaidia kufundisha timu za micherzo ili kufuka kwenye kiwango cha
kimataifa.
Katika
kikao hicho wamekubalina kuwa Timu ya soka ya ya Wanawake chini ya
Miaka 17 (Serengeti Girls) itakwenda kupatiwa mafunzo maalum kwenye
Klabu hiyo ikiwa ni maandalizi ya kwenda kwenye mashindano ya kombe la
dunia nchini India.
Katika
tukio hilo ujumbe wa timu hiyo ulimzawadia jezi Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania. Mhe Samia Suluhu Hassan ikiwa ni kuthamini mchango
wake mkubwa anaoutoa kuendeleza michezo nchini.
Subscribe to:
Posts (Atom)