SERIKALI kupitia Wizara ya Maliasili
na Utalii imeshauriwa kuweka msukumo mkubwa kwenye kutangaza vivutio vya utalii
vilivyopo kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini ili kuweza kutumia fursa hiyo
kukusanya mapato.
Ushauri huo ulitolewa leo na
Mkurugenzi Mtendaji wa Kibanga Tours&Travel, Emanuel Kibanga (Pichani kushoto)wakati
akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema ipo mikoa yenye fursa nyingi
za kiutalii lakini inashindwa kuonekana kutokana na kutotangaza ipasavyo.
Alisema kuwa iwapo suala hilo
litasimamiwa na kuchukulia hatua zinazokusudiwa itasaidia kuwapa ufahamu nzuri
watalii kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo mikoa ya kanda ya kaskazini
ikiwemo Tanga kwa wingi kutokana na kuwepo na historia ya kubwa ya kale.
“Ukiangalia mikoa ya Kanda ya Kaskazini inavivutio vyingi sana vya
utalii ukianzia na mkoa wa Tanga lakini vinakosa fursa ya kuonekana na wageni
wanaokuja kutembea hapa nchini na hivyo kuikosesha serikali mapato “Alisema
Mkurugenzi huyo.
Aidha pia alitumia nafasi hiyo
kuushauri mkoa wa Tanga kuandaa kongamano maalumu ambalo litaweze kutoa fursa
za kutangaza vivutio vya utalii kwa lengo la kuongeza ukusanya mapato.
Hata hivyo alisema wakati umefika
sasa watanzania wawekeze kwenye maeneo yaliyokuwa karibu na vivutio vya utalii
ili kuweza kuhamasisha wageni kwenda kuvitembelea ili kuharisisha.