Mkuu wa Wilaya ya Wete hayuko tayari kufanya kazi na asasi za kiraia zenye mlengo wa siasa

February 04, 2015
ime
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akimuapisha Bw. Hassan Khatib Hassan kuwa  Mkuu wa Wilaya ya Wete Pemba  katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar.
……………………………………………………………………………………
Na Masanja Mabula -Pemba  .
Mkuu wa Wilaya ya Wete Hassan Khatib Hassan amesema kuwa hatakuwa tayari kufanya kazi na asasi za kiraia ambazo zitakuwa zinafanya kazi kwa mlengwa wa chama cha siasa kwani hazitakuwa na mwelekeo mzuri .
Akizungumza na Uongozi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Jimbo la Mtabwe waliofika  Ofisini kwake kujitabulisha , amesema kuwa siasa ni sumu ya mafanikio ya Jumuiya na kwamba Jumuiya nyingi zimekuwa zikishindwa kufikia malengo yake kutokana na Viongozi kuzihusisha na masuala ya kisiasa .
Aidha Mkuu wa Wilaya ameelezea kusikitishwa na kitendo cha uharibifu wa mazingira katika Jimbo hilo hasa vitendo vya ukataji wa miti na kuitaka Jumuiya hiyo kuhakikisha kuwa maeneo ya wazi ambayo yameathirika kwa kukatwa miti ovyo yanarejeshwa katika hadhi yake kwa kupandwa miti
Amefahamishwa  kuwa asasi ya kiraia zina nafasi kubwa katika kufanikisha udhibiti wa uharibifu wa mazingira unaotokana na mabadiliko ya Tabianchi iwapo zitakuwa tayari kutoa elimu kwa jamii inayowazunguka.
Amesema kuwa katika kufanikisha suala la uhifadhi na udhibiti wa uharibifu wa mazingira kutokana na ukataji ovyo wa miti asasi za kiraia zinatakiwa kuwa mstari wambele kuwaelimisha wananchi athari za mabadiliko ya Tabianchi yanayotokea siku hadi siku. . Mkuu huyo wa Wilaya amesisitiza haja kwa Jumuiya hiyo kukaa pampja na asasi nyingine ambazo zinafanya kazi sawa na Jumuiya hiyo ili kuondoa suala la migongano katika utendaji wa kazi zao .
“Tunatambua kwamba asasi za kiraia zinanafasi kubwa katika kudhibiti suala la yharibifu wa mazingira na mafanikio zaidi yatapatikana iwapo mtakuwa tayari kushirikiana na Jumuiya nyingine ambazo zina malengo sawa na ya Jumuiya yenu ” alifahamisha .
Naye Diwani wa Wadi ya Mtambwe Hamad Mjaka  Bakar amesema kuwa lengo Jumiya hiyo ni kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira pamoja na kutafuta njia muafaka za  kutatua kero zianazo wakabili wananchi wa Jimbo hilo  .
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Jimbo hilo Said Massoud amesema kuwa uharibifu mkubwa wa mazingira unaotokea katika Jimbo hilo ni ukataji ovyo wa miti pamoja na  uvuvi wa chaza wa kutumia vijembe .
Amesema kuwa uvuvi wa aina hii umekuwa ukichangia sana matendo ya uharibifu wa mazingira na kuongeza kwamba Jumuiya tayari inaendelea na kampeni zake za utoaji wa elimu kwa wananchi ili kudhibiti vitendo hivyo .
“Vitendo hivi ni lazima tukiri kwamba vipo katika Jimbo letu la Mtambwe na hasa  vya ukataji miti ovyo pamoja uvuvi wa chaza kwa kutumia vijenmb vidogo vidogo na hili tunaendelea kupambana nalo na muda mfupi wananchi wataepukana nalo ” alieleza.
Hivyo Jumuiya hiyo imeiomba Serikali kuweka msukumo katika kufanikisha kuyadhibiti matendo hayo kwa kuwahakikisha kwamba wanaosafirisha miti mibichi wanachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria .

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »