SITTA AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA UONGOZI, BUNGE LA KATIBA KUANZA JUMANNE

August 04, 2014



Mwenyekiti wa Bunge Maalum Samuel Sita akiongoza kikao cha Kamati ya Uongozi cha Bunge hilo kilichokaa leo Jumatatu Agosti 4, 2014, kupanga ratiba ya Bunge hilo linaloanza  Jumanne, Agosti 5, 2014 mjini Dodoma. Bunge hilo linaanza baada ya kuahirishwa Aprili 25, mwaka huu, ambapo wajumbe wanaotoka vuguvugu la Umoja wa Katiba ya Wananchi wengi wao wakiwa ni wafuasi wa vyama vya upinzani, waligomea mchakato huo ambao ulikuwa umefikia hatua ya kupiga  kura ya kupitisha vipengele vilivyojadiliwa tayari kikubwa kikiwa ni muundo wa serikali. UKAWA inasisitiza kuwepo kwa muundo wa serikali tatu, wakati wajumbe wengine wengi wao wakiwa ni wale wa chama tawala CCM, wakiweka msimamo wa kuendelea na mfumo wa sasa wa serikali mbili.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »