KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AFANYA ZIARA MTERA KWA LUSINDE A.K.A (MTALIMBO)

March 10, 2015

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Manzase kata ya Fufu  jimbo la Mtera wilayani Chamwino, Katika mkutano huo Kinana amewaahidi wananchi hao kushughulikia matatizo ya maji, Umeme , Huduma za Afya na Mawasiliano kwa kushirikiana na Mbunge wa jimbo hilo Mh. Livingstone Lusinde na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mh. Chiku Galawa.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa Manzase na kuwaambia CCM Ipo Imara inajenga nchi na kuwataadharisha vijana wasikimbilie vyama visivyo na sera za maendeleo. 3 
Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde akihutubia wakazi wa Manzase ambapo aliwaambia kuwa watendaji wa Serikali wajitahidi kufuata maagizo na maelekezo ya Mheshimiwa Rais Kikwete kwa wakati. 4 
Mkuu wa wilaya ya Chamwino Bi. Farida Mgomi akiwasalimia wananchi. 7 
Umati wa wananchi wakisubiri mkutano huo kuanza  8 
Mbunge wa jimbo la Mtera Mh. Livingstone Lusinde akizungumza, huku Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza wakati alipotembelea  Kijiji cha Suli, kata ya Mvumi Makulu ambapo alijionea ujenzi wa shule ya Msingi Suli unavyoendelea ikiwa ni msaada wa Shirika la Maendelea la Korea (KOICA) wanaofurahia hotuba ya mbunge huyo kutoka kulia ni Mh. Chiku Galawa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM. 10 
Baadhi ya wajumbe wakiwa katika mkutano huo wa ndani ambao umefanyika eneo la shule ya sekondari ya Mvumi Mission. 13 
Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde akihutubia wajumbe wa mkutano mkuu wa jimbo la Mtera. 14 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi kabla ya kuzindua kisima cha maji ambapo aliwaambia wananchi hao watunze  sana miundo mbinu ya maji ili iendelee kudumu na kuwasaidia. 18 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa akina mama huku Mbunge wa jimbo la Mtera Mh. Livingstone Lusinde akishiriki  kupampu maji ya kisima cha mkono kilichopo katika shule ya msingi Mvumi Mission mara baada ya kukagua na kuuzindua mradi huo wa maji. 20 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde wakifurahia jambo mara baada ya kuvishwa Migorole kama heshima ya wazee wa kijiji cha Manzase kwa kutambua mchango wao kwa taifa na kijiji hicho kwa ujumla.
19

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »