Mgeni
Rasmi katika Semina ya Kukuza Uelewa wa Usimamizi wa Mazingira kwa
Watendaji wa Halmashari ya Jiji la Tanga, Bwana Salim Chima ambaye pia
ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga akifungua Semina hiyo ya siku moja
iliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
Mkurugenzi
wa Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Julius Ningu
akizungumza jambo katika Semina ya Kukuza Uelewa katika Masuala ya
Mazingira kwa Watendaji wa Halmashari ya Jiji la Tanga iliyofanyika
jijini humo leo.
wakurugenzi
wasaidizi wa Mazingira toka Ofisi ya Makamu wa Rais Bi Esther Makwaia
na Bi Magdalena Mtenga wakiwa pamoja na Mgeni Rasmi Bwana Salim Chima
wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa.
Washiki wa semina
Mgeni
Rasmi katika Semina hiyo Bwana Salim Chima akiwa katika picha ya pamoja
na washiriki wote walioshiriki katika Seminas hiyo
…………………………………………………………..
Na Victor Mariki – Ofisi ya Makamu wa Rais
Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira
imebainisha kuwa takribani ya asilimia 61 hadi 75 ya eneo la ardhi ya
Tanzania imeathirika na janga la ukame ambao unaweza kupelekea uzorotaji
katika ukuaji wa uchumi na hata kutoweka kwa baadhi ya viumbe hai.
Hayo yalielezwa na Afisa Mazingira wa Ofisi ya Makamu wa Rais,
Bi Zainab Shaban Bungwa wakati akitoa mada katika semina ya kukuza
uelewa wa masuala ya usimamizi wa mazingira kwa watendaji wa Halmashauri
ya jiji la Tanga mkoani humo leo.
Aidha Bi Bungwa alifafanua kuwa uchumi wa Tanzania unategemea
kwa kiasi kikubwa rasimali asili kama vile ardhi, misitu, wanyamapori na
maji ambapo inakadiriwa asilimia 75 ya wanachi waishio vijijini
hutegemea zaidi ardhi katika uendeshaji wa maisha yao.
Pia aliongeza kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira imechukua
hatua mbali mbali katika kukabiliana na janaga hilo kwa kuunda sera,
mikakati na sheria mbalimbali za kudhibiti uharibifu wa mazingira
nchini.
Baadhi ya mikakati, sera na sheria hizo ni Mkakati wa Hatua za
Haraka Kuhifadhi Mazingira na Vyanzo vya Maji, Mkakati wa Bahari na
Mabwawa, Program za Kupambana kwa Kuenea Hali ya Jangwa na Ukame,
Mkakati wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi pamoja na Program na
Miradi inayotekelezwa na Sekretarieti ya Mikoa katika suala la Utunzaji
Mazingira.
Sanjari na hayo Bi Bungwa alienda mbele zaidi kusema kuwa hivi
sasa robo ya dunia ipo hatarini kukumbwa na hali ya jangwa kwa kuwa
zaidi ya hekta bilioni 3.6 za ardhi yake tayari zimeshaathiriwa na janga
hilo ambalo mpaka sasa limeathiri zaidi ya watu milioni 900 duniani
kote .
Kwa upande wa bara la Afrika hivi sasa hali hiyo ya jangwa
imekuwa ni tatizo sugu kwakuwa mpaka sasa tayari asilimia 73 ya ardhi
yake imeshathirika vibaya na janga hilo hali ya jangwa.