Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika
mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Manzase kata ya Fufu
jimbo la Mtera wilayani Chamwino, Katika mkutano huo Kinana amewaahidi
wananchi hao kushughulikia matatizo ya maji, Umeme , Huduma za Afya na
Mawasiliano kwa kushirikiana na Mbunge wa jimbo hilo Mh. Livingstone
Lusinde na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mh. Chiku Galawa.
“Si sawa kabisa miradi yote ni agizo la Rais Jakaya Kikwete msiache
miradi mingine inakufa mking’ang’ania maabara tu, miradi yote ni muhimu
kwa wananchi na kama itakamilika wananchi hawa hawana tabu nina uhakika
tutabeba magunia ya kura huku” Mh. Livingstone Lusinde a.k.a Mtalimbo.
Aliongeza.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MTERA-DODOMA)
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa Manzase na
kuwaambia CCM Ipo Imara inajenga nchi na kuwataadharisha vijana
wasikimbilie vyama visivyo na sera za maendeleo.
Mbunge
wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde akihutubia wakazi wa
Manzase ambapo aliwaambia kuwa watendaji wa Serikali wajitahidi kufuata
maagizo na maelekezo ya Mheshimiwa Rais Kikwete kwa wakati.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimpongeza mbunge wa jimbo la Mtera Mh. Livingstone Lusinde mara baada ya kumaliza hotuba yake. Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Ndugu Adam Kimbisa akiwahutubia wananchi katika mkutano huo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua maendeleo ya ujenzi wa shule ya msingi Suli inayojengwa kwa msaada wa Korea.
Mbunge
wa jimbo la Mtera Mh. Livingstone Lusinde akizungumza, huku Katibu Mkuu
wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza wakati alipotembelea
Kijiji cha Suli, kata ya Mvumi Makulu ambapo alijionea ujenzi wa shule
ya Msingi Suli unavyoendelea ikiwa ni msaada wa Shirika la Maendelea la
Korea (KOICA) wanaofurahia hotuba ya mbunge huyo kutoka kulia ni Mh.
Chiku Galawa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi
na Uenezi CCM.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wajumbe wa Mkutano mkuu wa jimbo la Mtera.
Baadhi ya wajumbe wakiwa katika mkutano huo wa ndani ambao umefanyika eneo la shule ya sekondari ya Mvumi Mission.
Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde akihutubia wajumbe wa mkutano mkuu wa jimbo la Mtera.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda mti katika shule ya Sekondari ya FUFU ikiwa sehemu ya utunzaji mazingira.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na waalimu na wafanyakazi mbalimbali wa shule ya sekondari ya Mvumi Mission wakati alipowasili shuleni hapo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi kabla ya
kuzindua kisima cha maji ambapo aliwaambia wananchi hao watunze sana
miundo mbinu ya maji ili iendelee kudumu na kuwasaidia.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa
akina mama huku Mbunge wa jimbo la Mtera Mh. Livingstone Lusinde
akishiriki kupampu maji ya kisima cha mkono kilichopo katika shule ya
msingi Mvumi Mission mara baada ya kukagua na kuuzindua mradi huo wa
maji.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde wakifurahia
jambo mara baada ya kuvishwa Migorole kama heshima ya wazee wa kijiji
cha Manzase kwa kutambua mchango wao kwa taifa na kijiji hicho kwa
ujumla.