Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu

March 15, 2017
Leo March 15, 2017 Rais Magufuli ametengua uteuzi na kumsimamisha kazi Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge) Uledi Abbas Mussa. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa kutenguliwa kwa uteuzi na kusimamishwa kazi kwa Uledi Abbas Mussa kunaanzia leo tarehe 15 Machi, 2017.
Hatua hiyo imechukuliwa ili kupisha uchunguzi zaidi dhidi ya Uledi Abbas Mussa kufuatia kutozingatiwa kwa taratibu zinazotakiwa katika kushughulikia masuala ya uwekezaji.
Chanzo Millardayo.com

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »