TRL KUSAFIRISHA SARUJI YA TANGA KWA NJIA YA RELI

March 24, 2016
Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) Masanja Kadogoso kulia na Mkurugenzi wa Kampuni ya Saruji ya Simba Cement,Reinhardt Swart  wakitiliana  saini ya makubaliano baina yake na Kampuni ya Saruji ya Simba iliyopo Jijini Tanga kwa lengo la Kampuni hiyo kuanza kusafirisha shehena za mizigo kwa kutumia njia ya reli ili kuokoa athari za uharibifu wa Barabara zinazojitokeza kwa sasa kutokana na usafirishaji kwa kutumia malori
Waziri wa wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa kushoto akibeba Mfuko wa Saruji na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Saruji ya Simba Reinhardt Swart kulia baada ya utiaji wa saini ya makubalinao saini ya makubaliano baina yake na Kampuni ya Saruji ya Simba iliyopo Jijini Tanga kwa lengo la Kampuni hiyo kuanza kusafirisha shehena za mizigo kwa kutumia njia ya reli ili kuokoa athari za uharibifu wa Barabara zinazojitokeza kwa sasa kutokana na usafirishaji kwa kutumia malori

Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa akishuka kwenye ngazi mara baada ya kupakia mfuko wa saruji saini ya makubaliano baina yake na Kampuni ya Saruji ya Simba iliyopo Jijini Tanga kwa lengo la Kampuni hiyo kuanza kusafirisha shehena za mizigo kwa kutumia njia ya reli ili kuokoa athari za uharibifu wa Barabara zinazojitokeza kwa sasa kutokana na usafirishaji kwa kutumia malori.




SERIKALI imetia saini ya makubaliano baina yake na Kampuni ya Saruji ya Simba iliyopo Jijini Tanga kwa lengo la Kampuni hiyo kuanza kusafirisha shehena za mizigo kwa kutumia njia ya reli ili kuokoa athari za uharibifu wa Barabara zinazojitokeza kwa sasa kutokana na usafirishaji kwa kutumia malori.

Makubaliano hayo yalitiwa saini na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Reli Tanzania(TRL)Masanja Kadogosa na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Saruji ya Simba Reinhardt Swart wakishuhudiwa na Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa.

Akizungumzia hatua hiyo Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa alisema kwa sasa serikali inatumia shilingi milioni moja kwa kila kilometa moja ya Barabara kiasi ambacho ni kikubwa ukilinganisha na gharama ambazo zingetumika kwa ajili ya kuboresha njia za reli.

Prof.Mbarawa alisema Kampuni hiyo itakuwa ikisafirisha tani 35,000 sawa na tani 500,000 kwa mwaka  ambapo TRL itakusanya shilingi milioni 40 kwa kila mzigo jambo ambalo litarudisha uhai wa njia za reli na kuondoa uharibifu wa Barabara.

“Kwa mwezi magari haya makubwa yaani malori yanayobeba mizigo yanafanya zaidi ya tripu 3,500 sawa na tripu 35000 kwa mwaka sasa jiulize ni kwa namna gani Barabara zinaharibika na kusababisha gharama kubwa sana za ukarabati kwa serikali ….hivyo tunaamini mazungumzo yetu yataenda vizuri na kufika tulikokusudia”,alisema Waziri huyo.

Aliwataka watumishi wa Kampuni ya Reli (TRL)kufanya kazi kwa bidii hasa kwa kutambua kuwa kampuni hiyo ndiyo moyo wa uchumi wa nchi katika sekta ya usafirishaji na kamwe serikali haitamvumilia mtumishi mzembe kwenye sekta hiyo.

“Lazima wafanyakazi mshirikiane na kila mmoja ajitume katika kutimiza wajibu wake bora niwe na wafanyakazi wachache hata ishirini wenye kuliko kukaa hapa na watu wanaoiba dizeli na oili kama mtu hawezi na aondoke hatuwezi kuendelea kufanya kazi kwa mazoea na kuharibu shirika hili ambalo ni tegemeo la kiuchumi kwa Taifa”,alisisitiza.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TRL Masanja Kadogosa akizungumza hivi karibuni alisema kuwa kwa mwaka 2014/2015 Kampuni ya Saruji ya Simba Tanga ilisafirisha shehena ya mizigo tani 44,000 ambapo kutoka Julai hadi Disemba 2015 ilisafirisha tani 24,960.

Kadogosa alisema katika kufufua Kampuni hiyo ya TRL serikali imewekeza kiasi cha  Dola za Kimarekani Milioni 100 sawa Bilioni 200 za kitanzania huku ikilenga kuboresha huduma mbalimbali ikiwemo matengenezo ya miundo mbinu ya njia za reli.

Naye MKurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha saruji Swart alisema kuwa hatua hiyo itapunguza gharama za usafirishaji wa shehena za mizigo ya saruji ambapo katika safari zake wanatarajia tani 20,000 za saruji kutoka Pongwe kwenda Kigoma na tani 15,000 kutoka Pongwe kwenda Mwanza.

“Uzalishaji wa saruji kwa mwezi ni tani 105,00 na tunatarajia kusafirisha tani 35,000 kila mwezi kwenda mikoa mingine tukiamini njia hii itakuwa ni nafuu zaidi,”,alisema Mkurugenzi huyo.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella aliwahakikishia wamiliki wa kiwanda hicho kwamba serikali ya mkoa imejipanga vizuri kuhakikisha inaimarisha ulinzi na usalama wa mizigo yao ili kusitokee hujuma wakati wa usafirishaji.

“Tunajua kuna hujuma za wizi wa mizigo na mataruma ya reli lakini kama mkoa tutahakikisha tunapambana na hali hiyo kwa hali na mali ,”alisisitiza Shigella.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »