Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) Kagyabukama Kiliba (wa tatu kutoka kushoto) akiwa na baadhi
ya viongozi wa mkoa wa Dar es salaam na Halmashauri ya Wilaya ya Ilala
wakiwasili eneo la soko la Feri jijini Dar es salaa kujionea hali ya
usafi wa soko hilo.
Baadhi
ya wahudumu wakiendelea na usafi eneo la soko la Feri jijini Dar es
salaa huku Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Kagyabukama Kiliba na msafara wake
wakikagua na kujionea hali ya usafi wa soko hilo.
Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) Kagyabukama Kiliba (aliyevaa miwani) akishuhudia Majuto Alli
Majuto akiendelea na kazi yake ya kukaanga samaki aina ya pweza katika
soko la samaki la Feri jijini Dar es salaam.
Vijana
wakiendelea kazi ya kukaanga samaki katika soko la Feri katika
mazingira ambayo hali ya usafi siyo ya kuridhisha kwa ajili ya kulinda
afya ya mlaji.
Kijana
Hamisi Misango akimnyanyua samaki aina ya taa ili amuandae tayari kwa
kumuuza kwa wateja wanafuata kitoweo katika soko la samaki la Feri
jijini Dar es salaam.
Msafara
wa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa (TAMISEMI) Kagyabukama Kiliba wakishuhudia moja ya shimo la
maji mchafu ambayo yanaweza kuhatarisha usalama wa afya ya wananchi
wanaofika katika soko la samaki la Feri jijini Dar es salaam au wale
watakaotumia samaki hao kama hawatakuwa wameandaliwa katika hali ya
usafi na salama. Lengo ni wananchi wengi wanaofika sokoni hapo ni
kununua samaki waweze kuwauzia watu wasoweza kufika sokoni hapo na
wengine kwa ajili ya matumizi yao ya nyumbani.
Mama
lishe Zainabu Hamad anayefanya shughuli zake za kutoa huduma ya chakula
katika soko la Feri zoni 4 kizimba namba 12 akiongea na Naibu Katibu
Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) Kagyabukama Kiliba alipotembelea sokoni hapo kwa lengo la
kuhamasisha suala la usafi kwa manufaa ya kulinda afya ya wananchi
wanatumia huduma hiyo wakiwa sokoni humo.
Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) Kagyabukama Kiliba na msafara wake wakiwa katika eneo la soko
la Kariakaoo kukagua suala la usafi unavyozingatiwa sokoni humo. Licha
ya uchafu uliopo katika soko la Kariakoo, wafanyabiashara wa matunda
hawachukui tahadhari yeyote ya kulinda afya za walaji wa matunda ambapo
wanauza matunda aina ya mananasi bila kuyafunika sa kusababisha inzi
kuyazonga zonga matunda hayo kitu ambacho ni hatari kwa suala la usalama
wa afya ya malaji.
Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) Kagyabukama Kiliba akijionea wafanyabiashara wadogo
walivyovamia miundombinu ya Mradi wa Mabasi yaendayo kwa kasi katika
eneo la Kariakoo jijini Dar es salaam huku mafundi wakiendelea na kazi
ya kupaka rangi.
Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) Kagyabukama Kiliba akitembelea maeneo mbalimbali ya soko la
Kariakoo jijini Dar esa salaam.
(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)
(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)