matukio kutoka Bungeni DodomA

March 19, 2015

1
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Mhe.Juma Nkamia akijibu swali la Mhe.Haroub Shamis Mbunge wa jimbo la Chonga kuhusu jinsi gani serikali inawasaidia waadishi kuandika habari za kibiashara,Mjini Dodoma.
2
Mhe.Victor Kawawa akichangia hoja juu ya Muswada wa sheria ya udhibiti wa Ajira za wageni wa mwaka 2014 uliyosomwa na Waziri wa Kazi na Ajira Mhe. Gaudensia Kabaka, leo tarehe 18/03/2015 bungeni Mjini Dodoma.
3
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Janet Mbene akijibu swali la Mhe.Philipa Mturano Mbunge wa viti maalum lililokuwa likihoji ni namna gani Serikali imejipanga kuthibiti biashara ya vyuma chakavu kutokana na kuwepo na wizi wa mabomba.
4
Waziri wa Kazi na Ajira Mhe.Gaudensia Kabaka akisoma muswada wa sheria ya Udhibiti wa Ajira kwa Wageni ya mwaka 2014 kwa mara ya pili ndani ya Bunge, leo tarehe 18/03/2015 Mjini,Dodoma.
5
Waziri wa Fedha Mhe.Saada Mkuya (kushoto) akizungumza naWaziri wa Habari, Wizara wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe.Fenella Mukangara nje ya Ukumbi wa Bunge mara baada ya kikao, Mjini Dodoma.
6
Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia Mhe.January Makamba (kulia)pamoja na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mhe.Zitto Kabwe(kushoto) wakifurahi pamoja na Walimu na Wanafunzi kutoka Shule ya Msingi ya Dar es Salaam Independent nje ya Bunge mara baada ya kikao cha bunge, leo tarehe 18/03/2015 Mjini Dodoma.
7
Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe.Aggrey Mwanri akijibu swali la Mhe. Dkt Festus Limbu Mbunge wa Magu,lilikuwa likihoji ni kiasi gani cha kodi ya Majengo kimekusanya katika kipindi cha miaka mine na nusu ya kwanza ya mwaka wa fedha wa 2014/2015.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »