KAMPUNI YA VIVO ENERGY TANZANIA YATOA HUDUMA YA VYOO SAFI KWA SHULE KWA SHULE YA MSINGI KIUNGANI

October 23, 2023

 Kampuni ya Vivo Energy Tanzania, imekabidhi vyoo vilivyokarabatiwa katika Shule ya Msingi ya Kiungani. Ishara hiyo inaonyesha dhamira ya kampuni kutunza mazingira na kuhamashisha uboreshwaji wa afya katika jamii.


Akizungumza katika hafla ya kukabidhi, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Vivo Energy Tanzania, Bw.Mohamed Bougriba alisema, “Leo tunakabidhi vyoo hivi kama kielelezo cha hamasa yetu ya kushirikiana na wadau mbalimbali katika jamii kuboresha elimu na afya ya watoto. Tunaamini kwa dhati kuwa maboresho haya hayataleta manufaa ya kimwili tu, bali hata ustawi wao wa akili, afya na maisha yao kwa ujumla’

Aliendelea kwa kuhimiza wanafunzi kusoma kwa bidii ili kufikia ndoto zao, akimnukuu Baba wa taifa, Mwalimu Julius Nyerere kwa kusema, "Elimu si njia ya kuepuka umasikini, ni njia ya kupambana nao.’

Naye Mkuu wa Shule ya Msingi Kiungani Bibi Bonvilia Mlay alitoa shukrani zake za dhati kwa kampuni ya Vivo Energy Tanzania huku akisisitiza kuwa vyoo hivyo vipya vitawawezesha watoto wa shule hiyo kupata mazingira safi na salama na hivyo kuwaepusha na maradhi yatokanayo na usafi duni.

Meneja Mawasiliano wa Vivo Energy Tanzania, Grace Kijo pia alitoa shukrani zake za dhati kwa viongozi wa serikali za mitaa waliohudhuria, kwa ushirikiano wao mkubwa katika uendeshaji wa kampuni hiyo. Aliahidi kuendelea kufanya kazi kwa karibu na viongozi wa eneo hilo ili kuleta mabadiliko chanya na ya kudumu kwa jamii.

Vivo Energy Tanzania inaendelea kutekeleza sera yake ya uwajibikaji kwenye jamii, kwa kutambua kwamba kwa kuleta mabadiliko chanya katika ngazi ya elimu, inachangia katika kuboresha jamii kwa ujumla.

Kampuni inajivunia kuunga mkono Shule ya Msingi Kiungani katika dhamira yake ya kuweka mazingira safi na salama kwa wanafunzi wake na inatarajia kuendelea kushirikiana na jamii ili kuleta mabadiliko yenye tija.

Hafla hiyo ilihitimishwa na ushairi kutoka kwa wanafunzi wa darasa la nne wa shule hiyo, ikiwa ni sehemu ya kutoa shukrani kwa Vivo Energy Tanzania.


Mkurugenzi Mtendaji wa  Kampuni ya Vivo Energy Tanzania, Mohamed Bougriba (watatu kulia) na Afisa Elimu wa Manispaa ya Temeke, Abdul Buhety (wapili kulia) wakikata utepe  katika hafla ya kukabidhi choo chenye matundu 16 kilichokarabatiwa na kampuni hiyo kwa shule ya msingi Kiungani iliyopo Kurasini Manispaa ya Temeke jijini Dar es salaam. Kulia ni  Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bonivilia Malya.

Mkurugenzi Mtendaji wa  Kampuni ya Vivo Energy Tanzania, Mohamed Bougriba (wa pili kulia) akikabidhiwa tuzo ya heshima na Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi  Kiungani iliyopo Kurasini Manispaa ya Temeke ,Bonivilia  Malya mara baada ya  kukabidhi choo chenye matundu 16 kilichokarabatiwa    na kampuni hiyo. Wengine kushoto ni Afisa Elimu Manispaa ya Temeke, Abdul Buhety na kulia ni Meneja Masoko na Mawasiliano Vivo Energy Tanzania, Grace Kijo.

Mkurugenzi Mtendaji wa  Kampuni ya Vivo Energy Tanzania, Mohamed Bougriba akionyeshwa baadhi ya matundu ya vyoo na Mwanafunzi wa Darasa la Sita, Baraka Issa  mara baada ya kukabidhiwa msaada wa ukarabati wa vyoo hivyo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »