Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

WASIRA: VIONGOZI WA VIJIJI,VITONGOJI MSIWARUHUSU WAGENI KUPORA ARDHI

March 25, 2025 Add Comment

 

                                                      Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Karagwe

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Stephen Wasira, amewataka viongozi wa vijiji na vitongoji kutowaruhu wageni kutoka nchi jirani kuingia nchini na kuweka makazi ya kudumu kwa kuwa madhara yake ni makubwa kwa siku za baadaye.


Aidha, Wasira ameahidi kulifikisha suala hilo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa alitafute ufumbuzi wa haraka kuhakikisha wageni wote wanazingatia na kufuata utaratibu sahihi wa kuingia na kuishi nchini.

Wasira ameyaleza hayo leo Machi 23, 2025 alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM Wilaya ya Karagwe na Kyerwa mkoani Kagera ambao walimweleza kuwa kuna wageni kutoka nchi jirani wanapora ardhi ya Watanzania katika baadhi ya maeneo ya wilaya hizo.

“Nataka kuwaambia viongozi wetu wa vijiji na vitongoji msiwakaribishe, hatuwazuii kuja kwetu lakini waje kwa kufuata utaratibu. Mkiwaruhusu wakaingia wakajenga nyumba tena za kudumu siku ya kuwatoa itakuwa vita na watasema kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe, kumbe kuna vita ya wageni na Watanzania walionyang’anywa ardhi,” ameema.

Amesisitiza kuwa kama kuna jambo gumu duniani ni ardhi, hivyo wananchi wa mipakani wakiruhusu ikaangiliwa itakuja kuleta shida hapo baadaye kwa kuwa ardhi haiongezeki, lakini watu wanaongezeka.

“Kama kuna jambo gumu duniani ni ardhi, mkiruhusu ardhi yenu ikaingiliwa, mnasema kubwa, huku mnazaa namna hii, watu wanaongezeka kwa asilimia tatu kwa mwaka. Wakati nchi inapata uhuru tulikuwa milioni nane lakini leo tuko watu milioni 63, hawa ni watu wengi wanaongezeka.

“Ardhi inabaki ile ile, kwa hiyo msisherehekee jambo hili, sisi tuliwapeni viongozi wa vijiji na vitongoji mamlaka ya kusimamia hakikisheni hawa wageni hawapewi ardhi na hawaingii bila utaratibu.

“Tunawaambia kabisa na hatuna ugomvi kule wanakotoka sisi ni rafiki zetu, lakini na sisi tukitoka hapa Karagwe tukahamia kule watatufukuza tena watatufukuza haraka maana wako wengi na ardhi yao ni ndogo, nchi yao ina watu milioni 12 lakini ukubwa wake ni unazidiwa na Mkoa wa Kagera,” amesema.






TCAA YAJENGA MSHIKAMANO KUPITIA FUTARI NA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM

March 25, 2025 Add Comment

 Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imeandaa hafla maalumu ya futari kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka Shule ya Msingi Mzambarauni. Tukio hili limeleta faraja kwa wanafunzi hao na kuonyesha namna sekta ya usafiri wa anga inavyoweza kuchangia ustawi wa jamii.


Hafla hiyo, iliyofanyika katika Makao Makuu ya TCAA jijini Dar es Salaam, ilihudhuriwa na viongozi wa mamlaka hiyo pamoja na wadau wa sekta ya anga. Wanafunzi walipata fursa ya kushiriki chakula cha futari na kupokea zawadi kama sehemu ya mshikamano na upendo kutoka kwa jamii inayowazunguka.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Salim Msangi, alisema kuwa jukumu la taasisi hiyo si tu kusimamia sekta ya usafiri wa anga, bali pia kuhakikisha kuwa jamii inayozunguka inapata msaada na faraja inapohitaji. Alisisitiza kuwa kuwajali watoto wenye mahitaji maalum ni sehemu ya dhamira ya TCAA ya kuwa taasisi yenye mchango chanya kwa jamii.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari, alisisitiza umuhimu wa mshikamano katika jamii, akisema kuwa hatua kama hizi huleta matumaini kwa watoto na kuimarisha uhusiano wa kijamii.

Kwa wanafunzi wa Shule ya Mzambarauni, hafla hii ilikuwa zaidi ya futari, kwani iliwapa nafasi ya kujiona kuwa sehemu muhimu ya jamii. Baadhi yao walieleza furaha yao kwa kukutana na viongozi wa sekta ya anga na kuelewa zaidi kuhusu fursa zilizopo katika sekta hiyo.

Kupitia hafla hii, TCAA imeonyesha kuwa sekta ya usafiri wa anga si tu kuhusu uendeshaji wa ndege, bali pia ni sehemu ya jamii inayojali na kushiriki katika kuleta mabadiliko chanya kwa makundi yote.
Mgeni rasmi Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Salim Msangi wakikabidhi mkono wa Sikukuu ya Eid kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka Shule ya Msingi Mzambarauni wakati wa futari iliyoandaliwa na TCAA.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Salim Msangi akitoa mkono wa Sikukuu ya Eid kwa mlezi wa wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka Shule ya Msingi Mzambarauni wakati wa futari iliyoandaliwa na TCAA. Mgeni rasmi Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari akishuhudia tukio hilo.
Mgeni rasmi Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Salim Msangi wakipata futari pamoja na wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka Shule ya Msingi Mzambarauni wakati wa futari iliyoandaliwa na TCAA.
Mgeni rasmi Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari akitoa neno wakati wa futari iliyoandaliwa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Salim Msangi akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), wadau mbalimbali wa Usafiri wa Anga pamoja na wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka Shule ya Msingi Mzambarauni
wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na TCAA.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Juma Hassan Fimbo akitoa neno wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na TCAA.
Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), wadau mbalimbali wa Usafiri wa Anga pamoja na wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka Shule ya Msingi Mzambarauni wakiwa kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na TCAA.

DKT.BITEKO AWAPONGEZA WABUNGE KWA KUWASEMEA WATANZANIA

March 24, 2025 Add Comment


📌 *Asema Serikali itaendelea kuwawezesha wazawa kushiriki miradi ya nishati*


📌*Asema sekta ya nishati imepiga hatua kubwa*


*Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewapongeza waheshimiwa wabunge kwa kuihimiza Serikali kuendelea kuwezesha wazawa kushiriki katika utekelezaji wa miradi ya sekta ya nishati.


Dkt. Biteko amesema hayo leo Machi 24, 2025 wakati akijibu hoja za wabunge katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu randama ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2025/26 kilichofanyika bungeni Dodoma.

“ Nakubaliana na wabunge kuhusu kuangalia wazawa na kuwapa nguvu ili waweze kushiriki katika miradi ya nishati, tumekuwa tukifanya hivyo lakini tutaendelea kuangalia wazawa wenye uwezo ili tufanye nao kazi. Ninawashukuru  sana waheshimiwa wabunge kwa kuwasemea Watanzania ili washiriki katika miradi,” amesema Dkt. Biteko

Ameongeza kuwa licha ya kuwa na Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Serikali itaangalia zaidi namna ya kusaidia wazawa katika sekta ya nishati, huku akitolea mfano hatua iliyopigwa katika sekta hiyo. 

Amesema kuwa kwa sasa Serikali imeliwezesha Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kuwa na uwezo kuzalisha na kusambaza umeme nchini kwa kuimarisha mifumo na miundombinu mbalimbali.


“ Mwaka huu unaopita Watanzania 53,000 wamepata ajira katika sekta hii. Tumepokea pia maoni ya waheshimiwa wabunge kuhusu uwepo wa wazawa kwenye kila kampuni inayopewa kazi na kuangalia upya mfumo wa utoaji zabuni,” amesema Dkt. Biteko.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amesema kuwa mara baada ya kukamilisha mradi wa kufua umeme wa Julius Nyerere, Serikali inaanzisha miradi mipya ya kuzalisha umeme kwa kuwa mahitaji ya juu ya umeme yamekuwa yakiongezeka hadi kufikia megawati 253 mwaka 2025.

Aidha, kupitia kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dkt. Mathayo David kimejadili kuhusu randama ya bajeti ya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2025/26.


WIZARA YA NISHATI YATAJA VIPAUMBELE VYA BAJETI YA MWAKA 2025/2026

March 24, 2025 Add Comment


*📌 Rukwa, Kagera, Lindi. Mtwara kuunganishwa na gridi ya Taifa.*


*📌 Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kuendelea kuhamasishwa*


*📌 Serikali kuendelea kuimarisha utendaji wa Taasisi, Mashirika  chini ya Wizara ya Nishati,*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametaja  vipaumbele vya Wizara  ya Nishati katika Bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 ikiwemo kuendelea kutekeleza miradi ya uzalishaji, usafirishaji,  usambazaji  umeme na kufikisha gridi ya Taifa katika Mikoa iliyosalia ya Rukwa, Kagera, Lindi na Mtwara;

Akiwasilisha vipaumbele hivyo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Njshati na Madini, leo jijini Dodoma, Dkt. Biteko amesema  vipaumbele hivyo vimezingatia mpango wa Taifa wa Nishati wa mwaka 2025 hadi 2030.


“Mhe. Mwenyekiti vipaumbele hivi vimezingatia mpango wa Taifa wa Nishati wa mwaka 2025 - 2030 (National Energy Compact 2025 - 2030) utakaosaidia upatikanaji na uunganishaji wa umeme kwa wananchi, kuongeza mchango wa nishati jadidifu katika uzalishaji wa umeme na ushiriki wa Sekta Binafsi katika maendeleo ya Sekta ya Nishati ”. Amesema Dkt. Biteko

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amesema Serikali imewajengea wazawa uwezo mkubwa wa kutekeleza miradi ya umeme huku akitolea mfano wa ajira kwenye miradi ya umeme kufikia idadi ya  53,000.

Amesema  Dunia inahitaji nishati na mahitaji ya umeme yamekuwa yakiongezeka kwa kasi hivyo Serikali itaendelea kuongeza vyanzo vya kuzalisha umeme ili kukidhi mahitaji ya Watanzania.

Awali, Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Wizara ya Nishati, Petro Lyatuu alisema kuwa katika kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa umeme wa uhakika Wizara itaendelea kuimarisha Gridi ya Taifa (National Grid Stabilization Project) pamoja na kufanya matengenezo na ukarabati wa mitambo ya kuzalisha umeme;

“Mhe. Mwenyekiti tutandelea na usambazaji wa nishati katika Vitongoji, maeneo ya migodi, kilimo, viwanda na pampu za maji pamoja na vituo vya afya ili kuwezesha shughuli za

uzalishaji na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.” Aliongeza Lyatuu

Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia Lyatuu alisema Serikali itaendelea kuhamasisha na kuwezesha watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ikiwa ni utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034) na mpango wa Taifa ya Nishati wa mwaka 2025 - 2030 (National Energy Compact 2025 - 2030).

Aliongeza  kuwa Serikali itaendelea na shughuli za utafutaji, uendelezaji na usambazaji wa mafuta na gesi asilia pamoja na kutekeleza miradi ya kielelezo na kimkakati ya mafuta na gesi asilia

ikiwemo Mnazi Bay Kaskazini, Eyasi - Wembere, pamoja na mradi wa Kuchakata na Kusindika Gesi asilia kuwa Kimiminika (Liquefied Natural Gas - LNG Project).


Mradi mwingine ni ujenzi wa Bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania (East African Crude Oil Pipeline - EACOP).


Vile vile, amesisitiza kuwa Serikali itaendela kuimarisha utendaji wa Taasisi na Mashirika yaliyo chini ya Wizara ya TANESCO, REA, TPDC, PBPA, EWURA na PURA pamoja na Kampuni Tanzu ili yatoe huduma bora kwa wadau, kuimarisha mapato pamoja na tija na ufanisi katika uendeshaji;


Amesema lengo lingine ni kuongeza  kiwango cha upatikanaji wa umeme kutoka cha sasa cha asilimia 78.4 hadi kufikia asilimia 100 ifikapo mwaka 2030.


Naye, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. David Mathayo ameipongeza Serikali kwa kuja na vipaumbele vitakavyowawezesha watanzania kuwa na nishati ya uhakika.

IAA YAJIDHATITI KUWEKEZA KWENYE MADARASA MTANDAO MWAKA 2025/2026

March 22, 2025 Add Comment
























MKUU wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Eliamani Sedoyeka amesema IAA katika mwaka wa fedha 2025/2026 imejipanga kuwekeza zaidi ya shilingi bilioni nne(4bilioni) katika teknolojia za kufundishia na kujifunzia ikiwa ni pamoja na madarasa mtandao (smart classes).


Prof. Sedoyeka ameyasema hayo wakati wa Ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) leo Machi 21,2025 katika Kampasi ya Arusha, ziara iliyolenga kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu ya Chuo inayoendelea.


Amesema lengo la uwekezaji ni kuboresha mazingira ya kujifunzia kuendana na kasi ya maendeleo ya TEHAMA katika kuwafikia wanafunzi wengi kwa wakati mmoja, " kupitia 'smart classes' mwalimu ataweza kufundisha akiwa katika Kampasi mojawapo Kati ya Arusha, Dar es Salaam, Babati, Dodoma na Songea na wanafunzi wakajifunza popote walipo".


Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Mhe. Japhet Hasunga amesema uwekezaji utasaidia IAA kuwa Chuo mfano katika kutoa Elimu Kitaifa na kimataifa.


Ameongeza kuwa kupitia madarasa mtandao hata wanafunzi kutoka nje ya nchi wataweza kusoma na yatasaidia wanafunzi kupata Elimu katika ubora unaofanana kwa kuwa Mwalimu mmoja kutoka katika Kampasi moja ataweza kufundisha watu wengi kutoka maeneo tofauti kwa wakati mmoja.


Kwa upande wake mjumbe wa Kamati ya PAC, Mhe. Cendester Sichalwe ambaye ni mhitimu wa IAA, ametoa wito kwa wazazi na Watanzania wote kukiamini Chuo cha Uhasibu Arusha na kukifanya kuwa chaguo lao la kwanza kwa kuwa watakaposoma au kuleta watoto wao watapata Elimu Bora na inayoishi.


"Mimi nimesoma IAA kwa zaidi ya miaka saba naifahamu IAA, natoa wito kwa wanaohitaji kusoma chuo kuja IAA; Chuo hiki kina vielelezo vyote vya kumfanya mhitimu kukabili soko la ajira Kitaifa na Kimataifa; mimi nilivyomaliza Chuo ajira yangu ya kwanza ni kwenye mashirika ya Kimataifa na nimekuwa nikifanya kazi huko pia kabla sijawa mbunge", amesema Sichalwe.


Kadhalika, Mhe. Sichalwe ameongeza kuwa uboreshaji wa miundombinu inayoendelea kufanyika IAA kupitia mapato ya ndani na fedha kutoka serikali Kuu umelenga kuwafanya Watanzania kupata mazingira rafiki yatakayowawezsha kupata Elimu Bora itakayowawezesha kutoa mchango katika maendeleo ya Jamii na Taifa kwa ujumla.