PINDA AFANYA ZIARA FUPI JIJINI MWANZA

August 24, 2014

PG4A2820 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa mbele ya kaburi la Vedasto Kitwanga,mtoto wa Naibu Waziri Nishati na Madini, Charles Kitwanga (Wanne kulia)  wakati alipokwenda nyumbani kwa Naibu Waziri huyo  eneo la Usagara Mwanza August 23, 2014 kumpa pole kufuatia kifo cha mwanae . Wengine pichani ni mke wa Naibu Waziri huyo, Matrida   (wanne kushoto) na  kushoto kwa Waziri Mkuu ni binti yao, Agness Misoji Kitwanga  . Kulia ni  Katibu wa CCM wa Mkoa wa Mwanza, Joyce Masunga  na Watatu kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi, Erasto Ndikilo.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
 PG4A2872 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (kulia) baada ya kuwasili nyumbani kwa Naibu Waziri huyo, eneo la Usagara, nje kidogo ya jiji la Mwanza ambako alikwenda kumpa pole kufuatia kifo cha mwanae Vedastus Kitwanga kilichotokea hivi karibuni. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 PG4A2888 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akipigiwa magoti na Matrida Kitwanga (kulia) mke wa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (kulia) baada ya kuwasili nyumbani kwa Naibu Waziri huyo, eneo la Usagara, nje kidogo ya jiji la Mwanza ambako alikwenda kumpa pole kufuatia kifo cha mwanae Vedastus Kitwanga kilichotokea hivi karibuni. Katikati ni binti wa familia hiyo,Agnes Misoji Kitwanga.(Picha n Ofisi ya Waziri Mkuu)
PG4A2947 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na  wadau wa ujenzi wa jengo lenye Mnara wa kuongozea ndege katika  uwanja wa ndege wa Mwanza unaoboreshwa wakati alipofanya ziara ya kukagua maboresho ya uwanja huo August 23, 3024 Katikati ni Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dr. Charles Tizeba.(Picha na Ofisi ya Waziri MKuu) PG4A2951
PG4A2964 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua eneo  panapojengwa mnara wa kuongozea ndege kwenye uwanja wa Mwanza August 23, 3014. Kushoto kwake ni Waziri wa Uchukuzi, Dr. Charles Tizeba,(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) PG4A2972 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akisalimiana na baadhi  ya vibarua wanaofanyakazi ya ujenzi wa jengo lenye Mnara wa kuongozea ndege katika uwanja wa ndege wa  Mwanza baada ya kukagua ujenzi huo August 23, 2014.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) PG4A3009 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na   baadhi   ya vibarua wanaofanyakazi ya ujenzi wa jengo lenye Mnara wa kuongozea ndege katika uwanja wa ndege wa  Mwanza baada ya kukagua ujenzi huo August 23, 2014.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PG4A3034 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na vibarua wanaofanya kazi ya kupanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza wakati alipokagua upanuzi wa uwanja huo August 23, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) PG4A3111 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF), Eliud Sanga  (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarest Ndikilo baada ya kukagua ujenzi wa jengo la Soko la Kimataifa linalojengwa kwa ubia kati ya jiji la Mwanza na LAPF jijini humo August 23, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »