WAZIRI CHIKAWE AWAPA SOMO MAKATIBU KATA CCM NACHINGWEA, MKOANI LINDI

February 12, 2015

chik1 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kushoto) akizungumza na Makatibu Kata wa CCM, Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi leo. Katika mazungumzo hayo yaliyojumuisha Makatibu Kata zaidi ya 30, Waziri Chikawe aliwataka viongozi hao kuhakikisha wanazunguka katika kata zao kuhakikisha wanawahamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi kujiandikisha kwa ajili ya maandalizi ya kuipigia kura Katiba inayopendekezwa pamoja na Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika mwaka huu nchini. Katikati Meza Kuu ni Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Mussa Liliyo akifuatiwa na Mwenyekiti wa Makatibu Kata hao, Ally Napepa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, mkoani Lindi, Mathias Chikawe (kushoto) akimsikiliza kwa makini Katibu wa CCM Wilaya ya Nachingwea, Mussa Liliyo wakati alipokuwa akimwakikishia mbunge wao, kuwa timu ya Makatibu Kata wake wamejipanga kikamilivu katika kuwahamasisha wananchi jimboni humo kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwa ajili ya kuipiga kura Katiba iliyopendekezwa pamoja na Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika mwaka huu nchini. chik3 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, mkoani Lindi, Mathias Chikawe (wanne kushoto-mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Makatibu Kata wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jimboni humo baada ya kuwapa somo makatibu hao la kuhakikisha wanawahamasisha wananchi kujitokeze kwa wingi kujiandikisha kwa ajili ya kuipiga kura Katiba inayopendekezwa pamoja na Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika mwaka huu nchini. Picha zote na Felix Mwagara.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »