WATOTO BADO WANAENDELEA KUDHULUMIWA UTOTO WAO- UMOJA WA MATAIFA

October 18, 2015

 Picha hii kutoka maktaba inamwonyesha mtoto ambaye anatumika kama askari na hivyo kumnyima haki yake ya msingi ya kuishi utoto wake,  pamoja na kupata huduma zake za msingi kama vile afya, elimu, malenzi na ukuaji  wenye hadhi. Pamoja na  Umoja wa Mataifa kuendelea na kampeni yake ya kupinga watoto  kutumika kama askari, bado  taarifa za hivi karibu za Umoja wa Mataifa, zinaeleza kuwa watoto bado wanaendelea kutumika katika baadhi ya maeneo kama askari,  huku wengine wakiingizwa katika  biashara haramu  zikiwamo za ngono.
 Vickness Mayao kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii,  Jinsia na  Watoto,  akichangia majadiliano kuhusu haki za mtoto wakati wa Mkutano wa   Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Kamati iliyokuwa ikijadili kuhusu   haki za mtoto ambapo  akizungumza kwa  Niaba ya Serikali   Bi. Mayao amesema Serikali  inaendelea na uboreshwaji wa Sheria mbalimbali zinazolinda haki ya Mtoto  huku  ikisisitiza kwamba wajibu wa kwanza wa kumlinda mtoto  dhidi ya  madhara yoyote  ni ya Wazazi wenyewe.  aliyekaa nyuma ni Afisa mwingine kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii,  Jinsia na Watoto Bi. Grace Mbwilo
 .Pamoja na  kufanyika kwa  mikutano ya Kamati ya Tatu ya Baraza  Kuu la  Umoja wa Mataifa,  Mikutano  ya Kamati nyingine zikiwamo ya Pili inayohusika na masuala ya  Uchumi na Maendeleo pia imekuwa ikiendelea na vikao vyake. Pichani (katikati)ni Bw. Ahmed Makame Haji Kamishna wa  Tume ya  Mipango kutoka Serikali ya  Mapinduzi Zanzibar akiwa katika  moja wa Mikutano ya Kamati ya   Uchumi na Maendeleo  wapo  pia Bi. Halima Wagao kutoka Wizara ya Fedha ( ZNZ na Bi. Mtumwa Idrissa kutoka  Tume ya Mipango ( ZNZ)
 Bw. Suleiman Said Ali. Afisa  Mambo ya Nje , Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ( ZNZ) akifuatilia Majadiliano ya Kamati ya Nne ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, iliyokuwa ikijadili kuhusu masuala ya  misaada  ya  ulipuaji wa mabomu ya  Ardhini,  Bw.  Ali pia alishiriki katika Majadiliano ya Umalizwaji wa Ukoloni kwa  Makoloni 17 ambayo bado  hayajapata fursa ya kujitawala na kujiamulia  mambo yake yenyenyewe likiwamo  Koloni la Western Sahara, koloni pekee barani Afrika.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »