MEMBE AKUTANA NA WAZIRI MKUU WA UTURUKI

May 09, 2014

Waziri Mkuu wa Uturuki, Mhe. Recep Tayyip Erdogan (kulia) akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, Mhe. Bernard K. Membe (Mb). mazungumzo hayo yalifanyika katika Ofisi ya Waziri Mkuu mjini Ankara, Uturuki tarehe 08 Mei, 2014.
Mazungumzo yanaendelea kati ya Waziri Mkuu wa Uturuki (kulia) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania. Mwingine katika picha ni Bibi Victoria Mwakasege, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Waziri Membe kulia akishikana mkono na Waziri Mkuu wa Uturuki mara baada ya viongozi hao kumaliza mazungumzo. 
Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa aliyevaa shati la njano kulia ukiwa katika mazungumzo na ujumbe wa Uturuki unaongozwa na Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Emrullah Isler wa tatu kutoka kushoto. 
Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Bernard K. Membe akipokea zawadi kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu wa Uturuki
Waziri Membe naye akimpa zawadi ya kinyago Naibu Waziri Mkuu wa Uturuki 
Mhe. Membe na Naibu Waziri Mkuu wa Uturuki wakijadili suala baada ya zoezi la kukabidhiana zawadi kukamilika Mazungumzo ya Waziri Membe na Wazri wa Mambo ya Nje wa Uturuki
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe wa tatu kutoka kushoto na ujumbe wakijadili masuala mbalimbali kuhusu ushirikiano na Uutruki na ujumbe wa Uturuki unaonekana katika picha ya chini.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mhe. Almet Dovutoglu wa pili kutoka kulia akiwa na ujumbe wake wakati wa mazungumzo na Mhe. Membe. Mkutano na Waandishi wa Habari
Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Mhe. Bernard K. Membe akihutubia Mkutano wa Waandishi wa Habari huku akimshika mkono Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mhe. Almet Dovutoglu
Waziri Membe akiendelea kuwahutubia waandishi wa habari hawapo pichani Mapokezi ya Mhe. Membe nchini Uturuki
Waziri Membe akipeana mikono na watu waliofika Uwanja wa Ndege wa Ankara kumpokea
Waziri Membe kushoto akibadilishana mawazo na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania katika Chumba cha Wageni Maalum kwenye Uwanja wa Ndege wa Ankara
Waziri Membe akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Italia ambaye pia anawakilisha Uturuki aliyekaa kushoto pamoja na Bw. Salvator Mbilinyi, Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Italia aliyechutama wakibadilishana machache katika Chumba cha Wageni Maalum ndani ya Uwanja wa Ndege wa Ankara.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe akisalimiana na Naibu Meya wa jiji la Ankara ambaye naye alikuja Uwanja wa Ndege kumlaki
Naibu Meya wa jiji la Ankara aliyeketi kushoto akibadilishana mawazo na Mhe. Membe kabala ya kuondoka kutoka katika kiwanja hicho
Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania, Bw. Frank Muhina akiwa kazini kunukuu mambo mbalimbali kutoka kwa Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki.  

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »