Wawakilishi
wa Shirika la Umoja wa wamachinga Tanzania SHIUMA,pamoja na viongozi wa
UVCCM kata za jiji la Mwanza wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri
Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa nyumbani
kwake Ngarash Monduli mwishoni mwa wiki mara baada ya kumkabidhi mchango
wa shilingi milioni moja ili achukue fomu kuwania urais kupitia CCM.Pia
walimkabidhi Ngao na mkuki atakavyotumia katika safari yake ya
matumaini.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akionesha
kitambulisho cha uanachama wa shirikisho la Umoja wa wamachinga
Tanzania (SHIUMA) baada ya kukabidhiwa na uongozi wa shirikisho hilo
mwishoni mwa wiki huko Monduli.Pia alikabidhiwa shilingi milioni moja na
ombi la kumtaka achukue fomu kuwania urais kupitia CCM.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akihesabu
Fedha kiasi cha Shilingi Milioni 1, alizopewa na Shirika la Umoja wa
Wamachinga Tanzania pamoja na Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) kata za
jiji la Mwanza ili achukue fomu kuwania urais.