MAKAMBA AFUNGUA KONGAMANO LA VYUO VYA ELIMU YA JUU KUHUSU MUUNGANO

April 21, 2018



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akifungua kongamano la vijana kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vilivyopo mkoani Dodoma. Jumla ya Vyuo sita vimeshiriki katika Kongamano hilo lililofanyika katika Chuo cha Mipango, Dodoma na mada kuu ikiwa ni fursa zilizopo katika Muungano.

Sehemu ya wanafunzi kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vilivyopo mkoani Dodoma wakifuatilia hotuba ya ufunguzi kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba. Kongamano hilo limefanyika katika Chuo cha Mipango Dodoma na kuhudhuriwa na wanafunzi kutoka Vyuo vya Hombolo, Chuo cha Elimu ya Biashara, St. John, Chuo cha Mipango, Chuo cha Madini na Chuo Kikuu cha Dodoma.


Sehemu ya wanafunzi kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vilivyopo mkoani Dodoma wakifuatilia hotuba ya ufunguzi kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba. Kongamano hilo limefanyika katika Chuo cha Mipango Dodoma na kuhudhuriwa na wanafunzi kutoka Vyuo vya Hombolo, Chuo cha Elimu ya Biashara, St. John, Chuo cha Mipango, Chuo cha Madini na Chuo Kikuu cha Dodoma.



Waratibu wa kongamano hilo, kutoka kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Muungano Bi. Lupy Mwaikambo, Bw. Sifuni Msangi Kaimu Mkurugenzi Idara ya Muungano na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Joseph Malongo wakifuatilia hotuba ya ufunguzi kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »