PAMBANO LA STARS &SUPER EAGLE LASOGEZA MBELE MECHI YA AFRICAN SPORTS NA COASTAL UNION.

September 03, 2015




 Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Tanga,Frank Maduga akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mechi
NA MWANDISHI WETU, TANGA.
PAMBANO la Mechi ya kirafiki kwa mahasimu wa soka mkoa wa Tanga baina ya Coastal Union na African Sports limelazimika kusogezwa mbele kutokana na siku lilatalochezwa kutakuwa na mechi kati ya timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars” na Super Eagle ya Nigeria.
Viingilio kwenye mechi hiyo vitakuwa ni kati ya 5000 na 3000 kwa wakubwa na shilingi 1000 kwa watoto ili kuweza kutoa fursa kwa wapenzi wa soka kushuhudia mechi hiyo.
 

Mchezo huo wa Stars na Super Eagle ya Nigeria utakuwa ni wa kuwania kufuzu fainali za kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazochezwa mwaka 2017 nchini Gabon.



Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Tanga,Frank Maduga akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mechi
Mechi hiyo imeandaliwa pamoja na kudhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii Mkoa wa Tanga (NSSF) ambapo kabla ya mchezo huo kutakuwa na shughuli mbalimbali kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani ikiwemo uandikishaji wa kujiunga na huduma za NSSF pamoja na kujiandikisha kwa mafao ya matibabu yanayotolewa bure kwa wanachama wa mfuko pindi watimizapo miezi mitatu ya uanachama hai.
Afisa Matekelezo wa NSSF Mkoa wa Tanga,Athumani Juma Mohamed akizungumza jambo wakati wa mkutano wa waandishi wa habari leo
 Akizungumza na waandishi wa habari leo,Meneja wa shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),Frank Maduga amesema kuwa sababu za kusogezwa mbele mchezo huo ni kutoa fursa wapenzi wa soka nchini kuishuhudia timu ya Taifa na baadae kujionea mechi hiyo siku itakayopangwa.
Alisema kuwa shirika hilo mkoani hapa limeamua kutumia siku ya Jumamosi Septemba 5 mwaka huu kwa ajili ya kutoa elimu juu ya hifadhi ya jamiio na huduma zinazotolewa na shirika hilo ikiwemo upimaji wa afya bure,uandikishaji wa wanachama katika mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii na pia kwa ajili ya mafao ya matibabu ili wanufaike na huduma hizo.

Afisa Matekelezo wa NSSF Mkoa wa Tanga,Chiku Mohamed Saidi akigawa taarifa kwa waandishi wa habari kwenye mkutano huo.
Aidha alisema kuwa wameandaa michuano ya mpira wa miguu kwa wanawake itakayofanyika siku hiyo ikihusisha timu za Pangani, Muheza na timu mbili za wilaya ya Tanga ambapo mshindi wa mashindano hayo atapokea zawadi za ushindi pamoja na mshindi wa mechi ya watani wa jadi mjini Tanga iliyohamishiwa Jumapili ili kutoa fursa kwa wadau wengine wa michezo kushuhudia na kuishangilia timu ya Taifa inayocheza siku inayofuata.

Meneja huyo alisema kuwa siku ya Jumamosi kutakuwa na burudani toka kwa vikundi vya sanaa na mechi za wanawake zitaanza saa 2:30 asubuhi hadi saa 6:00 na fainali kufanyika jioni.
Aliongeza kuwa pamoja na kusaidia timu za Tanga na kukuza katika azma ya kukuza viwango vya soka mkoani hapa tukio linguine ni uzinduzi wa huduma ya maji kupitia tanki lililojengwa upya katika kijiji cha Wazee Mikanjuni.
Afisa Mafao wa NSSF Mkoa wa Tanga na Mratibu wa Shughuli hiyo,Salum Maftaa kushoto akifurahia jambo na wadau wa michezo leo
 Alieleza kuwa pia wanachama hao wapya watapata fursa ya kupata huduma ya matibabu ya ndani na nje ya mkoa zikiwemo hospitali za rufaa ndani ya muda mfupi wa miezi mitatu bila kuathiri michango yao au kwa manene mengine watapata matibabu ya bure.
 
Hata hivyo alisema kuwa huduma za mikopo inayotolewa na shirika hilo kupitia vyama vya akiba vya kuweka na kukopa (Saccos) itapatikana kwa wanachama wanaochangia si chini ya miwezi sita na ambao wamejiunga kwenye Saccoss zinakidhi vigezo.
 
  “Jamani ndugu zangu kubwa kuliko yote,Uzee haukwepeki na pia ulemavu na umauti ni majanga ambayo hakuna ajuaye yatamkuta lini na hivyo kinga ya uhakika dhidi ya kukosekana au kupungua kwa kipato kwa mtu na wategemezi ni kujiunga na mpango wa hifadhi ya jamii unaoendeshwa na NSSF “Alisema Maduga.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »