TPDC, KAMPUNI ZA WENTWORTH, MAUREL & PROM WASAINI MKATABA WA KUUZIANA GESI

September 12, 2014


1 (18) 
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (wa nne kushoto)  akipeana mkono na  Mkurugenzi Mtendaji wa  Kampuni ya  WENTWORTH  inayochimba gesi katika eneo la Mnazi Bay Mkoani Mtwara , Robert MacBean (wa tatu kushoto) mara baada ya kusaini Makubaliano ya Mkataba wa Kuuziana Gesi kati yake na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC). Wengine katika picha ni baadhi wa Watendaji Wakuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la maendeleo ya Petroli Tanzania TPDC na wawakilishi wa kampuni za WENTWORTH na MAUREL & PROM.
3 (12) 
Wajumbe waliohudhuria kikao cha Kusaini Mkataba wa Kuuziana Gesi kati ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), na Kampuni zinazochimba gesi katika eneo la Mnazi Bay Mkoani Mtwara za WENTWORTH Resources Limited na MAUREL & PROM wakisaini MKataba huo. Anayeshuhudia mbele ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo pamoja na wawakilishi wengine kutoka kampuni hizo, TPDC, Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Kampuni zinazochimba gesi katika eneo la Mnazi Bay Mkoani Mtwara za WENTWORTH Resources Limited na MAUREL & PROM zimesaini Mkataba wa Makubaliano wa kuuziana Gesi, ambapo kampuni hizo zitaingiza gesi hiyo katika visima vilivyopo Mnazi Bay Mtwara kwa ajili ya Mradi wa Bomba la Gesi.
Kikao hicho cha Makubaliano kimeongozwa na Waziri wa Nishati na Madini,  Profesa Sospeter Muhongo Wizarani ambapo Waziri Muhongo amesisitiza kuwa, Mkataba huo ni fursa nyingine ya Kiuchumi kwa Tanzania na kuongeza kuwa, Serikali imeazimia kuingia katika biashara ya gesi na hivyo imedhamiria  kufanya biashara yenye maslahi kwa taifa na iko makini katika usimamizi na utekelezaji wa biashara hiyo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »