WARSHA YA KUPITIA MKATABA WA KIMATAIFA WA MINAMATA KUHUSU KEMIKALI.

September 29, 2015

X4
Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais ambaye ni mgeni rasmi katika Warsha ya Wadau ya kupitia Mkataba wa Kimataifa wa Minamata unaohusu kemikali aina ya Zebaki na madhara yake katika mazingira, Dk. Julius Ningu akizungumza katika ufunguzi wa Warsha hiyo ya siku mbili inayoendelea jijini Dar es Salaam Septemba 29, 2015.
(Picha na OMR)
X1
Baadhi ya wajumbe katika Warsha ya Wadau kupitia Mkataba wa Minamata unaohusu kemikali aina ya Zebaki na madhara yake katika mazingira wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa katika Warsha ya siku mbili inayoendelea jijini Dar es Salaam
X2
Warsha ikiendelea.
X3 
Washiriki wa Warsha ya Wadau ya kupitia Mkataba wa Minamata kuhusu Kemikali aina ya Zebaki na Madhara yake katika Mazingira wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wa Warsha hiyo, Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Julius Ningu jijini Dar es Salaam.
…………………………………………………………………………………
Na victor Mariki na Pius Yalula – Ofisi ya Makamu wa Rais
Kuendelea kuwepo kwa kemikali aina ya zebaki katika mazingira ya binadamu na shighuli za kila siku za binadamu uwepo wa zebaki katika mzunguko wa chakula na madhara yake kiafya na mazingira ni baadhi ya hatua zinazotakiwa kuchukuliwa kwa pamoja katika kiwango cha kitaifa na kimataifa. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais, Dr. Julius Ningu wakati wa ufunguzi wa warsha ya siku mbili inayoendelea ya kupitia Mkataba wa kimataifa wa Minamata unaohususu kemikali aina ya zebaki na madhhara yake katika mazingira uliofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira Duniani (GEF) kupitia UNEP. Kwa mujibu wa Dr. Ningu kufuatia utafiti mdogo uliofanywa kuhusu kemikali ya zebaki nchini Tanzania umeonesha kuna takwimu chache zilizopo kuhusu matumizi ya kemikali ya zebaki ambayo kemikali hizi zaidi hutumika katka machimbo madogo ya dhahabu, vifaa vya kielotroniki vilivyoisha mda wake ikiwemo matumizi mbalimbali ya vifaa vya hospitali na kliniki pamoja na uvuvi haramu kwa kutumia sumu. Aidha Dr. Ningu alisema pamoja na juhudi za Serikali katika kukabiliana na tatizo hili bado changamoto hiyo imekuwepo hivyo kutaka juhudi za pamoja kufanyika ambapo kwa kuwata wanawarsha na jamii kwa ujumla kushirikiana kwa pamoja katika kutekeleza Mkataba wa Minamata kwa kutoa elimu kwa umma na uelewa kuhusu matumizi mabaya ya zebaki na athari zake katika mazingira.
Warsha hiyo ya kupitia Mkatabawa Kimataifa wa Minamata unaohusu kemikali aina ya zebaki na madhara yake katika mazingira, imehudhuriwa na wadau mbalimbali, sekta mtambuka , taasisi za serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali na kuratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais chini ya Ufadhili wa Mfuko wa Mazingira Duniani (GEF) kupitia shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira UNEP.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »