Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

TANGA UWASA KUBORESHA UWEZO WA UZALISHAJI MAJI KUFIKIA LITA MILIONI 60

March 17, 2025 Add Comment


Na Oscar Assenga,TANGA

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) imeweka bayana mpango mkakati wao wa kuboresha uwezo wa uzalishaji wa maji kutoka Lita Milioni 45 mpaka kufikia Lita Milioni 60 pamoja na kuongeza mtandao wa bomba la usambazaji wa maji kwa umbali wa kilomita 60

Mpango huo uliwekwa bayana leo na Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) Alawi Ahmadi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya wiki ya maji iliyoanza Machi 16 hadi Machi 22, 2025 yenye kauli mbiu “Uhifadhi wa uoto wa asili kwa uhakika wa Maji”

Alisema kwamba lengo la mipango hiyo ni kuhakikisha huduma inafika kwa wakazi wote pamoja na utekelezajii wa miradi mkubwa wa uboreshaji wa miundombinu kuanzia eneo la Bwawani,Mtambo wa kutibu maji pamoja na kuendeleza mtandao wa usambazaji maji katika maeneo mbalimbali .

“Tutaboresha uwezo wa kuzalisha maji kwa asilimia 25 ukilinganisha na mahitaji kwa sasa tunaweza kuzalisha maji lita milioni 45 tunataka kuzalisha maji lita milioni 60 kutakuwa na ongezeko la maji lita milioni 15 kwenye uwezo uliopo wa mtambo wetu”Alisema

Aidha alisema kwamba wataongeza pia mtandao wa bomba la usambazaji maji kwa kilomita 60 sasa hivi wana urefu wa kilomita 862 lakini wataongeza kilimota 60 ili kufikia watu wote waliopo kwenye eneo lao lka huduma,

Alisema kwamba mradi huo ulianza tokea mwezi Julai mwaka jana na unatarajia kuisha Desemba mwaka huu ambapao kwa sasa umefikia asilimia 15 kwa maana vifaa vyote vinayotakiwa kutekeleza mradi huo vimewasili eneo la mradi na wakandarasi wamekwisha kuanza kazi kwa maeneo mbalimbali.

“Mradi huu vifaa vyote vinavyotakiwa vimewasili na gharama za mradi huo ni Sh.Bilioni 53.12 ambazo walizipata kwa kuuza hati fungani na kwa sasa utoaji huduma umefikia asilimia 93 ya wakazi wa Jiji ya Tanga, Muheza na Pangani”Alisema

Alisema kupitia kauli mbiu hiyo Tanga Uwasa inapanga kufanya tathimini na kuweka vipaumbele kwenye mambo mbalimbali ikiwemo jitahida zinazofanyika na matokeo ya uhifadhi wa mazingira ili kufanikisha kutunza vyanzo vya maji ili viweze kuwa endelevu.

“Lakini kupunguza athari za uchafuzi wa vyanzo vya maji ili kupunguza athari zake kwa watumiaji na kupunguza gharama za kuyasafisha pamoja na utekelezaji wa miradi ya kuboresha hali ya huduma kwa upande wa maji safi na taka”Alisema

Alisema pia kuendelea na utatuzi wa kero za huduma zinazowapata wananchi kwa sasa katika maeneo mbalimbali ya huduma pamoja na kutoa elimu kwa wateja juu ya huduma kwa kutumia vyombo vya habari, madawati ya huduma kwa wateja.

“Katika wiki ya maadhimisho ya wiki ya maji Tanga Uwasa imejipanga kutoa elimu kwa wateja kuhusu masuala mtambuka ya maji kutumia vyombo vya habari, madawati maalumu ya huduma kwa wateja na kuwatembelea majumbani pamoja na kutoa msahama wa tozo ya kurejesha huduma kwa wateja ambao wamesitishiwa huduma ya maji pamoja na kuruhusiwa kuweka mikataba ya kulipa madeni yao kwa awamu yaani kidogo kidogo”Alisema

Awali akizungumza Kaimu Mkurugenzi wa Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira wa Tanga Uwasa Mhandisi Salum Hamis alisema wana mradi mkubwa wa hati fungani ambapo wana maeneo makubwa manne ambayo yatasaidia kumaliza shida ya maji katika Jiji la Tanga na miji ya Muheza na Pangani.

Alisema kwenye huo mradi wanakwenda kuupanua mtambo wa kusukuma maji mabayani kutoka uwezo wa sasa wa kusumua maji kutoka Lita 42,000 kwa siku mpaka kufika 60,000 kwa siku ikiwemo kujenga bomba linguine kubwa kutoka mabayani mpaka kituo chao cha kusafisha maji Mowe lenye kipenyo cha Milimita 600.

“Sasa hivi wana Bombo lenye milimita 600 na wanaongeza la pili na lingine ni kituo cha kusafisha na kutibu maji Mowe kwa sasa kina uwezo wa kusafisha na kutibu maji kwa uwezo wa mita za ujazo 45,000 kwa siku kwenye huo mradi tunakwenda kukiongeza kufikia uwezo wa mita za ujazo 60,000 kwa siku “Alisema

WASIRA APELEKA HABARI NJEMA TUNDUMA KUHUSU UPATIKANAJI WA MAJI,UPANUZI WA BARABARA

March 16, 2025 Add Comment

 Na Said Mwishehe,Tunduma


MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Stephen Wasira amewahakikishia wananchi wa Tunduma Mkoani Songwe kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan iitahakikisha inatatua changamoto ya uhaba wa maji katika eneo hilo na Mkoa kwa ujumla.

Amesema katika kutatua changamoto ya maji Machi 20 mwaka huu Waziri wa Maji Jumaa Aweso na Waziri wa Fedha Dk.Mwigulu Nchemba watakuwa Tunduma kwa ajili ya kuingia makubaliano na mkandarasi atayekajenga Mradi wa maji kwa ajili ya kutatua kero hiyo.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mji wa Tunduma Mkoani Songwe ,Wasira amesema tayari Serikali imewekq mkakati wa kumaliza changamoto ya uhaba wa maji kupitia Mradi huo ambao utaanza kutekelezwa baada ya mkandarasi kusaini mkataba wa kutekeleza ujenzi wa mradi huo.

“Nimekuja hapa kuwawmbia changamoto hii ya maji ambayo ni ya muda mrefu ya uhaba wa maji inakwenda kupata ufumbuzi.Machi 20 mwaka huu mawaziri wawili wa maji na fedha watakuja kusaini mkataba na mkandarasi atakayejenga mradi huo.”

Kuhusu kero ya msongamano wa malori ,Wasira amesema atawasiliana na Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega ili kuhakikisha upanuzi wa barabara wa njia katika Mji wa Tunduma unatekelezwa kama ambavyo Ilani ya Uchaguzi Mkuu inavyoelekeza.

Amesema atamshauri Waziri wa Ujenzi kuhakikisha kunakuwa na mkandarasi ambaye atajenga kuanzia Tunduma ili wakutane kati na mkandarasi ambaye ameanza kujenga barabara ya njia nje mkoani Mbeya lengo likiwa ni kuwezesha ujenzi wa barabara kujengwa kwa kasi na hatimaye kuondoa changamoto ya msongamano wa malori.

“Wakati nakuja Tunduma nilikuwa namtafuta Waziri wa Ujenzi katika simu yake ili kuzungumza naye kuona umuhimu wa kuwa na mkandarasi ambaye atajenga kipande cha kuanzia hapa Tunduma.Hivyo nikirudi nitakwenda kuzungumza naye kuhusu hili.”amesema na kufafanua ujenzi wa upanuzi wa brabara hiyo tayari umeanza mkoani Mbeya.

Katika hatua nyingine Wasira ametumia nafasi hiyo kuzungumzia kuhusu malalamiko ya bodaboda kusumbuliwa na Polisi wa usalama barabarani ambapo amewataka bodaboda kupunguza makosa ya barabarani ili wasisumbuliwe lakini wakati huo huo Polisi nao kulegeza masharti kidogo ili wazungumze lugha moja.




PURA YAONGEZA JITIHADA KUFUNGAMANISHA SEKTA YA MAFUTA NA GESI NA SEKTA YA ELIMU NCHINI

March 15, 2025 Add Comment

 


Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imeendelea kutekeleza programu mbalimbali zinazolenga kufungamanisha sekta ya mafuta na gesi asilia na sekta ya elimu nchini.

Miongoni mwa programu hizo ni pamoja na kutoa fursa kwa wadau wa sekta ya elimu kutembelea miundombinu ya uzalishaji na uchakataji wa gesi asilia iliyopo katika mikoa inayozalisha gesi asilia nchini kwa lengo la kuongeza uelewa wa wadau hao muhimu.

Katika hili, tarehe 14 Machi 2025, PURA iliwezesha ziara ya wadau kutoka vyuo vya elimu ya juu, vyuo vya elimu ya kati na vyuo vya ufundi nchini kutembelea mitambo ya kuzalisha na kuchakata gesi asilia iliyopo Mkoani Mtwara.

Ziara hiyo pia ilihusisha wadau kutoka mamlaka zinazohusika na udhibiti wa ubora wa elimu ikiwemo Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET)

Kupitia ziara hiyo, wadau hao walipata fursa ya kutembelea mitambo ya kuzalisha na kuchakata gesi asilia iliyopo Mnazi Bay inayoendeshwa na kampuni ya Maurel et Prom na mitambo ya kuchakata gesi asilia iliyopo eneo la Madimba inayoendeshwa na GASCO ambayo ni kampuni tanzu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

Pamoja na maeneo hayo, wadau hao walipata fursa ya kutembelea Chuo cha Ualimu Mtwara (Kawaida) kwa lengo la kuona namna ambavyo matumizi ya gesi asilia yameleta mapinduzi katika chuo hicho baada ya kuacha matumizi ya kuni kama chanzo cha nishati wakati wa kupika na kuhamia katika matumizi ya gesi asilia.

Wakizungumza wakati wa ziara hiyo, wawakilishi wa wadau hao akiwemo Dkt. Malehe Cosmas Setta ambaye ni Mthibiti Ubora Mkuu kutoka TCU, Bw. John Ndega ambaye ni Meneja anayehusika na utafiti ndani ya VETA na Dkt. Adela Syikilili ambaye ni mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wamesema ziara hiyo, pamoja na kuongeza uelewa, imewasaidia kupata picha halisi ya kiwango cha utaalamu kinachohitajika katika tasnia ya mafuta na gesi asilia jambo ambalo litaongeza tija wakati wa maandalizi ya mitaala inayohusiana na masuala ya mafuta na gesi.

Kwa upande wake, mwakilishi kutoka PURA Bw. Musa Ryoba alisema kuwa ziara hiyo ni mwendelezo wa jitihada za PURA katika kuhakikisha kuwa sekta ya mafuta na gesi asilia nchini inafungamanishwa na sekta nyingine za kiuchumi ikiwemo elimu kwa kuwa ili sekta ya mafuta na gesi iwe na mchango mkubwa katika uchumi ni lazima sekta hiyo ifungamanishwe na sekta zingine hususan sekta za kimkakati.
Mhandisi Haruna Mchessu kutoka kampuni ya Maurel et Prom akielezea jambo kwa wadau wa elimu wakati ziara iliyoandaliwa na PURA kwa lengo la kuongeza uelewa wa wadau hao kuhusiana na masuala ya uzalishaji na uchakataji wa gesi asilia katika eneo la Mnazi Bay Mkoani Mtwara.
Wadau wa masuala ya elimu katika picha ya pamoja na wataalamu kutoka PURA na  Maurel et Prom wakati ziara iliyoandaliwa na PURA kwa lengo la kuongeza uelewa wa wadau hao kuhusiana na masuala ya uzalishaji na uchakataji wa gesi asilia Mkoani Mtwara.
Mhandisi Haruna Mchessu kutoka kampuni ya Maurel et Prom akielezea jambo kwa sehemu ya wadau wa elimu wakati ziara iliyoandaliwa na PURA kwa lengo la kuongeza uelewa wa wadau hao kuhusiana na masuala ya uzalishaji na uchakataji wa gesi asilia katika eneo la Mnazi Bay Mkoani Mtwara.

KAMATI YA BUNGE UJENZI WA BARABARA YA TANGA-PANGANI BAGAMOYO UENDELEE KUPITIA ENEO LA HIFADHI YA TAIFA YA SAADANI

March 14, 2025 Add Comment


Na Oscar Assenga, PANGANI

KAMATI ya Kudumu ya Bunge Miundombinu imeshauri Serikali ujenzi wa barabara ya kutoka Tanga-Pangani –Bagamoyo upitie katika eneo la Hifadhi ya Taifa ya Saadani ili kufungua mkoa huo kiuchumi na kuongeza idadi kubwa ya watalii.

Ushauri huo wa Kamati ulitolewa leo na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Moshi Kakoso mara baada ya kamati hiyo kutembelea ujenzi wa barabara ya Tanga-Pangani pamoja na kukagua ujenzi wa Daraja la Mto Pangani

Alisema kwa sababu Serikali haijengi barabara kuwafurahisha wananchi bali kuufungua uchumi wa nchi sasa kama wanapeleka barabara na kuichepusha kwenye eneo ambalo lingekuwa na tija zaidi wanaomba hilo walifanyie upembuzi yakinifu huko serikali na wapate majibu ya msingi yenye ufanisi kwenye miradi ambayo ni ya kimkakati.

“Kujenga barabara hiyo wangeiacha na Serikali iliamua kujenga barabara upande wa ufukweni pembezoni mwa bahari ili ilete maendeleo kwa wananchi wa maeneo hayo sasa hawakatai kile kipande ambacho kimepita huko hivyo nendeni mkakae kile kipande ambacho kitakuwa kimebaki cha kukatisha pale nendeni mkakae mkiingize kwenye mfumo ambao mtaujua nyie”Alisema

Mwenyekiti hiyo alisema kwamba wakakae Wizara na Ofisi ya Makamu ya Rais ili kuangalia uwezekano wa barabara hiyo iweze kuifungua iende eneo la Hifadhi ya Taifa ya Saadan na kuweza kuufungua ushoroba wa utalii pamoja na kuifungua kiuchumi mkoa wa Tanga na Taifa kwa ujumla.

“Mhe Naibu Waziri tunawapongeza kwa ujenzi unaoendelea wa daraja ni mzuri na maendeleo ya mradi wa daraja bunge limeridhishwa na litakapokamilika litaleta sura nzuri kwenye maeneo ya wilaya ya Pangani na mkoa na litakuwa kivutio na daraja pekee ambalo litakuwa juu sana na wanaona serikali uwekezaji wake utakuwa na tija zaidi”Alisema Mwenyekiti huyo wa kamati.

Hata hivyo akizungumza wakati akihitimisha ziara ya kamati hiyo aliishauri Serikali kuhakikisha inakamilisha haraka barabara ya Tanga-Pangani ili kuepusha serikali kutokuingia gharama nyengine za kulipa fidia.

Alisema kwamba uwekezaji unaowekezwa katika Daraja la Mto Pangani hautakuwa na maana iwapo barabara unganishi haitakuwepo huku akitaka lifanyiwe kazi kuhakikisha wanakamilisha ujenzi huo ili uende sambamba na daraja.

Hata hivyo aliiomba Serikali iwasimamie wakandarasi waweze kukamilisha ujenzi wa barabara kwa mujibu wa mkataba ambao mlishakubaliana nao wabunge wamehoji kuna wasiwasi kwamba ile miezi minne kwamba wanaweza kukamilisha kipande cha barabara na wasipowasimamia wataongeza muda mwengine wa ziada.

“Simamieni kile kipande kikamilike kije kuunga kwenye eneo la Barabara narudi kusema Bunge lingependa barabara ya Kutoka Tanga ingeenda kupitia eneo la Hifadhi ya Saadani wangekuwa wameufungua mkoa kiuchumi na kuongeza idadi ya watalii”Alisema

Awali akizungumza Naibu Katibu Mkuu wizara ya Ujenzi Msonde wataendelea kufuatilia kuona wapi inakwama na nni kifanyike

Msimamizi wa Barabara ya Tanga-Pangani kutoka Wakala wa Barabarani nchini (Tanroad) Mkoa wa Tanga Mhandisi Godson Yohana alisema daraja la Mto Pangani lina urefu wa mita 525 ambapo kwa miradi ya madaraja nchini hilo ni daraja la pili kwa ukubwa na la kwanza ni Kigongo Busisi Mwanza.

Alisema ujenzi wa mradi huo ulianza Desemba 7 mwaka 2022 na gharama za mradi Bilioni 82.2 na unatekelezwa na Kampuni ya Shandon Likway Group ya kutokea nchini china na ujenzi huo umefikia asilimia 55 na unahusisha barabara na ujenzi wa daraja.

Mhandisi huyo alisema kwamba nguzo zote za kushika daraja zimekwisha kamilika na wanaendelea na ujenzi na mkandarasi yupo eneo la mradi huku akieleza ujenzi wa barabara loti ya kwanza umefikia asilimia 75 na mkandarasi mpaka sasa amekamiisha kipande cha kiliomita 15.8.

Alisema changaoto kubwa iliyowachelewesha kwenye mradi huo ni upatikanaji wa jiwe lenye sifa ya kutumika kwa lami ambayo wanaiweka hapo kutokana na uwepo wa teknolojia mpya kwamba mawe yanayotumika kusagia kokoto yanatakiwa kuwa na nguvu na viwango vya juu.

“Jiwe hilo tumelipata Muheza kilimota 60 kutoka eneo la mradi na walikuwa na leseni za watu wanaoyamiliki ilikuwa na changamoto kidogo lakini yamekamilila mradi huo unatarajiwa kukamilika 16June 2025”Alisema

Hata hivyo alisema kilomita zilizobaki ni 34 ambapo wanaishukuru Serikali tayari imemlipa mkandarasi huyo tokea Desemba mwaka jana kiasi cha Bilioni 4.7 na mwezi wa pili mwaka huu walilipaswa Bilioni 10.8.

Alisema mwanzoni walikuwa na changamoto mbalimbali kusimama kwa mradi na wamempa wiki mbili arudi kazi na kwa sasa wanaendele kuweka vifaa ili kuendelea na ujenzi huo

Mwisho.

KAMATI YA BUNGE YAIPONGEZA SERIKALI KWA MABORESHO MAKUBWA YA MIUNDOMBINU BANDARI YA TANGA

March 13, 2025 Add Comment


Na Oscar Assenga,TANGA

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeipongeza Serikali kwa maboresho makubwa ya miundombinu katika Bandari ya Tanga ambayo yamekuwa chachu ya kuongeza ufanisi katika utendaji wake.

Kauli ya Kamati hiyo ilitolewa leo na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Selemani Moshi Kakoso baada ya kumaliza ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maboresho na miundombinu ya sekta ya Uchukuzi katika Mkoa wa Tanga.

Alisema kwamba kamati hiyo imeridhishwa na utendaji kazi wa mamlaka hiyo hasa baada ya maboresho ya miundombinu iliyofanywa na Serikali na hivyo kuiongezea ufanisi wa kazi pamoja na ukusanyaji wa mapato.

“Kwa kweli sisi kama Kamati tumeridhishwa na utendaji kazi wa mamlaka ya Bandari na nieleze kwamba tutaendelea kuisadia TPA kutimiza maono ya Rais na kufikia malengo yao na Serikali kwa ujumla”Alisema

Awali akizungumza Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile aliishukuru kamati kwa ziara yao iliyowawezesha kujionea kazi kubwa inayofanywa na Serikali katika katika kuboresha sekta hiyo.

“Niwahakikishie kamati kwamba maoni, ushauri na maelekezo mliyoyatoa yatafanyiwa kazi kuhakikisha mkoa wa Tanga unafunguka kiuchumi kutokana na maboresho yanayoendelea kufanywa na Wizara ya Uchukuzi”Alisema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) Plasduce Mbosa alisema kukamilika awamu ya mbili za maboresho ya maboresho ya Bandari ya Tanga kwa gharama ya shilingi Bilioni 429.1 kumekuwa chachu ya maendeleo na kufungua ushoroba wa kanda ya kaskazini.

“Niishukuru kamati ya kudumu ya Bunge Miundombinu kwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa TPA ili mamlaka hiyo iweze kutekeleza mipango yake ya maboresho ya Bandari na kuwa chachu ya maendeleo ya uchumi wa Taifa “Alisema