Showing posts with label afya. Show all posts
Showing posts with label afya. Show all posts

PEPFAR YAUPONGEZA MKOA WA TANGA KWA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA UTOAJI WA HUDUMA ZA VVU

August 30, 2024 Add Comment

 




Na Oscar Assenga, KOROGWE


JUMLA ya vijana 134 wenye umri kati ya miaka 15 hadi 25 wamejiandikisha kwenye kliniki ya tiba na matunzo ya VVU katika Hospitali ya Mji wa Korogwe huku asilimia 90 ya vijana hao wakifanikiwa kufubaza makali ya VVU.

Hayo yalibainishwa wakati wa ziara ya waandishi wa habari mkoani Tanga walipotembelea hospitali ya wilaya ya Korogwe (Magunga)na Kituo cha Afya cha St.Raphael  vinayowezeshwa na Shirika la THPS kupitia Mradi wa Afya Hatua unaofadhiliwa na Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa kupambana na UKIMWI (PERFAR), kupitia Kituo cha Kudhibiti  na Kuzuia Magonja cha Marekani (U.S. CDC).

Kwa mujibu wa Kaimu Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI (RACC) mkoani Tanga, Bi. Judith Kazimoto, THPS kupitia mradi wa Afya Hatua, kwakushirikiana na timu za usimamizi wa Afya za Mkoa na Wilaya, wanatekeleza afua mbalimbali za kupambana na VVU, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa huduma rafiki kwa vijana katika vituo 67 vya afya vilivyopo mkoani humo, ikiwemo Hospitali ya Mji wa Korogwe.

Ili kuhakikisha huduma bora za kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, kina mama wajawazito wanaoishi na VVU hupatiwa huduma zote muhimu, na mara baada ya kujifungua, Watoto wao husajiliwa na kuchukuliwa vipimo vya VVU mapema.

Kupitia mradi wa Afya Hatua, watoa huduma katika kituo cha Afya cha St. Raphael huhakikisha usajili wa Watoto hao unafanyika na wanachukuliwa sampuli za damu ili kufanyiwa kipimo cha VVU ndani ya wiki sita baada ya kuzaliwa kwao na kuhakikisha wanapatiwa huduma stahiki.

“Kwa kipindi cha kuanzia Oktoba 2023 hadi Julai 2024, jumla ya wapokea huduma za VVU wajawazito 26 walijifungua katika kituo hicho. Watoto waliozaliwa na kina mama hawa walisajiliwa ndani ya siku saba baada ya kujifungua. Kati ya hao, 24 (93%) walichukuliwa vipimo na wote (100%) na matokeo yalionesha wote walizaliwa bila maambukizi ya VVU”, alisema Bi. Kazimoto.

Katika kipindi cha miaka 21 iliyopita, serikali ya Marekani kupitia Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na UKIMWI (PEPFAR) imewekeza zaidi ya dola bilioni 7 nchini Tanzania kwa ajili kukabiliana na janga la VVU. 

Kwa mujibu wa Mratibu wa PEPFAR nchini Tanzania, Bi. Jessica Greene, PEPFAR ilipoanza kazi hapa Tanzania, mwaka 2003, kulikuwa na watu wasiozidi 1,000 tu ambao waliokuwa kwenye matibabu ya VVU.  

“Hivi sasa, PEPFAR inasaidia zaidi ya watu milioni 1.5 waliopo kwenye huduma ya tiba na matunzo.  Vifo vinavyotokana na UKIMWI nchini vimepungua kwa 76% na maambukizi mapya yamepungua kwa 58%, tangu 2003”, alisema Bi. Greene.

Bi. Greene alisema ingawa lengo la kutokomeza VVU/UKIMWI ifikapo mwaka 2030 ni kubwa lakini linaweza kufikiwa. 

“Serikali ya Marekani inajivunia kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika jitihada za kufikia malengo ya UNAIDS 95-95-95 ifikapo mwaka 2025, ambayo yanalenga 95% ya watu wanaoishi na VVU kufahamu hali zao, 95% ya waliogundulika kuwa na VVU wapate matibabu, na 95% ya wale walio kwenye matibabu waweze kufubaza VVU”, alisema. 

 Utafiti wa hivi karibuni wa Athari za VVU Tanzania 2022-2023 (Tanzania HIV Impact Survey 2022-2023) umeonesha kuwa jitihada za kupambana na VVU mkoani Tanga zimefanikisha kufikia viwango vya juu vya kufubaza VVU kwa 93.5%. 

“Tunaupongeza mkoa ya Tanga kwa hatua hii nzuri na tunaamini wataendelea kudumisha mafanikio hayo tunapoelekea kuyafikia malengo ya UNAIDS 95-95-95”, alisema Bi. Greene







TOENI ELIMU ZAIDI KWA WANANCHI JUU YA UGONJWA WA MPOX;WAZIRI MHAGAMA

TOENI ELIMU ZAIDI KWA WANANCHI JUU YA UGONJWA WA MPOX;WAZIRI MHAGAMA

August 21, 2024 Add Comment

 Na WAF, Namanga- Arusha

Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama amewataka wataalamu wa Afya nchini kuongeza kasi ya kutoa elimu ya ugonjwa wa Mpox ili wananchi wawe na uelewa mpana dhidi ya ugonjwa huo.

Waziri Mhagama ametoa agizo hilo leo Agosti 21, 2024 wakati wa ziara kwenye Kituo cha Forodha cha Mpaka wa Namanga Halmashauri ya Wilaya ya Longido mkoani Arusha alipofika kuona utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Mpox.

“ Nimezungumza na mmoja wa wasafiri lakini hajui dalili za za ugonjwa wa Mpox hivyo ipo haja ya kuongeza kasi ya utoaji elimu kwa wananchi ili kuwa na uelewa juu ya ugonjwa huo”, ameeleza Mhe. Mhagama na kuongeza

“Kuwe na mabango na vipeperushi vinavyotoa elimu juu ya ugonjwa kuelezea Dalili, unaambukizwaje na namna ya kujikinga ili kila msafiri anayeingia na kutoka nchini awe na uelewa mpana” amesisitiza Waziri Mhagama.

Mhe. Mhagama amesema kwa sasa mpaka Tanzania ni Salama na hakuna mgonjwa yeyote aliyebainika kuwa na ugonjwa huo hivyo wananchi waendelee kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa wa Mpox .

“ Natoa wito kwa wananchi kila mmoja awe mlinzi kwa mwenzake pale atakapo ona dalili za ugonjwa huo kwa mtu basi atoe taarfa kwa wataalamu wa afya, Kituo cha kutolea huduma za afya kilichopo karibu yake au kuwasiliana na Wizara ya Afya kwa Namba ya 199 ili kuhakikisha nchi inakuwa salama”, ametoa wito.

Akihitisha ziara yake Waziri Mhagama amewahakikishia watanzania kuwa Wizara yake imejipanga kikamilifu kwa kuimarisha Huduma za uchunguzi na maabara maeneop ya mipakani ili kuhakikisha ugonjwa huo hauingii nchini    

PROFESA ASSAD ATAKA USHIRIKIANO UJENZI WA HOSPITALI YA KIISLAMU TANGA

August 04, 2024 Add Comment

 










Na Oscar Assenga, TANGA

MDHIBITI  na Mkaguzi  Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mstaafu Profesa Mussa Assad amesema ni umuhimu kuwepo kwa ushirikiano wa pamoja ili kuhakikisha ujenzi wa Hospitali ya Kiislamu Mkoani Tanga unakamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma.

Profesa Assad aliyasema hayo mwishoni mwa wiki Jijini Tanga wakati aliposhiriki kwenye Kongamano la tathimini ujenzi wa Hospitali ya Kiislamu Mkoa wa Tanga lililokwenda sambamba na kufanyika kwa harambee ya kuchangia ujenzi wake huku akieleza ni ushirikiano ni lazima wawe wamoja katika kufanikisha hilo.

Harambee hiyo ilikwenda sambamba na uliokwenda sambamba na kukagua eneo la Ujenzi wa Hospitali hiyo lililopo Kata ya Masiwani, Kupanda miti ya Matunda pamoja na kuweka jiwe la Msingi.

Alisema kwa sababu jambo ambalo linafanyika ni la kuokoa maisha na ukiokoa maisha ya mtu mmoja utakuwa umeokoa maisha ya watu wote kwani hata vitabu vitakatifu vya Mungu (Quran) vimeandikwa hilo.

“Hata vitabu vitakatifu vya Mwenyezi Mungu vinaeleza kumtibu mtu mmoja na kuyaokoa maisha yake ni sawa utakuwa umeuokoa umma nzima lakini tatizo ambalo analiona ni ajizi kwamba wanafikiria hawawezi leo kufanya jambo hilo labda wasubiri kesho itawezakena na mwisho miaka inapita anzeni sasa”Alisema.

“Hilo ni tatizo kubwa la ajizi hivyo tuondoe ajizi tulifanye kazi hi kwa ushirikiano mkubwa ili kuweza kutimiza malengo tuliojiwekea ya kuhakikisha ujenzi wa eneo hilo unaendelea “Alisema

“Leo nimefurahi kwa sababu kuna kazi kubwa imefanywa na amesikitika hatua zake zimekwenda taratibu mno na nimekuwa nikipita sana kwenye eneo hilo kila mwezi kwenda Tongoni na wala sijasikia kuwepo wa shughuli hizi pia kinachomsikitisha zaidi ni kumetolewa nondo 72 katika ujenzi huu”Alisema

Aidha alisema maana yake hawajali vitu vyao wenyewe hivyo ni wajibu wao kuhakikisha wakifanya vitu hapo vilindwa ili kuepusha kuibiwa na wezi jambo ambalo litapelekea kuepukana na vitendo hivyo.

“Lakini niwasihi katika jambo hilo tuwe pamoja na kuongeza mshikamano ili kulifanikisha jambo hilo na mwakani mungu akipenda kutakuwa wamepandisha jengo pia tutaendelea kuona namna wadau mbalimbali wanaweza kuchangia kwenye ujenzi huu”Alisema

Kwa makadirio ya Fedha za ujenzi wa Hosptali hiyo unakadiriwa kuwa ni zaidi ya Sh.Bilioni 2.4 sio fedha ndogo hivyo ni lazima waone namna ya wao wenyewe wajipange wafanya juhudi kubwa za kuanza kazi hiyo na wao waanze wenyewe na wao watakaoona hivyo wanaweza kuona namna ya wadau wengine kuwaunga mkono.

“Lakini niwaambie kwamba Mwenyezi Mungu akijalia nikirudi Dar nitahamasisha wenzangu kuona namna nzuri ya kuliendelea jengo hlo lianze haraka sana kutokana na umuhimu mkubwa lilikokuwa nalo”Alisema

Alisema kwamba Mwenyezi Mungu amewajalia neema nyingi waislamu hivyo ni vema wajiulize wameifanyia nini hiyo neema ya umri wamekaa miaka miwili jengo hilo hivyo maana yake wamefanya ajizi na hawakufanya hima ya kutekeleza kazi hiyo.

“Jambo la muhimu ni kujikumbusha kwamba tumepewa neema ya umri siku zinavyokwenda tujipime namna gani tumefanya kazi hizo inshallah Mwenyezi Mungu ajalie tukae pamoja juhudi hizi ziendelezwe ili mwakani tusiwe na msingi tuwe tumepanda kama sio ghorofa moja itakuwa ghorofa mbili na hilo tutaliweza kama tutakuwa wamoja”Alisema

Awali akizungumza kuhusu mradi huo wa Ujenzi wa Hospitali inayozingatia maadili ya Kiislamu Mjumbe wa Halmashauri Kuu wa Baraza la Waislamu Taifa (Bakwata) Sheikh Khamis Mataka alisema kwamba MwenyeziMungu atalipa nguvu jambo hilo ili litimie na uwezo huo wanao.

Alisema kwamba uwezo wa kulitimiza jambo hilo upo ndani yao wao wenyewe wakiondokana na matatizo na changamoto walizojiwekea wao wenyewe wataona namna suala hilo litakavyopata mafanikio.

Naye kwa upande wake Dkt Ally Fungo alisema kwamba mradi huo wa kimkakati umedhamiria kutatua tatizo la kimkakati kama halitatatuliwa litaadhidhiri dhamira ya jamii ya kiislamu kwa kwa maana hapo watakuwa na kituo cha afya cha kutoka tiba kinachzingtia maadili ya kiislamu ambayo ni ya kibinadamu.

Alisema kwamba hospitali hiyo haitakuwa ya waislamu pekee bali wote lakini haiwezekani wakina mama wakatibiwa na daktari mwanaume hiyo ni hospitali ya kimkakati kutatua kimkakati hospitali ya waislamu wenyewe kwa fedha zao wenyewe.

“Hospitali hii itakuwa na majengo sana kuanzia Jengo la Utawala ,Jengo la Madaktari,Wodi za Wakina Mama,Kina Baba ,Maabara,Mochwari ,na nyenginezo na gharama zake kwa awali tungetumia Bilioni 1.5 lakini kipindi kimepita miaka mitatu iliyopita”Alisema

Hata hivyo alisema kutokana na uchumi duniani kuadhirika hivyo sasa wamefanya ufuatiliaji vitu vimebadilika na bei ya vitu imeongezeka na hivyo watalazimika watumie bilioni 2.4 hilo sio jambo dogo ni kubwa hivyo watashirikiana na wadau wote kufanikisha hilo.

WANAOUGUA UGONJWA WA HOMA YA INI ASILIMIA KUBWA HAWAONI DALILI ZA MOJA KWA MOJA

July 28, 2024 Add Comment

Na Hadija Bagasha, Tanga.



WAKATI watanzania wakiadhimisha siku ya Homa ya Ini Duniani imeelezwa kwamba wagonjwa wanaougua ugonjwa huo asilimia kubwa hawaoni dalili za moja kwa moja isipokuwa asilimia ndogo.

Hayo yalibainishwa leo na Daktari wa Kituo cha Siha Polyclinic cha Jijini Tanga Kasanga Bashir Kasanga wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya siku hiyo ambapo wameazimisha kuwa kutoa vipimo bure kwa wananchi wa mkoa huo.

Alisema kwamba dalili za awali mara nyingi zinakuwa ni zile ambazo sio za moja kwa moja “Non Specific Symptoms” ambazo zinaweza kufananishwa na magonjwa mengine na kwa dalili ambazo ni viashiria vya moja kwa moja vya homa ya ini ni hali ya manjano kwenye sehemu za macho na mabadiliko ya ngozi mikono kubadilika rangi,rangi ya choo kubadilika ,maumivu ya tumbo na kukosa hamu ya kula.

Aidha alisema kwamba athari za homa ya ini iwapo kwamba matibabu yake hayajafanyika itapelekea ini kushindwa kufanya kazi yake ya kawaida na kupelekea vifo huku akiitaka jamii kuona umuhimu wa kupata chanjo ya homa hiyo ili kuweza kukabiliana nayo.

“Ndugu zangu leo wakati tunaadhimisha siku ya homa ya Ini Duniani ni vema kutoa wito kwa wananchi kuona umuhimu wa kujitokeza kupima na iwapo wakibainika kuwepo na ugonjwa huo waanza kuchukua hatua za kukabiliana nao”Alisema

“Kwa sababu mwamko wa wananchi kujitokeza kupima unasuasua lakini ukichukua takwimu kule tulipotoka na tunapoelekea kwa kweli mwamko umeshaanza kuwa ni mzuri kwa siku ya leo mwamko umekuwa ni mzuri na hatua zinazoonekana kulingana na mwamko wa watu ni nzuri na hiyo ni kuendelea kupongeza juhudu mbalimbali ambazo zinafanywa na Wizara ya Afya na Shirika la Afya Duniani (WHO)”Alisema

Akizungumzia umuhimu wa kuchanja homa ya ini alisema kuna umuhimu mkubwa kwa sababu ya takwimu zinaonyesha kwa magonjwa makubwa ya matatizo ya homa ya ini asilimia 45 mpaka 50 yanachangiwa na homa za ini

“Hivyo umuhimu wa kuchanja ni kuhakikisha jamii inabaki salama bila kuwa na magonjwa hayo homa ya ini hepatitis B,C kutokana na kwamba hatua za mwanzo haina dalili isipikuwa dalili zinajitokeza wakati ugonjwa umekuwa umefika mbali zaidi”Alisema

“Nitumie siku hii kuwahamasisha jamii ione umuhimu wa kuchanjo kwa maana iweze kujikinga na hapatatis B na C maana ni muhimu unapochanja hapatatis B uweze kujua na

Awali akizungumza Awadhi Abdul kutoka kwenye Kituo hicho alisema kwamba wao wameamua kuadhimisha siku hiyo kwa kufanyia watu vipimo vya homa aya ini na kutoa chanjo wao kama siha wanajitahidi kuhakikisha jamii inapata uelewa katika masuala ya kiafya lakini kutoa matibabu mbalimbali kwa jamii.

Aidha alisema kwamba ukiachia na homa ya ini wao wanatoa huduma mbalimbali za kimatibabu wana madaktari bingwa, huduma za maabara na huduma za mionzi mbalimbali, CTScan na MRI kwa gharama nafuu na zinazojali hali ya mtanzania.

“Tunashukuru kwa mwitikio ambao wameupata kwa jamii na lengo lao kubwa ni kuhakikisha wanapiga vita homa ya ini kwa wananchi kwa kutoa elimu “Alisema

Naye kwa upande wake Daktari Jovin Amani alisema homa ya ini inathari kwa ujumla na dalili zake ni kujisikia kuchoka na viungo,kupata manjano,kupoteza fahamu au kutapika damu hivyo wanawashauri watanzania waweze kujitokeza kupima ili kujua afya zao kwa ujumla maana homa ya ini i inaweza kuambukiza mtu yoyote inaweza kusambazwa kutoka mtu moja hadi mwengine.

ACHENI MATUMIZI HOLELA YA DAWA - WAZIRI UMMY

June 20, 2024 Add Comment

 


Na WAF - Arusha

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewataka Watanzania kuacha matumizi holela holela ya Dawa ili kuepuka usugu wa vimelea dhidi ya dawa hususani za antibaotik kushindwa kufanya kazi ipasavyo na kugharimu maisha na nguvu kazi ya Taifa.

Waziri Ummy amesema hayo leo Juni 19, 2024 Jijini Arusha wakati wa kilele cha maadhimisho ya Miaka 50 ya Jumuiya ya Afya ya nchi zacMashariki, Kati na Kusini mwa Afrika (ECSA-HC) ambapo mgeni Rasmi alikuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango.

"Usugu wa vimelea vya magonjwa Dhidi ya Dawa ni janga kubwa ambalo jamii ya Watanzania inapaswa kupambana nalo kwa dhati kwa kuwa madhara yake ni Mkubwa na yanagharimu fedha nyingi." Amesema Waziri Ummy

Amesema, ikiwa umeandikiwa dawa unywe kwa siku Tano basi maliza siku zote Tano, zingatia matumizi sahihi ya dawa hususani za antibaiotik na usitumie dawa bila ya kuandikiwa na daktari au mtaalam wa mifugo, unakuta dawa za mifugo anapewa binaadamu tuepuke kutengeneza janga kubwa ambalo litakwenda kugharimu Sekta ya Afya kwa siku za usoni kwa kuendelea na matumizi holela ya dawa." Amesema Waziri Ummy

Waziri Ummy ameongeza kuwa madhara ya matumizi holela ya dawa hupelekea mgonjwa kukaa hospitalini ama kuugua kwa muda mrefu bila kupona lakini pia mgonjwa kutumia gharama kubwa kwa ajili ya kujiuguza na hata kupoteza maisha kutokana na changamoto hiyo ya usugu wa vimelea dhidi ya Dawa

"kuongezeka kwa mzigo wa magonjwa Yasiyoambukiza katika ukanda huu, Jumuiya ya Afya ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika (ECSA-HC) imejipanga kuja na Tafiti zitakazo saidia kuja na ushahidi wa kisayansi utakao saidia mbinu sahihi za kupambana na magonjwa hayo na kuweka sera nzuri zitakazosaidia kufikia suala la Afya kwa wote.

Aidha, Waziri Ummy amesema katika miaka 50 ya Jumuiya ya Afya ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika (ECSA-HC) ku
na mengi makubwa ya kujivunia kwa kuwa Taasisi hiyo imekuwa ikitoa msaada wa kiufundi katika masuala ya afya na nchi za ukanda wa mashariki, kati na kusini mwa Afrika wataendelea kuongeza mashrikiano baina ya nchi wanachama ili kubuni na kuendeleza afua zaidi za Afya ambazo zitasaidia kukabiliana na changamoto zinazoikabili Sekta hiyo barani Afrika

”Jumuiya ya Afya ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika (ECSA-HC) wametusaidia sana sisi kama Tanzania katika kufanya tafiti za kisayansi kuhusu magonjwa ya kuambukiza lakini kubwa ni kuweza kutusaidia tukatengeneza mpango mkakati wa kupambana na magonjwa sugu pamoja na majanga kwa kujitathimini katika kupambana na magonjwa makubwa ya kuambukiza kama Ebola, Covid na homa ya bonde la ufa na kudhamini masomo kwa wataalamu wa Afya." Amesema Waziri Ummy.