Showing posts with label elimu. Show all posts
Showing posts with label elimu. Show all posts

PANGANI KUJA NA MKAKATI WA UFUMBUZI WA KUONGEZA KIWANGO CHA UFAULU WA WANAFUNZI

September 04, 2023 Add Comment

Mkazi wa Kijiji cha Kwakibuyu Ramadhan Mohammed akiwasilisha mada katika mafunzo ya kuwajengea ujuzi wa uhamasishaji jamii katika utetezi wa utatuzi wa changamoto za kielimu kwenye vijiji vya Mkaramo,Ubangaa,Mkwajuni,Kwakibuyu,Kipumbwi na Stahabu.mafunzo hayo yaliendeshwa na asasi ya Tree of Hope chini ya ufadhili wa Foundation for Civil Society (FCS)



Pangani Kujenga maelewano baina ya wazazi,wananchi,walimu ,viongozi na wanafunzi  imeelezwa kuwa ndiyo ufumbuzi wa kuongeza kiwango cha ufaulu wa  mitihani ya kitaifa kwa wanafunzi Wilayani Pangani.

Wajumbe wa kamati ya kuhamasisha uwajibikaji jamii na mamlaka zinazohusika kuboresha elimu katika vijiji vya Kipumbwi, Mkalamo,Ubangaa na Stahabu walisema hayo walipokuwa wakizungumza

Wajumbe hao ambao walikuwa wakizungumza baada ya  mafunzo elekezi ya utekelezaji wa mradi wa kujamasisha jamii na mamlaka zinazohusika kuboresha elimu katika jamii unaosimamiwa na asasi isiyo ya kiserikali  ya Tree Of Hope chini ya ufadhili wa Shirika la Foundation For Civil Society (FCS) walisema wanakwenda kutumia kila mbinu sahihi kuhakikisha maelewano yanajengeka kwa sababu wamebaini ndiyo kiini cha mafanikio.


Ali Ibrahim wa Kijiji cha Kwakibuyu ambacho wanafunzi wake wanasoma shule ya msingi Kipumbwi Wilayani hapa alisema badala ya kutupiana lawama ufaulu utapatikana kwa Kujenga maelewano na kuwa kitu kimoja katika kutekeleza majukumu.


"Ipo changamoto ya utoro,uhaba wa walimu na baadhi ya shule kukosa maji..kila changamoto ina njia zake wazazi wakichangia vyema vyakula wanafunzi watavutika na hawatatoroka,lakini uhaba wa walimu wazazi wakichangia kuwalipa posho walimu wastaafu ufaulu utaongezeka" alisema Ali.


Mratibu wa mradi huo kutoka Tree of Hope,Goodluck Malilo alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwapa mbinu wajumbe wa kamati hizo za utatizi wa changamoto za kielimu kwenye maeneo ya vijiji hivyo ili kuboresha elimu na kuinua kiwango cha ufaulu.


"Changamoto za kielimu katika vijiji vingi zunajulikana na kila mwananchi,

 mamlaka na walimu na uwepo wake siyo kwa sababu wenye mamlaka wameshindwa kuzitatua bali zimekosa utetezi na hili ndilo jukumu la wanakamati" alisema Malilo.


Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Zainab Abdallah  alisema kamati hizo zinasaidia kuwezesha kila mmoja kuona uchungu na maendeleo ya elimu na kutimiza wajibu wake.


 

WANAFUNZI WAHIMIZWA KUPENDA MASOMO YA SAYANSI

August 15, 2023 Add Comment

 

Mkurugenzi wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Maulilio Kipanyula akikabidhi majarida ya OYLA Africa kwa wawakilishi wa wanafunzi wa shule zilizopokea msaada wa majarida hayo kutoka kampuni ya Baobab Shalom Limited katika hafla fupi iliyofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Msalato Jijini Dodoma tarehe 14 Agosti 2023.
…..

Mkurugenzi wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Maulilio Kipanyula amewahimiza wanafunzi wa kitanzania kupenda masomo ya sayansi na teknolojia kutokana na mchango wake katika kuleta maendeleo ya nchi.

Prof. Kipanyula amesema Sayansi na Teknolojia imeleta mapinduzi makubwa kitaifa na kimataifa na hasa katika sekta za elimu, habari, biashara na huduma mbali mbali za kijamii.

Ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya sita imeweka kipaumbele katika sekta ya elimu ambapo imewekeza kwa kiwango kikubwa ikiwa ni pamoja na kutoa vifaa vya kujifunzia na kufundishia hivyo kuwahamasisha wanafunzi kujifunza kwa bidii na kuwa wabunifu.

Alikuwa akizungumza katika hafla fupi ya kugawa majarida 700 yanayofahamika kama OYLA Africa ambayo yametolewa na kampuni ya Baobab Shalom Limited ya jijini Dar es Salaam kufuatia Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) yaliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TEA Bi. Bahati Geuzye na Mkurugenzi wa Baobab Shalom Limited Bw. Yev Semikov katika ofisi za TEA jjijini Dodoma tarehe 14 Agosti 2023.

Bw. Semikov amesema lengo la Majarida hayo ni kuwezesha wanafunzi wanaoyatumia kuwa wabunifu na wadadisi kwa lengo la kuboresha mazingira na maisha yao kwa ujumla.

Mkurugenzi Mkuu wa TEA Bi. Bahati Geuzye ameshukuru kampuni ya Baobab Shalom Limited kwa kutoa msaada huo wa majarida kupitia Mfuko wa Elimu unaosimamiwa na TEA na kuongeza kuwa TEA iko tayari wakati wote kushirikiana na wadau wa elimu na kuwahakikishia kuwa misaada ya elimu inayopita kwenye Mfuko wa Elimu wa Taifa inasimamiwa kikamilifu na kutumika kama ilivyokusudiwa.


Mkurugenzi wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Maulilio Kipanyula akikabidhi majarida ya OYLA Africa kwa wawakilishi wa wanafunzi wa shule zilizopokea msaada wa majarida hayo kutoka kampuni ya Baobab Shalom Limited katika hafla fupi iliyofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Msalato Jijini Dodoma tarehe 14 Agosti 2023.

Mkurugenzi Mkuu wa TEA Bi. Bahati Geuzye (wa pili kulia) na Mkurugenzi wa Baobab Shalom Limited Bw. Yev Semikov (wa pili kushoto) wakisaini Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) kwa ajili ya kugawa majarida 700 ya OYLA Africa yanayohimiza wanafunzi kusoma masomo ya Sayansi, Teknolojia na Hisabati katika hafla fupi iliyofanyika jjijini Dodoma tarehe 14 Agosti 2023.
Mkurugenzi Mkuu wa TEA Bi. Bahati Geuzye (wa pili kulia) na Mkurugenzi wa Baobab Shalom Limited Bw. Yev Semikov (wa pili kushoto mstari wa mbele) baada ya kusaini Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) kwa ajili ya kugawa majarida 700 yanayohimiza wanafunzi kusoma masomo ya Sayansi, Teknolojia na Hisabati katika hafla fupi iliyofanyika jjijini Dodoma tarehe 14 Agosti 2023.


Mkurugenzi wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Maulilio Kipanyula ( wa pili kulia mstari wa mbele) akipokea jarida la OYLA Africa kutoka kwa Mkurugenzi wa Baobab Shalom Limited Bw. Yev Semikov (wa pili kushoto). Majarida hayo yanalenga kuhimiza wanafunzi kusoma masomo ya Sayansi, Teknolojia na Hisabati.


Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Msalato ya jijini Dodoma walioshiriki hafla ya kupokea Majarida ya OYLA Africa kwa ajili ya kuhimiza wanafunzi kupenda masomo ya Sayansi, Teknolojia na Hisabati yaliyotolewa na Kampuni ya Baobab Shalom Limited ya jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wanafunzi katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi wakiwa wameshika magazeti ya OYLA Africa yaliyotolewa Kampuni ya Baobab Shalom Limited ya jijini Dar es Salaam.

CCM TANGA YASITISHA UJENZI WA SHULE SHIKIZI KUTOKANA NA KUJENGWA KATIKA CHANZO CHA MAJI

August 14, 2023 Add Comment









CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Tanga, kimesitisha ujezi wa shule shikizi inayojengwa katika  kijiji cha Mahezangulu, katika halmashauri ya Bumbuli, kutokana na shule hiyo kujengwa katika chanzo cha maji.


Akitoa maelekezo ya kusitishwa kwa ujenzi wa madarasa mawili ya shule hiyo inayojengwa katika kitongojo cha Kweusolo, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Rajab Abdallah alisema wananchi lazima waheshimu vyanzo vya maji na utunzaji wa mazingira.


Awali Mwenyekiti wa kijiji cha Mahezangulu, Seif Sekidele alisema kutokana na uhitaji wa shule shikizi kwa watoto wa kitongoji hicho walionelea wajenge shule katika eneo hilo licha ya kuwa ni eneo la chanzo cha maji kutokana na uhitaji mkubwa wa shule.


"Mheshimiwa Mwenyekiti kijiji chetu kina shule mbili za msingi lakini ukiingia shule ya Mahezangulu darasa lenye watoto 50 basi 32 wanatoka katika kitongoji hicho," alisema Mwenyekiti huyo wa kijiji.


Meneja wa Wakala wa maji na usafi wa mazingira Vijijini (RUWASA) wilayani Lushoto Erwin Sizinga, alisema serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 243 kwa ajili ya mradi wa maji wa kijiji hicho na eneo lililojengwa shule ni la chanzo cha maji cha mradi huo.

"Wenzetu wa bonde la mto Pangani walitwambia chanzo cha maji katika kijiji hiki kina maji ya kutosha isipokuwa wananchi wasilime katika chanzo hiki ili chanzo kiwe cha uhakika na endelevu," alisema Sezinga.

Mbunge wa jimbo la Bumbuli na Waziri wa Nishati, January Makamba, alisema alikataa kuwasaidia kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi huo na kumweleza Mwenyekiti wa kijiji hicho kama mbunge yupo tayari kutoa fedha ili wapate eneo jingine kwa ajili ya kujenga shule nyingine badala ya hiyo.


Diwani wa kata ya Mahezangulu Rashid Abdallah 'Chid boy' alitaka serikali ikubali shule hiyo iendelee kujengwa katika eneo hilo na wataalamu watafute chanzo kingine cha maji ili watoto wa kitongoji hicho wapunguziwe umbali wa kwenda katika shule ya msingi Mahezangulu. 


Diwani alikubali kauli ya Mwenyekiti wa kijiji hicho cha Mahezangulu kwamba hakuna eneo jingine litakaloweza kujengwa shule zaidi ya eneo hilo ambalo ni la serikali ambalo zamani lilikuwa linepandwa miti na sasa ipo miti miwili tu na wananchi wanalima mahindi.

"Natoa maelekezo hapa pasiendelezwe paachwe, kuleta fedha kuindeleza shule hii ni kuendelea kuharibu chanzo cha maji bora tupate lawama kutoka kwa wananchi lakini tukilende hiki chanzo cha maji," alisema Mwenyekiti wa CCM mkoa.

Alimwagiza mkuu wa wilaya ya Lushoto Kalist Lazaro kuhakikisha wananchi hawalimi katika eneo hilo ili kuziokoa fedha za serikali zilizoletwa kwa ajili ya mradi wa maji, zisipotee bure.

Alisema CCM katika ilani yake ilisema kwamba hadi mwaka 2025 wananchi katika maeneo ya Vijiji watapata maji kwa asilimia 85 hivyo kuruhusu ujenzi huo kutasababisha ahadi hiyo isikamilike kwasababu ya watu kushindwa kutunza mazingira.

Mwenyekiti wa CCM mkoa ameendelea ziara zake za kutembelea wilaya za mkoa wa Tanga kuona uhai wa chama na utekelezaji wa ilani ya chama ya mwaka 2020-2025.

Mwisho

MHE HEMED ABDULLA ASEMA JUHUDI ZINAZOCHUKULIWA NA VIONGOZI WA MKOA KUSINI UNGUJA ZACHANGIA KUKUA KWA UFAULU

August 13, 2023 Add Comment

 Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amesema kukuwa kwa ufaulu Mkoa wa Kusini unguja kumetokana na juhudi zinazochukuliwa na Viongozi wa Mkoa huo kwa kuzingatia maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025.


Mhe. Hemed ameyasema hayo wakati akiwasalimia wanachama wa Chama Cha Mapinduzi Jimbo la Paje na Jimbo la Makunduchi katika muendelezo wa ziara yake ya kukagua uhai wa Chama Mkoa wa Kusini Unguja.


Amesema kwa mwaka wa masomo 2022 Mkoa wa kusini Unguja umeongoza kwa ufaulu kutokana na juhudi za Makusudi zilizochukuliwa na Jumuiya ya Mwanamke Initiative Foundation (MIF) kwa kushirikiana na Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM).

Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imechukua jitihada za kuanzia masomo ya Kidato cha Tano na kidato cha Sita Skuli ya Hasnuu Makame ili kupunguza masafa kwa wanafunzi kufuata elimu hiyo.


Aidha Mhe. Hemed amempongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuelekeza zaidi ya Bilioni 230 fedha za Mkopo wa Uviko 19 ambazo zimeelekezwa kwenye miradi mingi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa Hospital za Wilaya na Mkoa, Skuli za Ghorofa pamoja na madarasa.


Aidha amewakumbusha wananchi na wanachama wa CCM kuendelea kudumisha Amani na Utulivu iliopo na kuwataka kuwa na umoja na mshikamano baina yao.


Nae Katibu wa Siasa na uhusiano wa Kimataifa Khadija Ali Salum amesema Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Unguja wana kila sababu ya kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kuelekeza miradi mingi ya Maendeleo Mkoani humo pamoja na kuwapongeza Wabunge, Wawakilishi na Madiwani kwa kuwatumikia wananchi wao.


Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Rashid Hadid ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Nane inayoongozwa na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi imeelekeza miradi mingi ya maendeleo Mkoa wa Kusini Unguja na tayari Serikali imeahidi kujenga Tenki kubwa la maji mkoani humo ambalo litamaliza changamoto ya upatikanaji wa huduma ya Maji safi na Salama Mkoani humo.


Katika ziara hiyo Mhe. Hemed ameweka Jiwe la Msingi ujenzi wa Ofisi ya Jumuiya ya Maendeleo na urekebishaji wa maadili Bwejuu (JUMAMABWE) ambapo ameipongeza Jumuiya hiyo kwa juhudi zake za kusaidia kurekebisha tabia katika jamii hiyo.


Aidha ameeleza kuwa eneo hilo limezungukwa na mahoteli ya Kitalii na kuwataka wana Jumuiya hiyo kuhakikisha wanatoa elimu ya kuzingatia Maadili, silka na tamaduni kwa wenyeji na wageni wanaofika maeneo hayo.


Akisoma taarifa ya ujenzi huo Katibu wa Jumuiya ya Maendeleo na urekebishaji wa maadili Bwejuu Bwana Hassan Simai Issa ameeleza kuwa Jumuiya hiyo imeanzishwa mwaka 2018 na kupatiwa usajili mwaka 2019 ambapo ujenzi huo unaendeshwa kwa nguvu za wananchi na wadau mbali mbali wa Maendeleo waliozunguka kijiji hicho.


Amefafanua kuwa kuwepo kwa Jumuiya hiyo kutazalisha fursa mbali mbali kwa vijana, kuweka jamii katika Mila, Silka na Tamaduni, pamoja na kuinua uchumi wa Zanzibar.


Katika ziara hiyo Mhe. Hemed ameshiriki Ujenzi wa Ofisi ya CCM Jimbo la Paje, ameweka Mawe la Msingi Tawi la CCM Bwejuu Kusini, Ujenzi wa Ofisi ya Jumuiya ya maendeleo na urekebishaji wa maadili Bwejuu, Tawi la CCM Sheba, na nyumba ya maendeleo Shehia ya Kajengwa.




WAZIRI MKENDA AKUTANA NA MKURUGENZI MKAZI WA BENKI YA DUNIA NCHINI

July 18, 2023 Add Comment






 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda leo Julai 17, 2023 jijini Dar es Salaam amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Bw. Nathan Belete na ujumbe wake.


Kikao hicho kilikuwa na lengo la kujadili mpango pendekezwa wa utekelezaji wa mageuzi ya Elimu na ushirikiano na Benki ya Dunia katika
utekelezaji huo.


Aidha wamekubaliana kuboresha miradi ya BOOST na SEQUIP ili iweze kukidhi kuwezesha mahitaji ya utoaji elimu ujuzi pamoja na kujadili maendeleo ya Miradi mingine katika ngazi ya elimu ya ufundi.