WANAWAKE TANGA TISHIO % 50 KWA 50

November 06, 2014

ALIYEKUWA MKUU WA MKOA TANGA LUTENI (MSTAAFU) CHIKU GHALAWA KATIKA MOJA YA VIKAO MKOANI HAPA AMBAYE KWA SASA AMEHAMISHIWA MKOA WA DODOMA

WANAWAKE Mkoani hapa wametakiwa kuwa sehemu ya kukua kwa uchumi wa Taifa, na kuunga mkono dira ya Taifa 2025, MKUKUTA na Malengo ya milenia kwa kufanya biashara na ujasiriamali wenye tija zitakaz waongezea kipato.

Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 ilianzwa kutekelezwa mwaka 2000 ili kuongoza harakati za maendeleo ya uchumi na jamii zitakazoiwezesha Tanzania kufikia hadhi ya nchi yenye kipato cha kati na kuondoana na umaskini uliokithiri.

Malengo ni kuboresha hali za maisha ya watanzania, kuwepo kwa kwa mazingira ya amani, usalama na umoja, Kujenga utawala bora, kuwepo na jamii inayoelimika vyema na inayojifunza; na Kujenga uchumi imara unaoweza kukabiliana na ushindani kutoka nchi nyingine.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Luteni (mstaafu) Chiku Ghalawa alipokuwa akifugua kampeni ya Wanawake na Uchumi kwenye ukumbi wa Naivera Compex, eneo la Bombo Mkoani hapa.

Amesema kwa muda mrefu uchumi wa nchi umeongozwa na wakulima na wafanyakazi na kwamba wakati kwa wajasiriamali na wafanyabiashara ni sasa kuwa wachangiaji wakubwa wa pato la Taifa.

Kampeni hiyo imeandaliwa na asasi isiyo ya kiserikali ya Angels Moment kwa kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa lengo la kuwaonyesha wanawake kuwa si kila changamoto inaashiria kurudisha nyuma juhudi zao  bali ni firsa ya kusonga mbele kwa kuanzisha mpya yenye ushindani.

Awali Mkurugenzi wa Kampeni ya Wanawake na Uchumi, Mahada Erick amesema pamoja na juhudi nyingi za kumkomboa mwanamke mjasiriamali bado ameendelea kukumbana na changamoto zilezile kila siku hali inayosababisha wengine kukwepa biashara na ujasiriamali kwa kuogopa matokeo ya waliotangulia kushindwa.

Licha ya changamoto hizo Mkuu wa Mkoa wa Tanga amewatia moyo wanawake walioudhuria hafla hiyo wapatao 300 kuwa halmashauri ya Jiji la Tanga imetenga asilimia 10 ya pato lake kuwanufaisha pamoja na vijana huku akiwasisitizia wasiwaache kinababa nyuma kwani baadhi yao mkoani hapa hawajishughulishi jambo ambalo ni fedheha na kugusia maandiko yanayosema asiye fanya kazi na asile.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »