Mwanamuziki
maarufu nchini na sehemu nyingi za dunia – Diamond Platnumz ambaye
aliwahi kuwa mpenzi wa mwanadada Wema Sepetu ameendelea kuuhakikishia
ulimwengu kuwa, mpenzi wake wa sasa ZARI al-maarufu kama “The boss
lady”, ni mama mtarajiwa aliyebeba ujauzito wa msanii huyo nguli nchini
na kwamba hii sio project nyingine.
Huku akitumia mafumbo kwenye maneno yake ambayo wataalamu wetu
wa Kiswahili ndio wametufafanulia kisanifu zaidi, Diamond aliandika
“Kileeeeeeee kinaanza kumuharibia mtu Mavazi..”
huku akiweka picha yake na mpenzi wake huyo wakitoka kwenye show
ya miaka 38 ya CCM huko songea. Baada ya kukaa chini vizuri na
wataalamu wetu hawa wa fasihi , walituhakikishia kuwa “Kileeeee”
katika sentensi hiyo sio kitu kingine bali ni ujauzito alionao mrembo
huyo na mara nyingi ukichunguza ndio kitu kinachomuharibia mwanadada au
yoyote mavazi kirahisi hasa “kinapoanza” kuwa kikubwa.
Kweli tumeamini lazima ujue tofauti ya msalaba na kujumlisha.
|