SHEKIFU:Mgeni rasmi Kilele cha Maadhimisho kuzaliwa Chama cha Mapinduzi wilayani Handeni”

February 01, 2015
MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga, Henry Shekifu anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha kuazimisha miaka 38 ya kuzaliwa chama hicho zitakazofanyika kimkoa wilayani Handeni leo mwaka huu.

Sherehe hizo kitaifa mwaka huu zinatarajiwa kufanyika Mkoani Ruvuma zinazoambatana na shughuli za kimaendeleo kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini.

Akizungumza na Tanga Raha Blog, Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga, Shijja Othumani alisema kuwa kabla ya kuelekea kilele hicho chama hicho kilianza kulifanya mambo mbalimbali ikiwemo kuwakutanisha vijana kwenye Kongamano pamoja na kuwapa uelewa juu ya umuhimu wa katiba inayopendekezwa.

Shijja alisema kuwa shughuli nyengine za kijamii zilizofanyika ni pamoja na jumuiya ya wazazi kutembelea wagonjwa kwenye vituo mbalimbali vya afya kwa lengo la kuwafariji

Alisema kuwa licha ya kufanya hivyo lakini Jumuiya ya Wanawake ya Chama hicho mkoa wa Tanga(UWT) walifanya mikutano ya hadhara kuwaeleza wananchi masuala mbalimbali ya kufanya ili kuweza kujikwamua kiuchumi.

Hata hivyo alisema kuwa shughuli zilizofanywa zimeongeza uzalendo miongozi mwa washiriki ambao wanaweza kuwa chachu ya maendeleo kwa wengine katika kuhakikisha kazi za ujenzi wa taifa zinafanyika.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »

EmoticonEmoticon

:)
:(
=(
^_^
:D
=D
=)D
|o|
@@,
;)
:-bd
:-d
:p
:ng