WIKI YA MAJANGA KWA VIGOGO "NIGERIA HOI KWA SUDAN.STARS YABUIRUZA BENIN 4-1"

October 13, 2014


BINGWA MTETEZI WA AFCON (NIGERIA) AMEAIBISHWA NA SUDAN KWA KUCHAPWA GOLI 1-


Bingwa mtetezi wa kombe la mataifa ya Afrika (AFCON), Nigeria, jana ameonja joto la jiwe baada ya kujikuta wakibanwa mbavu na Sudan kwa kuchapwa goli 1-0. Goli hili linaifanya timu ya taifa ya Nigeria chini kocha wa Stephene Keshi kuburuza mkia katika kundi lao lenye timu za Congo Brazaville na Afrika Kusini.

Sudan walipata goli la kwanza na la ushindi mnamo dakika za mwisha wa kipindi cha kwanza ya mpepetano huo kupitia mshambuliaji wao, Bakri Almadina

STARS YAMSHIKISHA ADABU BENIN KWA KUMCHARAZA MAGOLI 4-1 KAMA VILE WALIKUWA WAMESIMAMA


Nahodha wa Stars "Nadir Haroub Cannavaro (kushoto)akishangilia bao lake na Beki wa timu hiyo Oscar Joshua

Watu wengi walikuwa wakiibeza sana Stars kuelekea katika mchezo wa jana dhidi ya Benin, lakini ndiyo hivyo Wahenga walisema, "mdharau mwiba, mguu huota tende" na ndicho kilichowakuta Wa Benin leo katika dimba la taifa licha ya kusheheni nyota wengi wanaocheza soka la kulipwa barani Ulaya kama vile, Stephane Sesegnon anayekipa kunako West Bromwich Albion. 


Magoli ya Stars yalifungwa na beki Haroub Canavaro, Amri Kiemba, Thomas Ulimwengu, pamoja naye Juma Luizio. Goli la kufutia kijasho la Benin Lilifungwa na mshambuliaji Sadel akipokea pasi maridadi kutoka kwake kiungo mshambuliaji, Stephane Sesegnon dakika ya 90 ya mchezo huo.
Ushindi huo ni furaha kubwa kwa watanzania ambao walikuwa wamekata tamaa na timu yao ya taifa iliyopo chini ya kocho Mholanzi Mart Nooij kufuatia matokeo mabovu ya hivi karibuni katika michuano ya kuwania tiketi za kupangwa katika makundi ya michuano ya AFCON yatakayo fanyika mwakani nchini Moroco.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »