Urembo:
Mrembo na mwigizaji wa filamu za kibongo, Diana Elizabeth Michael
‘Lulu’ hivi majuzi alitupia picha yake ya zamani mtandaoni (hiyo hapo
juu) ikiwa kama ni “ThrowBackThursday” (TBT) yake, na kuiandikia mameno
haya;
“Let me ThrowitBack ,Shikana Mama, Enzi ZaUjanaSijawahi kuwa mweusi lol..! Rangi Ya Mtume Nimezaliwa Nayo”
Wengi walimsifu na kumpongeza Lulu kwa kuweza kuitunza ngozi yake
kwakutupia “comments” na kugonga “likes” za kutosha kwenye picha hiyo,
kwani anaonekana kuwa hatumii madawa/vipodozi ya kujichubua kama wadada
wengi wa siku hizi hutumia madawa/vipodozi ili kubadili rangi za ngozi
zao.
Jiwe gizani, wewe je hautumii? Hata wakaka nao nasikia wamo!