Showing posts with label afya. Show all posts
Showing posts with label afya. Show all posts

DKT MAHERA : WATAKAOBAINIKA WAMEFANYA UZEMBE HANDENI TUTAWACHUKULIA HATUA

November 19, 2023 Add Comment

 

Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt Wilson Mahera  akizungumza na waandishi wa habari  mara baada ya kutembelea na kukagua Hospitali ya wilaya ya Muheza
Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt Wilson Mahera  akitembelea maeneo mbalimbali katika Hospitali ya wilaya ya Muheza kushoto ni Mganga Mkuu  wa Mkoa wa Tanga Dkt Japhet Simeo 
Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt Wilson Mahera  akikagua hali ya upatikanaji wa dawa wakati alipotembelea Hospitali ya wilaya ya Muheza
Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt Wilson Mahera  akikagua hali ya upatikanaji wa dawa katika Hospitali ya wilaya ya Muheza

Na Oscar Assenga Muheza

Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt Wilson Mahera amefanya ziara ya kutembelea na kukagua hospitali ya wilaya ya Muheza huku kieleza kwamba kwa wale watakaobainika walifanya uzembe wilayani Handeni watachukuliwa hatua kali ikiwemo kuwanyang’anya leseni.

Dkt Mahera aliyasema hayo mara baada ya ziara hiyo ambapo alisema kwamba Serikali imefanya uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya afya ili wananchi wapate huduma bora hivyo wao hawatakubali kuona watumishi wanakiuka maadili.

Alisema hivyo lazima watumishi wabadilike waache kufanya kazi kwa mazoea na vitendo hivyo visijirudie kwani kufanya hivyo kunapelekea kuzorotesha huduma hivyo niwasihi muendelee kutoa huduma nzuri na kufanya kazi kwa waledi katika kuwahudumia wananchi.

Dkt Mahera alisema yupo mkoani Tanga kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa madaktari wa meno hivyo akaona apite katika Hospitali hiyo kuangalia huduma za afya kutokana na kwamba Serikali ya imewekeza fedha nyingi kuwekeza kwenye sekta ya afya ikiwemo miundombinu.

“Kwa kweli niwapongeze mnaosimamia mradi huu wa Hospitali ya wilaya ya Muheza changamoto niliyoiona hapa ni maji Hospitali ya wilaya kama hii inapata maji kutoka Tang tumekagua maabara maji hakuna bahati nzurti mmechimba kisima na halmashauri imenunua pamp niagize mkamilisha haraka miuondombinu ya maji iweze kuingia kwenye maabara”Alisema Dkt Mahera

“Lakini pia watumishi fanyeni kazi kwa waledi na kujituma na kuendelea kuhakikisha watoto njiti pale wanapojitokeza waendele kuboresha huduma hizo kwenye maeneo yenu kama nchi tumepata mafanikio makubwa sana kuzuia vifo vinavyotokana na mama na mtoto.

Hata hivyo alisema kwamba katika bajeti ya mwaka kesho wataangalia namna ya kupata fedha kwa ajili ya kukamilisha mradi huo ambao ni muhimu kwa ajili ya utoaji huduma

“Mh Rais Dkt Samia Suluhu amekuja na mpango wa M-Mama ili mama anapohitaji huduma ya Rufaa anaipata na niwaambie kwamba kwa wale kwa wale ambao watabainika wanafanya kazi kwa mazoea na kukiuka maadili hatutawavumilia tutaendelea kuwachukulia hatua kali “Alisema

Hata hivyo alisema kwamba miaka 5 iliyopita walikuwa na Hospitali za wilaya 77 sasa zipo 177 za Serikali hivyo hilo ni jambo la kujivunia sana na huduma zinazotolewa kwenye hospitali hizo ni za msingi unakutana na huduma mbalimbali muhimu.

SERIKALI YAUPONGEZA MFUKO WA PEPFAR UKITIMIZA MIAKA 20 YA KURUDISHA MATUMAINI YA WENYE VVU NCHINI.

November 15, 2023 Add Comment

 *Zaidi ya Dola za Kimarekani Bilioni 6 zatumika


*Mwaka 2022 pekee ikitumia Dola 450 milioni kupambana na maambukizi ya ukimwi nchini


Na Zuhura Rashidi, Iringa


SERIKALI ya Tanzania imeupongeza Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR), kwa jitihada zake katika kuleta matumaini mapya katika mikoa iliyoelemewa na mzigo mkubwa wa maambukizi ya ugonjwa wa HIV na Kifua Kikuu.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bi. Halima Dendegu wakati wa ziara ya wawakilishi wa mfuko wa PEPFAR, Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), mashirika yanayotekeleza miradi ya ukimwi pamoja na waandishi wa habari mkoani humo wakitembelea miradi na vituo vinavyotoa huduma za ukimwi ikiwa ni sehemu ya matukio kuadhimisha miaka 20 tokea kuanzishwa kwa mfuko huo.

Mkuu wa Mkoa huyo alisema Iringa ni mmoja wa mikoa iliyoathiriwa sana na maambuki ya VVU lakini kwa msaada wa PEPFAR chini ya Shirika la USAID imewawezesha kuwa na vituo vya huduma na tiba (CTC) 261 kutoka vinane vilivyokuwepo awali, huku 136 vikiendeshwa na USAID vilivyosaidia kuleta mabadiliko chanya katika utoaji elimu na huduma bora kwa kutumia vifaa vilivyoboreshwa na wahudumu wa afya wenye elimu na ujuzi katika utoaji wa huduma bora za afya.

“Tafadhali pokeeni pongezi za dhati kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassani, tunashukuru sana kwa misaada tunayoipokea kwani tunatarajia kushuka kwa maambukizi mapya kwa magonjwa ya ukimwi, kifua kikuu huku tukiendelea kupunguza unyanyapaa kwa wenye VVU.

Awali akizungumza mafanikio miradi ya PEPFAR inayosimamiwa na USAID, Mkurugenzi Mkazi wa shirika hilo nchini, Bwana Craig Hart alisema tokea mwaka 2003 serikali ya Marekali imetoa zaidi ya Dola za Kimarekani Bilioni 6 ikiwa ni pamoja na Dola 450 Milioni kwa mwaka 2022 pekee katika kupambana na ugonjwa wa Ukimwi chini Tanzania.

“Mwaka 2003 ni watanzania 1000 tu waliokuwa wakipokea dawa za kupunguza makali ya VVU (ARV), leo wakati tukiadhimisha miaka 20 ya PEPFAR zaidi ya watanzania milioni 1.5 wananufaika na mpango huu wa tiba wa kuokoa maisha yao ikiwa ni asilimia 98 ya watu wanaoishi ya VVU.

“Misaada yetu kwa watu wa Tanzania ni uwekezaji wa baadae, kwani kufikia mwaka 2050 robo ya watu wote duniani wataishi Afrika, nchini Tanzania theluthi mbili ya idadi ya watu wakiwa ni vijana chini ya umri wa miaka 25, hivyo kufanya uwekezaji katika kizazi kijacho kuwa ni jambo muhimu mno na lisiloepukika”, anasema Bwana Hart.

Naye Mratibu wa Mfuko wa PEPFAR nchini Bi. Jessica Greene alimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa kugusia maeneo manne ambayo mfuko huo umekuwa ukiyapa kipaumbele akiyataja kama; tiba, utoaji huduma bora, vituo vya afya na dawa za kupunguza makali ya VVU.

“Tumeungana na Serikali ya Tanzania katika kuhakikisha vipaumbele hivi vinafanikiwa na tutandelea kuhakikisha watu wenye VVU wanapata huduma boza za matunzo na tiba”, alisema Bi. Jessica.

Baadhi ya miradi inayofadhiliwa na PEPFAR chini ya usimamizi wa USAID ni USAID Afya Yangu Kanda ya Kusini unaolenga utoaji huduma jumuishi za matunzo, matibabu na kuzuia maambukizi ya VVU na kifua kikuu na kuboresha mazingira wezeshi ya utoaji wa huduma bora za afya katika mikoa sita ya kusini mwa Tanzania, huku mradi wa USAID Kizazi Hodari Kusini unaoangalia utoaji wa huduma jumuishi za watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi pamoja na walezi wao ili kuboresha afya, ustawi na ulinzi wa watoto yatima pamoja na vijana katika mikoa 11, miradi hii ikiendesha na Shirika la Deloitte.

Mradi mwingine ni ‘Epic’ unaotekelezwa na Shirika la FHI360 uKjjikita katika kufikia na kuendeleza udhibiti wa janga la VVU huku ukijihusisha katika kutoa msaada wa kitaalamu na huduma za moja kwa moja katika kuondoa vikwazo kufikia malengo ya 95-95-95 ukilenga makundi maalumu wakiwemo wasichana, wamama vijana, wanaume na wanawake walio katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU.

Aidha mradi wa ‘Hebu Tuyajenge’ ukishirikisha watu wanaoishi na VVU, unalenga katika kuongeza matumizi ya huduma za upimaji VVU, tiba na uzazi wa mpango mongoni mwa vijana balehe na wenye VVU ukitekelezwa na Baraza la Taifa la Watu wanaoishi na VVU Tanzania (NACOPHA).

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bi. Halima Dendego, akipokea cheti cha shukurani kwa kutambua  mchango wake katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi na unyanyapaa kwa wenye VVU katika Mkoa wa Iringa, kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, wakati wa ziara ya waandishi wa habari mkoani humo leo ikiwa ni sehemu ya matukio kuadhimisha miaka 20 ya Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR). Ziara hiyo, ililenga kuangalia mafanikio ya miradi inayohudumia wenye VVU na kusimamiwa na mashirika ya Deloitte, Nacopha na FHI360. 
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa mradi wa USAID Afya Yangu Kanda ya Kusini Dk. Marina Njelekela, kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo. Wa kwanza kushoto ni muwakilishi wa PEPFAR  nchini, Bi. Jessica Greene na Mkurugenzi Msaidizi wa USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya   Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, Bi. Dorothy Matoyo (kulia) kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo. Wa kwanza kushoto ni mwakilishi wa PEPFAR  nchini, Bi. Jessica Greene na Mkurugenzi Msaidizi USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann.

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana. Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa Shirika la FHI360, Bwana Bernard Ogwang,  kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa USAID Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa mradi wa Rise project, Maende Makokha, kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo. Kushoto ni mwakilishi wa PEPFAR  nchini, Jessica Greene na  Mkurugenzi Msaidizi USAID Kitengo cha Afya nchini, Bi. Anna Hofmann.

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa Shirika wa Nacopha, Bwana Deogratius Rutatwa, kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa.

Mratibu wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi ( PEPFAR) nchini, Bi. Jessica Greene  akizungumza katika hafla hiyo.

 Mkurugenzi Mkazi  wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bw Craig Hart (katikati) , akipozi kwa picha ya kumbukumbu mjini Iringa leo, na baadhi ya wawakilishi kutoka mfuko wa PEPFAR, USAID na Mashirika yanayoratibu miradi ya Ukimwi inayofadhiliwa na PEPFAR kwa usimamizi wa USAID. 


KAIMU NAIBU MRATIBU MKUU WA MASUALA YA UKIMWI WA PEPFAR NCHINI MAREKANI ATEMBELEA SHUGHULI ZINAZOTEKELEZWA KUPITIA UFADHILI WAO

November 09, 2023 Add Comment












Na Oscar Assenga,TANGA


KAIMU Naibu Mratibu Mkuu wa Masuala ya Ukimwi wa mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Ukimwi (PEPFAR) Dkt Rebbeca Bunnell na ujumbe wake wamefanya ziara ya kutembelea katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo akiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt Grace Magembe.

Akiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo walitembelea shughuli zinazotekelezwa kupitia ufadhili wa PEPFAR kupitia kituo cha kudhibiti na kuzuia magonjwa cha Marekani (CDC) kinachosaidia upatikanaji wa baadhi ya huduma katika Hospitali hiyo huku akiridhishwa na huduma zinazotolewa.

Kupitia PEPFAR, CDC ilianza kusaidia Asasi ya Kiraia ya Gift of Hope Foundation mwaka 2019 ili kuwezesha huduma za kinga miongoni mwa vijana walioathirkka na matumizi ya dawa zaa kulevya na kusaidia upatikanaaji wa huduma za afya kwa watu wanaojidunga kutumia dawa za kulevya.

Hadi kufikia Octoba 2023,The Gift Of Hope Foundation imesaidia zaidi ya wapokea huduma 365 kupata Methadone katika kliniki ya waraibu wa dawa za kulevya (MAT) ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo huku wateja 22 wakiwa katika nyumba ya kusaidia kuacha matumizi ya dawa za kulevya (Sober House).

The Gift Of Hope pia imepanua huduma zake ili kutoa msaada wa kisaikolojia –kijamii na huduma za uhamasishaji,ikijumuisha kukaa kwa muda waa miezi mitatu katika Sober House kwa wapokea huduma wakati wanaahudhuria kliniki za MAT ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo.

Katika ujumbe wake pia wametembelea kliniki ya tiba saidizi ya Methadone (MAT) na kupata taarifa juu ya huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na VVU (WAVIU) zikiwemo huduma za uchunguzi na matibabu ya kifua kikuu,homa ya Ini B na C na uchunguzi wa ukatili wa kijinsia.

Kliniki hiyo ya MAT ilianzishwa mwaka 2020 na hadi kufikia Septemba mwaka huu ilikuwa imewaahudumia jumla ya wapokea huduma 959 kati yao wanawake 27 na wanaume 932 ambapo hiyo ni kliniki pekee ya MAT mkoani Tanga.

“Kliniki hii inatoaa huduma za kina za kuzuia VVU pamoja na tiba matunzo, huduma za kifua kikuu, huduma za msaada wa kisaikolojia na kijamii na uibuaji wa watu wanaojidunga /kutumia dawa zaa kulevya ...The Gift of Hope ni mojawapo ya Asasi za Kiraia zinazoibua na kuunganisha wateja na matibabu katika kliniki ya MAT”

Dkt Bunnell pia ametembelea kliniki ya tiba na matunzo ya VVU (CTC) na kupata taarifa juu ya huduma jumuishi ya tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na VVU ikiwa ni pamoja na ujumuishaji wa huduma za uchunguziz wa saratani ya mlangio wa kizazi.

Ambapo hadi kufikia Octoba 2023 kituo hicho kilikuwaa na zaidi ya wapokea huduma 2,700 waliosajiliwa katika huduma za dawa zaa kufubaza makali ya VVU (ART).

Kwa kipindi cha Octoba 22 hadi Septembea 2023 wanawake 1,287 wanaopataa huduma zaa tiba na matunzo katika kliniki hiyo walifanyiwa uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi ambapo 47 sawa ana asilimia 3.65 walibainika kuwa na viashiria vya awali vya saratani yaani VIA Positive,na 38 walitibiwa kwa tiba Mgandisho (cryotherapy) .

Ambapo wapokea huduma 23 walihisiwa kuwa na saratani ya mlango wa kizazi na walifaanyiwa uchunguzi wa kina na kumi na sita kati yao walithibitishwa kuwa na saratani ya mlango wa kizazi.

Ujumbe huo pia utaelezwa kuhusu shughuli za chanjo ya Human Papillomavirus (HPV) zinazofaanywa katika kituo hicho huku ikieleza walikuwa na wasichana 27 waliostahili kupata chanjo hiyo na walisimamia wasichana 26 kati yao 21 walikamilisha dozi tatu za HPV,wasichana watano wakiwa bado kwenye ratiba ya kupata dozi ya pili.

Kadhalika Dkt Bunnell amepataa fursa ya kuzungumza na vijana rika balehe wa kike na kiume wanaopatiwa huduma tiba na matunzo katikaa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga ili kujifunza wanavyonufaika na afua zinazofadhiliwa na PEPFAR na CDC Hospitalini hapo.

Hata hivyo pia Dkt Bunnell ametembelea maabara hya Hospitali hiyo na kushuhudia uchakataji wa sampuli za damu iliyo kaushwa (DBS) na makohozi kwa ajili ya kipimo cha kifua kikuu na kuelezwa jinsi ambavyo sampuli za wingi wa VVU huchakatwa ili kusafirishwa kwa upimaji kwenye maabaraa husika.

Kwa sasa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga inapokea Ufadhili wa PEPFAR/CDC kupitia Shirika lisilo la Kiserikali la Tanzania Healthe Promotion Support (THPS).


Tanzania Health Promotion Support (THPS) ni Taasisi ya Kitanzania iliyoanzishwa mwaka 2011 kwa kufuatia Sheria ya Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali Na 24 hya mwaka 2002.

THPS inatekeleza kazi zake kwa kushirikiana na Wizara ya Afya,Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalumu,Wizara ya Maendeleo ya Jamii ,Jinsia,Wazee na Watoto ,Ofisi ya Rais -Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Wizara ya Mambo ya Ndani na Wizara ya Afya huko Zanzibar.

Lengo la THPS ni kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa watanzania ,kupitia uimarishwaji wa mifumo ya afya na jamii ili kutoa huduma bora za afya zikiwemo za VVU na UKIMWI,Kifua Kikuu,Kuzuia ukatili wa Kijinsia,Afya ya Mama na Mtoto ,Afya ya Uzazi na Afya ya Vijana  ikiwemo kuboresha mifumo ya maabara na Taarifa za Afya,Uviko 19 na Tafiti za Afya ya Jamii

Mradi wa CDC/PEPFAR Afya hatua (octoba 2021 hadi Septemba 2026) umelenga kutoa huduma jumuishi, katika vituo vya Afya (Kigoma, Pwani, Shinyanga na Tanga) na katika jamii (Kigoma, Pwani na Tanga) huduma za Kinga, matibabu na matunzo ya VVU zikiwemo huduma za kitabibu za Tohara kwa wanaume katika mikoa ya Kigoma na Shinyange na Programu ya Dreams kwa wasichana balehe na wanawake wadogo katika mkoa wa Shinyanga

ZAIDI YA WATOTO LAKI TATU, HUZALIWA WAKIWA NJITI KWA MWAKA- DKT. BITEKO

November 08, 2023 Add Comment

 Na WMJJWM, Dodoma


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Dotto Biteko ametoa wito kwa wadau wa masuala ya Afya ya Watoto nchini, kushirikiana kutokomeza tatizo la watoto waliozaliwa kabla ya wakati (watoto njiti).

Wito huo umetolewa kwa niaba yake na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima wakati wa hafla ya kusherehekea mafanikio ya Ajenda ya Mtoto Njiti (2021) iliyofanyika jijini Dodoma Novemba 07, 2023.

Amesema takribani watoto milioni 15 duniani huzaliwa Njiti huku nchi za Bara la Asia na Afrika hasa kusini mwa jangwa la Sahara, zikiongoza kwa asilimia 80 ya vifo vya watoto hao.

"Inakadiriwa kila mwaka watoto 336,000 huzaliwa njiti nchini Tanzania na zaidi ya watoto 11,500 hupoteza maisha kutokana na changamoto za kuzaliwa njiti. Ni kweli kwamba kiwango cha kuzaliwa kwa watoto njiti hapa nchini kimekuwa kikiongezeka. Hatuna budi kuzidisha mapambano na ningefurahi siku moja itokee taarifa kuwa hakuna vifo vya watoto njiti nchini kwetu," amesema Waziri Dkt. Gwajima.

Waziri Dkt. Gwajima ameipongeza Taasisi ya Doris Mollel Foundation kwa kuzindua na kufanikisha kuhamasisha Wizara ya Afya na wadau wote wanaotoa Bima za afya nchini kujumuisha gharama za matibabu ya watoto njiti katika mifuko yao ya bima pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kujumuisha elimu ya watoto njiti kwenye masomo ya Sayansi na Baiolojia.

Ameongeza kuwa, Serikali inaweka mikakati ya namna bora ya kupiga hatua katika masuala ya kiafya kwa raia na maisha ya watoto nchini lakini ni muhimu kuongeza juhudi za pamoja na wahisani.

Akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Ridhwan Kikwete amebainisha kwamba yeye binafsi akipata nafasi ya kuwasilisha hoja kuhusu sheria ya utumishi na likizo ya uzazi atashauri likizo ya uzazi ifikie miezi sita ili watoto njiti wapate malezi stahiki. Ameongeza kwamba sababu za kuzaliwa watoto njiti ni pamoja na Mila na Desturi pamoja na mimba za utotoni.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Ustawi na Maendeleo ya Jamii Mhe. Fatma Toufiq amesema Taasisi ya Doris Foundation imefanya kazi kubwa na kufikia hatua Serikal kutenga Bajeti ya kuhudumia watoto hao, hivyo Kamati hiyo itaendelea kupigania kuhakikisha sheria ya likizo ya uzazi inapita ili mtoto njiti aweze kupata malezi stahiki. Amewaomba Waheshimiwa Wabunge kupitisha sheria ya wanawake kukaa miezi 6 baada ya kujifungua watoto njiti na wanaume mwezi mmoja.

Awali Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel Foundation, Doris Mollel ameelezea lengo la hafla hiyo ni kujadili namna Serikali na Wadau husika wanavyoweza kufanikisha ajenda kuu ya kisera ya watoto njiti ambayo ni kurekebishwa kwa sheria ya likizo ya uzazi ya sasa kutoka siku 84 hadi 180 ambayo ni moja ya ajenda tatu zilizozinduliwa na Kamati ya Bunge ya Huduma za Maendeleo ya Jamii na Doris Mollel Foundation mwaka 2021.













TADB YAADHIMISHA MWEZI WA SARATANI YA MATITI KWA ELIMU NA VIPIMO KWA WANAFANYAKAZI WAKE

November 01, 2023 Add Comment

 Na Mwandishi Wetu


Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imeendesha semina ya mafunzo ya uelewa wa saratani ya matiti , saratani ya mlango wa shingo ya kizazi, saratani ya tezi dume na maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa wafanyakazi wake.

Semina hiyo iliyoambatana na upimaji kwa wafanyakazi hao, iliendeshwa kama sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali katika kukabiliana na Saratani nchini.

Akiongea wakati wa semina hiyo, Mkuu wa rasilimali watu na utawala wa TADB Bi. Noela Ntunkamazina alisema kuwa kwa kushirikiana na Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, (ORCI) TADB wameungana na mataifa mengine kuwaongezea uelewa wa saratani mbalimbali wafanyakazi wake mwezi Oktoba ambao unatambulika kama mwezi wa kuongeza uelewa wa Saratani ya matiti.

“Kwa kutambua kuwa saratani ni ugonjwa unaoathiri jinsia zote na kwa kuelewa kuwa kupitia upimaji wa afya mara kwa mara saratani hugundulika mapema na hivyo kwa kupata tiba sahihi muathirika huweza kupona, kama TADB tumeona vyema kuwapa wafanyakazi wetu fursa ya kupata elimu na kupima ilikufahamu hali zao za kiafya,” alisema.

Daktari Bingwa magonjwa ya Saratani kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Sadiq Siu alibainisha kuwa saratani ya matiti ni saratani ya pili inayoongoza kwa vifo vya wanawake nchini ikitanguliwa na saratani ya shingo ya uzazi. Pia alibainisha kuwa saratani ya matiti inaathiri siyo tu wanawake bali hata wanaume.

“Naipongeza TADB kwa kuona umuhimu wa kuwaletea wafanyakazi wake fursa hii muhimu ya kupata uelewa wa saratani mbalimbali na pia kupata nafasi ya kupima saratani ya matiti, saratani ya shingo ya kizazi na saratani ya tezi dume. Ni jambo muhimu kwa taasisi nyingine kuiga na kuwaelimisha wafanyakazi wake. Kwa pamoja tunajukumu la kuchangia kupunguza vifo vitokanavyo na saratani. Ugonjwa huu unakua kwa kasi. Ikumbukwe kuwa kwa kugundulika mapema na kuzingatia matibabu sahihi, saratani inaweza kutibika.

Bi. Felister Rutta mmoja wa wafanyakazi wa TADB aliishukuru menejimenti ya benki hiyo kwa kuwaletea semina hiyo ambayo alisema itawasadia wanyakazi kuufahamu ugonjwa huo na hivyo kuchukua tahadhari ikiwa ni pamoja na kuwaelekeza ndugu jamaa na marafiki.
Daktari Bingwa wa magonjwa ya Saratani kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Sadiq Siu (wa kwanza kushoto aliyesimama)akitoa mada juu ya saratani ya matiti, saratani ya mlango wa shingo ya kizazi na saratani ya tezi dume kwa wafanyakazi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) ikiwa ni sehemu ya benki hiyo kuadhimisha mwezi wa saratani ya matiti kwa kutoa elimu kwa wafanyakazi wake pamoja na kuwafanyia vipimo.

Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) wakifuatilia kwa makini mada juu ya saratani ya matiti, saratani ya mlango wa shingo ya kizazi, saratani ya tezi dume iliyokuwa ikitolewa na Daktari Bingwa wa magonjwa ya saratani kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Sadiq Siu ikiwa ni sehemu sehemu ya benki hiyo kuadhimisha mwezi wa saratani ya matiti kwa kutoa elimu kwa wafanyakazi wake pamoja na kuwafanyia vipimo.